11 KUSHTAKIWA KUHUSIANA NA MAANDAMANO

Waandamanaji 11 waliokamatwa jana na polisi jijini Nairobi wakati wa maandamano ya kupinga bei mpya za juu za mafuta wanatarajiwa kufukishwa mahakamani hii leo. 11 hao walikamatwa na maafisa wa DCI waliokuwa wamevalia mavazi ya raia, kamanda wa polisi eneo la Nairobi Issa Mohamud akithibitisha kukamatwa huko. Miongoni mwa waliokamatwa ni mwanaharakati Julius Kamau. Imetayarishwa […]

MURKOMEN: KUNA MAELFU YA WAHUNI NCHINI

Imebainika kwamba kuna magenge 100 yenye maelfu ya wanachama ambayo yanaendelea kuvuruga mikutano ya kisiasa nchini, serikali ikidai magenge hayo yanafadhiliwa na baadhi ya wanasiasa. Akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu usalama, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, ameilaumu idara ya mahakama kutokana na ongezeko la uhuni, akisema idara hiyo imelegeza masharti. Aidha, […]

IEBC YASISITIZA MUDA WA USAJILI HAUTAONGEZWA

Huku zoezi linaloendelea la usajili wa wapiga kura wapya likikaribia kutamatika, tume huru ya uchaguzi na mipaka imepuzilia mbali uwezekano wa kuongeza muda wa usajili, ikisisitiza kuwa zoezi hilo litakamilika Jumapili hii jinsi ilivyopangwa. Kulingana na tume hiyo, imetoa fursa kwa kila mkenya katika kila eneo kujisajili, ikiwataka ambao hawajasajiliwa kutumia muda uliobaki wa takribani […]

TANZANIA YAMKOSOA RUTO KWA ‘KUWADOGOSHA’ MAJIRANI

Serikali ya Tanzania imepuzilia mbali kauli za Rais William Ruto kwamba Kenya ina barabara nyingi za lami ikilinganishwa na mataifa yote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikisema kauli hizo ni za kudhalilisha. Akitetea bei za juu za mafuta nchini ikilinganishwa na mataifa jirani, Ruto alisema kuwa Kenya ni nchi yenye kiwango cha kati cha uchumi, […]

WALIMU WA JSS WATANGAZA MGOMO

Huku wanafunzi wakijiandaa kurejea shuleni kwa muhula wa pili wiki ijayo, huenda shughuli za masomo katika shule za sekondari msingi, JSS zikatasambaratika kutokana na mgomo wa walimu wa shule hizo ulioratibiwa kuanza Jumatatu. Lengo la mgomo huo ni kuishinikiza serikali kuwapa ajira ya kudumu, mbali na bima ya afya wakisema wamekuwa wakinyimwa huduma za matibabu […]

CHECHE AITAKA JUNIOR STARLETS KUDUMISHA NIDHAMU KABLA YA MECHI YA UGANDA

Kocha mkuu wa Junior Starlets Mildred Cheche amewataka wachezaji wake kubaki na nidhamu na kutojisahau huku wakijiandaa kwa mchezo wa pili wa mchujo wa Kombe la Dunia la wasichana wenye umri chini ya miaka kumi na saba Starlets wanatarajiwa kukutana na upinzani mkali kutoka Uganda katika hatua hii baada ya kuibwaga Namibia kwa jumla ya […]

MATHARE UNITED WOMEN WAPANDA DARAJA KURUDI LIGI KUU

Kikosi cha Mathare United Women kimehakikisha kupanda daraja kuelekea ligi kuu ya wanawake nchini baada ya kampeni nzuri katika Ligi ya Taifa ya Daraja la Pili Timu hiyo ilithibitisha mafanikio yake kwa ushindi wa mabao matatu kwa bila dhidi ya Gitothua mwishoni mwa wiki ushindi ulioweka wazi ubabe wao msimu huu na kurejea kwao katika […]

KAMWOROR KUREJEA LONDON MARATHON AKITAFUTA REKODI MPYA

Mshindi mara mbili wa New York City Marathon Geoffrey Kamworor anatarajiwa kurejea kwenye mbio za London Marathon Jumapili hii akiwa na lengo la kuboresha na kuvuka kiwango chake bora alichowahi kukimbia Katika mashindano ya mwaka 2023 Kamworor alikimbia muda wake bora zaidi wa saa mbili dakika nne na sekunde ishirini na tatu katika mbio za […]

BAADHI YA MCA NAIROBI WAMWOMBA RUTO AINGILIE KATI KUOKOA JIJI

Sehemu ya wawakilishi wadi wa jiji la Nairobi wamemwomba Rais William Ruto kuingilia kati na kusaidia kurekebisha hali ya jiji wakidai uongozi wa sasa umeshindwa kutekeleza majukumu yake Wakiongozwa na Mwakilishi wadi wa  Nairobi South Waithera Chege viongozi hao wamemtuhumu gavana Johnson Sakaja kwa ubaguzi wa baadhi ya maeneo na kushindwa kuboresha huduma kwa wananchi Hata hivyo wanakumbusha kuwa Rais Ruto […]

MAANDAMANO YA MAFUTA YAPOA HUKU MVUA IKIDHOOFISHA USHIRIKI

Mwanasheria wa katiba na mshauri wa masuala ya uchumi Makau Mutua amechochea mjadala kabla ya maandamano ya kupinga bei ya mafuta kwa kauli yake akihusisha kupanda kwa bei hizo na changamoto za usafirishaji katika njia muhimu ya kimataifa ya mafuta Maandamano ya vijana wa Gen Z jijini Nairobi hayakupata mwitikio mkubwa mapema baada ya mvua […]