GOR WAREJESHA UONGOZI WA POINTI 6 KILELENI

Miamba wa soka nchini Gor Mahia walirejesha uongozi wa pointi 6 kileleni mwa jedwali la ligi kuu ya soka nchini, KPL, kufuatia ushindi wao wa mabao 3-0 dhidi ya wanabenki wa KCB. Ushindi wa Green Commandos ukijiri baada ya AFC Leopards kupunguza mwanya wa pointi kwa kuwachabanga Posta Rangers 2-1, uliihakikishia Gor mfululizo wa mechi […]

KENYA ARMY YAITIA PRISONS GEREZANI KVF

Mkondo wa pili wa ligi ya voliboli ya wanaume ulipamba moto katika siku ya 4 uwanjani Kasarani Indoor Arena hapo jana, timu zikijizatiti kuandikisha matokeo ya kuridhisha. Katika tukio moja, Prisons Nairobi waliipepeta Eldoret Water seti 3-2, kabla ya Kenya Army kutamatisha msururu wa ushindi wa Kenya Prisons kwa kichapo cha seti 3-0. Kabla ya […]

OWINO AMLAUMU OMOLLO KWA VURUGU KISUMU

Mbunge wa Embakasi East Babu Owino amemshutumu katibu mkuu katika wizara ya usalama wa kitaifa Raymond Omollo kwa madai ya kufadhili vurugu zilizoshuhudiwa dhidi ya viongozi wa upinzani katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Kisumu. Kwenye mahojiano na shirika moja la habari nchini, Owino amedai kwamba zaidi ya watu 200 walipangwa kuwashambulia uwanjani humo […]

SERIKALI: UPINZANI UNAJIRUSHIA VITOZA MACHOZI

Serikali imeibua madai kwamba viongozi wa upinzani wamekuwa wakipanga vurugu kwenye mikutano yao kwa lengo la kuvutia huruma kutoka kwa wananchi ili wapate uungwaji mkono, hatua ambayo serikali inasema itakabiliana nayo kisheria. Akizungumza siku moja baada ya mkutano wa viongozi hao kaunti ya Kakamega kutatizwa kwa vitoza machozi, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, […]

DCI YACHUNGUZA VURUGU ZA MBALE

Idara ya upelelezi wa jinai DCI imeanzisha uchunguzi katika tukio la vurugu baina ya makundi mawili hasimu zilizoshuhudiwa mjini Mbale kaunti ya Vihiga wakati wa mkutano ulioongozwa na katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna, na kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyetambuliwa kama George Otobe, mkazi wa Kisumu. Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa Otobe alimdunga mtu […]

WANDANI WA KINDIKI WATETEA ‘TONGE’ 

Mjadala kuhusu ni nani atakayekuwa naibu rais wa Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu ujao umeendelea kushika kasi huku wandani wa naibu Rais wa sasa Kithure Kindiki wakisisitiza kuwa wadhifa huo hautapokonywa Kindiki. Wakizungumza kwenye mkutano mjini Embu wakiwa wameandamana na Kindiki, wandani hao wamemtaka kinara wa ODM Oburu Oginga kukoma kukimezea mate kiti hicho. […]

UPINZANI WAKOSOA ‘UTEPETEVU’ NPS

Muungano wa upinzani umeikosoa serikali kwa madai ya kuruhusu polisi kutumia nguvu kupita kiasi, mbali na njama ya kuwaficha maafisa wa polisi wanaokiuka sheria wanapokuwa kazini. Wakiongozwa na aliyekuwa Waziri wa usalama wa kitaifa Fred Matiang’i, viongozi wa muungano huo wameshutumu vuta nikuvute iliyoshuhudiwa nje ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kisumu, na kuwataka […]

KINOTI KIARA AIPA KENYA UBINGWA WA AFRIKA

Kijana wa Kenya Kinoti Kiara ameipa nchi sababu ya kusherehekea baada ya kutwaa ubingwa katika Mashindano ya Afrika ya Cadet na Junior ya mchezo wa upanga yaliyofanyika jijini Dakar, Senegal. Akiwania dhidi ya vijana wenye vipaji vikubwa barani Afrika, Kiara alionyesha utulivu wa hali ya juu, akicheza kwa nidhamu, kuimarisha safu ya ulinzi na kushambulia […]

AMBANI AONYESHA IMANI KATIKA MBIO ZA UBINGWA

Kocha mkuu wa AFC Leopards, Fred Ambani, amesema bado ana imani kikosi chake kina uwezo na ari ya kuwasaka wapinzani wao wakuu Gor Mahia katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya FKF. Kadri msimu unavyoingia hatua ya maamuzi, Ambani amesema wiki zijazo si mzigo kwa timu yake bali ni fursa ya kuonyesha uthabiti, nidhamu […]

ODONGO ATAJA MAENEO YA KUBORESHA KWA LIONESSES

Kocha wa muda wa timu ya taifa ya raga ya wanawake, Kenya Lionesses, Simon Odongo, ametaja mapokezi ya mpira wakati wa kuanza mchezo na maamuzi uwanjani kuwa maeneo yanayohitaji kuboreshwa kabla ya duru ijayo ya World Rugby Sevens Challenger Series itakayofanyika Uruguay mwezi ujao. Odongo alizungumza baada ya tathmini ya kina ya mashindano ya Divisheni […]