WAFCON 2026 YAAHIRISHWA

Dimba la taifa bingwa barani Afrika la wanawake mwaka huu, WAFCON 2026 limeahirishwa, zikiwa zimesalia siku 11 kabla ya tarehe iliyokuwa imeratibiwa kuanza kwa mashindano hayo. Kupitia taarifa, shirikisho la soka barani Afrika, CAF, limesema Makala ya mwaka huu yataandaliwa mwezi Julai kutokana na kile ambacho limetaja kwamba sababu zisizoweza kutabirika. Makala ya mwaka huu […]

MIRADI ITAKAYOFADHILIWA NA HAZINA YA MIUNDOMBINU…

Bunge la kitaifa limefafanua miradi itakayofadhiliwa na hazina ya kitaifa ya miundombinu ya shilingi trilioni 5, likisema ni miradi mikuu kama vile barabara kuu za kitaifa, miundombinu ya reli, viwanja vya ndege, bandari, uzalishaji wa umeme na na usambazaji. Hii ni kufuatia kupitishwa kwa mswada wa hazina hiyo hapo jana baada ya marekebisho kadhaa, afisi […]

DUALE: SHA INAWAHUDUMIA WALIMU

Waziri wa afya Aden Duale amekana kuwepo kwa changamoto kubwa kwa walimu kupata matibabu chini ya bima ya afya SHA, akisisitiza kuwa walimu zaidi ya 249,000 na watu wengine wanaowategemea wakiwemo Watoto wa walimu hao wametibiwa chini ya bima hiyo. Duale amehakikisha kuwa changamoto za awali katika utekelezaji wa mpango huo zinaendelea kushughulikiwa ili kufanikisha […]

BUNGE LAIMARISHA UANGALIZI WA HAZINA MPYA

Bunge limewaondolea wakenya hofu ya fedha za hazina mpya ya miundombinu kufujwa kutokana na muundo wake wa awali, baada ya kuidhinisha kubuniwa kwa baraza litakalosimamia hazina hiyo. Kwa mujibu wa mswada wa hazina hiyo, baraza hilo litamjumuisha Waziri wa fedha, gavana wa Benki Kuu ya Kenya, mwanasheria mkuu wa serikali, na wanachama wengine 6 wasio […]

EACC YAINUA MJELEDI

Tume ya maadili na kukabili ufisadi, EACC, imewataka makatibu wakuu katika wizara zote na maafisa wengine wakuu serikalini kujiepusha na kampeni za kisiasa jinsi wanavyohitajika kisheria. Tume hiyo imeonya kuwachukulia hatua za kisheria maafisa watakaokiuka sheria hiyo, onyo yao ikijiri huku makatibu wakuu na maafisa wengine wakionekana hadharani kwenye mikutano ya kisiasa na kufanya kampeni. […]

SERIKALI YAKADIRIA UKUAJI WA UCHUMI

Uchumi wa taifa unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.3 mwaka huu wa 2026 kutoka asilimia 4.7 mwaka 2024 huku serikali ikiendeleza mikakati ya kuimarisha udhabiti wa uchumi, kuongeza ukusanyaji wa mapato ya taifa na kukuza sekta muhimu. Akiwa mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu bajeti, Waziri wa fedha John Mbadi, amesema shilingi trilioni 3.45 […]

RUTO APOKEA MABALOZI WATATU NCHINI

Rais William Ruto amepokea hati za utambulisho za mabalo watatu ambao wameteuliwa katika Ikulu ya Nairobi ikiwa ni kuashiria mwanzo wa kazi zao za kidiplomasia nchini. Watatu hao ni pamoja na Rulan Mahmoud Samara wa Jordan, Jacinto Januario Maguni wa Mozambique na Saad Bin Abdullah Alnofaia wa Saudi Arabia. Ruto amewahakikishia mabalozi hao ushirikiano kamili […]

HISA ZA UUZAJI WA KPC ZILIIPA KENYA $ 829 M, RIPOTI 

Kenya imekusanya shilingi bilioni 106.3 kutokana na ofa ya awali ya umma (IPO) ya Kampuni ya Mabomba ya Kenya (KPC), baada ya mauzo hayo kupata asilimia 105.7 ya usajili ukiongozwa na wawekezaji wa taasisi za kikanda na za ndani ya nchi. Ofa hiyo, ambayo ni ubinafsishaji mkubwa zaidi wa Kenya katika karibu miongo miwili, ilivutia ushiriki […]

ARSENAL YAKARIBIA TAJI EPL, CITY WAYUMBA

Timu ya Arsenal imekaribia ubingwa wa taji la ligi kuu ya soka nchini Uingereza, EPL, kufuatia ushindi wao mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Brighton ugani Amex, huku wapinzani wao wa karibu Manchester City wakidondosha pointi 2 muhimu, walipoandikisha sare ya mabao 2-2 nyumbani dhidi ya Nottingham Forest. Katika mtindo wa ubingwa, Bukayo Saka aliwapa […]

MATANO AKOSOA USIMAMIZI, WACHEZAJI WAKE

Kocha mkuu wa klabu ya KCB Robert Matano, amewalaumu wasimamizi wa mechi ya jana kati ya timu hiyo na Nairobi United ambako timu yake ilishindwa kupata pointi 3 muhimu, akisema mwamuzi aliwapa Naibois penalti isiyofaa. Kwenye kikao na wanahabari baada ya mechi hiyo iliyoishia sare ya bao 1-1, amesema hali hiyo iliwanyima vijana wake ushindi […]