HUENDA MAPATO YA KENYA YAKAELEKEZWA KWA MIKOPO, RIPOTI

Kenya ni miongoni mwa nchi 23 zinazotarajiwa kutoa zaidi ya asilimia 20 ya mapato yao kwa malipo ya deni la nje huku suala hilo likiendelea kusumbua utawala wa Rais William Ruto. Ripoti ya hivi punde ya Debt Justice, mshirika wa shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Uingereza, Christian Aid inaonyesha Kenya itatumia […]

KUCO YALETA NAFUU HOSPTILANI

Wakati uo huo, chama cha maafisa wa Kliniki KUCO kimefutilia mbali mgomo wao ambao umedumu kwa zaidi ya siku 100, baada ya mashauriano na baraza la magavana. Katika taarifa, katibu mkuu wa KUCO George Gibore, amesema wamekubalinaa kutia Saini mktaba wa kurejea kazini wakati wa mashauriano hayo. Akitangaza kufutilia mbali kwa mgomo huo ulioanza tarehe […]

KENYA YAAMRISHWA KUMFIDIA MWANAHABARI WA PAKISTAN

Mahakama kuu mjini Kajiado imeiagiza serikali ya kenya kuilipa shilingi milioni 10 familia ya mwanahabari Arshad Sharif raia wa Pakistan aliyuawa kwa kupigwa risasi hapa nchini mnamo mwezi Oktoba mwaka jana. Akitoa uamuzi huo, hakimu Stella Mutuku amesema hatua ya kutumia nguvu na kumpiga risasi kichwani mwanahabari huyo ilikuwa kinyume na sheria . Aidha, amemkosoa […]

MCAS TAITA WASUTWA BAADA YA KUMBANDUA SPIKA

Wiki moja baada ya spika wa bunge la kaunti ya Taita Taveta Wisdom Kazungu kubanduliwa baada ya wawakilishi wadi kukosa imani katika utendakazi wake, baadhi ya wakazi, wanaharakati na viongozi kwenye kaunti hiyo wamekosoa hatua hiyo. Wamedai kwamba wawakilishi hao walikuwa na njama ya kutetea maslahi yao na wala si ya wananchi. Wakizungumza mjini Voi, […]

KMPDU YAGAWANYIKA?

Huku madaktari wakianza mgomo wao wa kushinikiza kuajiriwa kwa wenzao wanagenzi, dalili za mgawanyiko zimeanza kuchipuka katika uongozi wa muungano wao wa kitaifa KMPDU. Katika maandamano ya kutaka kupiga kambi nje ya makao makuu ya wizara ya Afya, madaktari hao wameimba wimbo wa kumkashifu naibu katibu mkuu wa KMPDU Dennis Miskellah ambaye hawana imani naye. […]

NIKO SALAMA;SYLVANUS OSORO

Mbunge wa Mugirango Kusini Silvanus Osoro amewahakikishia wapiga kura usalama wake katikati ya mizozo kuhusu kuendelea kuunga mkono Mswada wa Fedha wa 2024 uliokataliwa. Katika mtandao wa kijamii jana Jumapili ambapo alishiriki kipande cha picha yake akitangamana na wenyeji huko Mugirango Kusini, ambapo alithibitisha kuwa yuko salama. Imetayarishwa na Janice Marete

DCI INACHUNGUZA MADAI YA UUZAJI WA SILAHA ILIYOMUUA TOM MBOYA

Idara ya Upelelezi dci inasema imeanza uchunguzi baada ya ripoti kuibuka kuwa mzee wa miaka 92 anadaiwa kununua bastola ambayo ilitumika kumuua Tom Mboya. Katika chapisho kwenye X, DCI imesema hatua itachukuliwa uchunguzi utakapokamilikaMboya aliuawa kwa kupigwa risasi Julai 5, 1969, katika Barabara ya Moi Avenue. Habari za kuuawa kwa Mboya zilienea kama moto wa […]

BAYERN WAMNYAKUA OLISE

Bayern Munich wamemsajili mshambuliaji wa Ufaransa Michael Olise kutoka Crystal Palace, Bayern ililipa kifungu cha kutolewa cha euro milioni 70 ($75 milioni) kwa klabu hiyo ya Ligi Kuu ili kupata huduma ya Olise kwa mkataba wa miaka mitano. Olise, 22, alikamilisha matibabu katika mji mkuu wa Bavaria siku ya Jumapili. Olise mzaliwa wa London, amewakilisha […]

EQUITY HAWKS WAFUZU KWA FAINALI

Equity Hawks ilifuzu kwa fainali ya Ligi Kuu ya Kitaifa ya Wanawake ya Mpira wa Kikapu ya Kenya kwa ushindi wa 3-2 dhidi ya Zetech Sparks Jumapili kwenye Ukumbi wa Nyayo Gymnasium. Wanabenki waliwacharaza wanafunzi 61-46 katika Mchezo wa Tano kati ya mfululizo wa michezo mitano. Equity itamenyana na mabingwa watetezi Mamlaka ya Bandari ya […]

KIPYEGON AVUNJA REKODI YAKE

Mkenya Faith Kipyegon alivunja rekodi yake ya dunia ya mbio za mita 1500 kwa wanawake katika mashindano ya Paris Diamond League hapo jana. Hatua hiyo inakuja kama nyongeza ya wakati kwa bingwa wa Olimpiki mara mbili kabla ya Michezo ya Olimpiki ya Paris baadaye mwezi huu. Jessica Hull wa Australia  alitumia muda wa 3:50.83 na […]