MUSALIA AONYA WAKENYA KUHUSU EBOLA

Waziri mkuu Musalia Mudavadi amewataka wakenya kufuata maagizo yanayotolewa na wizara ya Afya kufuatia mulipuko wa ugonjwa wa Ebola ulioripotiwa katika mataifa jirani ya Uganda na Demokrasia ya Congo DRC. Akizungumza katika kaunti ya Morang’a Mudavadi amesema japo kenya haijaripoti kisa chochote cha Ebola uzembe unaweza kuhatarisha taifa hivyo wananch wanapaswa  kujitahadhari katika muingiliano wa […]

KEPSA YAONYA KUHUSU VIPENGELE KATIKA MSWADA WA FEDHA WA 2026

Muungano wa Sekta ya Kibinafsi ya Kenya (KEPSA) umepinga baadhi ya vipengele vya Mswada wa Fedha wa 2026, ukionya kwamba baadhi ya hatua zinazopendekezwa za ushuru zinaweza kukandamiza biashara, kudhoofisha ushindani wa Kenya na kupunguza kasi ya kuunda kazi. Ukiwakilishwa mbele ya Kamati ya Kitaifa ya Idara ya Fedha na Mipango ya Kitaifa, viongozi wa KEPSA wameambia Bunge […]

CHELSEA WALAUMIWA KWA UTOVU WA NIDHAMU

Kocha wa muda wa Chelsea Calum McFarlane amesema utovu wa nidhamu ulikuwa sababu kubwa iliyosababisha timu hiyo kukosa nafasi ya kushiriki mashindano ya Ulaya msimu ujao. Chelsea walimaliza katika nafasi ya 10 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufungwa mabao 2-1 na Sunderland Katika mechi ambayo, beki wa Ufaransa Wesley Fofana alitolewa nje kwa kadi nyekundu, ikiwa ni […]

MANCHESTER UNITED WANAPANGA KUMBAKISHA BRUNO FERNANDES

Manchester United wameanza mazungumzo ya kumbakisha nahodha wao Bruno Fernandes licha ya kuwepo kwa kipengele cha kuvunja mkataba wake chenye thamani ya pauni milioni 57. Ripoti zinaeleza kuwa mazungumzo ya awali tayari yamefanyika huku klabu hiyo ikiwa tayari kumzawadi kiungo huyo kwa mkataba bora zaidi. Bruno pia anaripotiwa kuvutiwa na vilabu vya Ulaya pamoja na […]

VIPIMA UBORA WA HEWA VYAWEKWA KABLA YA MBIO ZA NAIROBI CITY MARATHON

Vipima ubora vya hewa vinne vimewekwa katika maeneo muhimu kando ya Barabara ya Nairobi Expressway kuelekea mashindano ya Nairobi City Marathon yatakayofanyika Juni 7. Mashindano hayo yataanza City Hall Way na kumalizikia Uhuru Park huku sehemu kubwa ya mbio ikifanyika kwenye barabara hiyo. Mtafiti wa masuala ya ubora wa hewa kutoka Taasisi ya Mazingira ya Stockholm Ngongang Wandji amesema vifaa hivyo […]

ROONEY ONYANGO AITA AFCON 2027 FURSA YA KIPEKEE KWA KENYA

Beki wa kimataifa wa Kenya Rooney Onyango amesema mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2027 yatakuwa nafasi ya kipekee kwa soka ya Kenya kuandika historia mpya. Onyango ambaye kwa sasa anachezea Klabu Sogndal nchini Norway amesema mashindano hayo yatakuwa na uzito mkubwa kihistoria na kihisia kwa wachezaji wa Kenya. Beki huyo wa kulia mwenye umri wa […]

SERIKALI KUANZISHA MFUMO WA MIUNDOMBINU JULAI

Waziri wa Hazina ya Kitaifa John Mbadi amesema Mfuko wa Kitaifa wa Miundombinu utaanza kufanya kazi rasmi mwezi Julai mwaka huu kusaidia kufadhili miradi ya maendeleo nchini. Mbadi akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu kawi amesema baadhi ya miradi ya nishati imewekwa chini ya mfumo wa ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi. Aidha amesema baadhi ya miradi imehamishiwa […]

MARAGA AKOSOA SERIKALI KWA KUPUUZA MAAGIZO YA MAHAKAMA

Aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga ameikosoa serikali kwa kupuuza maagizo ya mahakama na kuahidi kulinda utawala wa sheria iwapo atachaguliwa kuwa rais. Akizungumza katika kaunti ya  Turkana Cwakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ukombozi, Maraga amesema serikali ya sasa haiheshimu Katiba wala maamuzi ya mahakama. Amedai kuwa serikali imekuwa ikipuuzilia mbali maagizo ya fidia kwa wananchi waliojeruhiwa […]

VIONGOZI WA UASIN GISHU WATAKA ULINZI WA RAIS UIMARISHWE

Baadhi ya viongozi kutoka Kaunti ya Uasin Gishu wamekosoa hitilafu ya kiusalama iliyotokea wakati wa ziara ya Rais William Ruto katika Kaunti ya Kilifi. Viongozi hao wakiongozwa na Gavana wa Kaunti hiyo Jonathan Bii wametaka hatua zaidi kuchukuliwa kuimarisha usalama wa mkuu wa nchi. Wamesema ni muhimu kuhakikisha matukio kama hayo hayajirudii tena siku zijazo. Imetayarishwa na […]

STEPHEN MULE AKOSOA MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA

Mbunge wa Matungulu Stephen Mule amekosoa mfumo wa serikali kwa serikali wa uagizaji wa mafuta akitaka soko huria lirejeshwe. Mule pia amependekeza kupunguzwa kwa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa mafuta kutoka asilimia 8 hadi 4 ili kupunguza mzigo kwa wananchi. Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja humu nchini, Mule amesema mfumo wa sasa umepunguza ushindani na kuchangia […]