PEREIRA AANZA KWA KISHINDO FOREST IKIICHANA FENERBAHÇE

Kocha mkuu wa Nottingham Forest Vitor Pereira alianza kwa kishindo katika klabu hiyo kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Fenerbahçe katika mkondo wa kwanza wa mwondoano wa dimba la Europa League jana usiku, nao Stuttgart wakiilaza Celtic mbao 4-1. Pereira aliteuliwa kuwa mkufunzi wa 4 wa Forest msimu huu baada ya kukubali kutia Saini […]

UBAGUZI WA RANGI: REAL MADRID YAWASILISHA USHAHIDI UEFA

Miamba wa soka barani Ulaya Real Madrid wamesema kuwa wamewasilisha walichotaja kama ushahidi wote uliopo kwa shirikisho la UEFA kuunga mkono mlalamishi ya nyota wao raia wa Brazil Vinicius Junior kuhuus ya ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya mkondo wa kwanzaywa awamu ya mwondoano ya klabu bingwa barani Ulaya dhidi ya Benfica. Mechi hiyo […]

LIGI YA KPL YAINGIA WIKI YA 21

Ligi kuu ya soka nchini, KPL, inaingia wiki ya 21 wikendi hii huku viongozi Gor Mahia wakishikilia Kikiki usukani wa ligi hiyo wakilenga ubingwa wa 22. Green Commandos wanaongoza ligi hiyo na pointi 43 baada ya kusakata mechi 20, wakifuatiwa na mahasimu wao AFC Leopards walio na pointi 37 ingawa wana mechi moja mkononi, nao […]

AFCON 2027: WABUNGE WAPINGA PENDEKEZO LA KUONGEZA BAJETI

Kamati ya michezo katika bunge la kitaifa imekatalia mbali pendekezo la wizara ya michezo kutaka mgao wa bajeti ya maandalizi ya kombe la taifa bingwa barani Afrika AFCON 2027 uongezwe. Haya yanajiri licha ya kuibuka kwamba Kenya haijalipa ada yake ya lazima ya shilingi bilioni 3.5 zinazohitajika ili kuwa mwenyeji wa dimba hilo. Chini ya […]

KAMATI YA ELIMU YATOA AGIZO KWA TSC

Kamati ya elimu katika bunge la kitaifa imeitaka tume ya kuwaajiri walimu TSC kuhakikisha kuwa watahaniwa wote waliokamilisha masomo ya shule za msingi na upili wanapewa vyeti vyao mara moja bila kuzingatia iwapo wana madeni ya karo au la. Mwenyekiti wa kamati hiyo Julius Melly, akizungumza kwenye kikao cha kupokea sera za bajeti za wizara […]

UPINZANI WATISHIA MASHTAKA BINAFSI DHIDI YA POLISI 12

Muungano wa upinzani umefutilia mbali mikutano yake na Inspekta mkuu wa Polisi Douglas Kanja, na badala yake utawafungulia mashtaka ya jinai maafisa 12 wa polisi na wabunge wawili kutoka kaunti za Murang’a na Nyeri kuhusiana na uvamizi dhidi ya kanisa moja wakati wa ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua katika kaunti ya […]

CHARLES KANJAMA RAIS MPYA LSK

Jumbe za kongole zimeendelea kumiminika kufuatia ushindi wa wakili Charles Kanjama kwenye uchaguzi wa urais wa chama cha wanasheria nchini LSK, ili kuchukua usukani kutoka kwa rais anayeondoka Faith Odhiambo. Miongoni mwa waliompongeza kwa ushindi wa uchaguzi uliofanywa hapo jana ni kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, Waziri wa afya Aden Duale, Odhiambo na aliyekuwa mshindani […]

URUSI YAKANA KUWASAFIRISHA WAKENYA VITANI

Ubalozi wa Urusi humu nchini umejitenga na ripoti ya uchunguzi wa idara ya ujasusi NIS na ile ya upelelezi wa jinai DCI iliyouhusisha ubaliozi huo na madai ya kuwasafirisha wakenya kisiri kupigana katika vita kati ya Urusi na Ukraine. Kupitia taarifa, ubalozi huo umesema kuwa ripoti hiyo si ya kweli, na kwamba haujakuwa ukitoa stakabadhi […]

SZOBOSZLAI APENDEKEZWA NA VAN DIJK KUWA NAHODHA WA LIVERPOOL

Virgil van Dijk amependekeza kuwa Dominik Szoboszlai anaweza kumrithi kama nahodha wa Liverpool, akimuelezea kama kiongozi anayefaa kwa timu. Szoboszlai amekuwa mchezaji muhimu msimu huu mgumu kwa mabingwa wa Ligi Kuu, akionyesha ujuzi wa kucheza nafasi mbalimbali ikiwa ni pamoja na beki wa kulia. Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah, amemsifu Szoboszlai kama moja ya wachezaji bora […]

KENYA YALENGA USHINDI KATIKA MBIO ZA 3,000M

Kenya inashirikirisha kikosi chenye nguvu katika mbio za mita 3,000 za Hauts-de-France Indoor ikiwa na wanariadha watatu wa kiwango cha dunia wakilenga kuonyesha ubora wao. Kikosi hicho kinaongozwa na Jacob Krop, mshindi wa fedha wa mita 5,000 katika mashindano ya dunia 2022, pamoja na Frankline Kibet, bingwa wa Dunia wa Cross Country Under-20, na Edwin Kurgat, […]