MASENETA WAPANGA KUFUTILIA MBALI NYADHIFA ZA CAS, NA KUPUNGUZA IDADI YA PS

Nafasi za makatibu waandamizi CAS zimepangwa kutupiliwa mbali na idadi ya makatibuu wakuu PS kupunguzwa katika juhudi za kupunguza gharama ya uendeshaji wa serikali. Seneti inalenga kuwasilisha hoja ya kuunganisha mashirika na taasisi za serikali ili kupunguza idadi ya wafanyikazi. Imetayarishwa na Janice Marete

AMRI YA RUTO KWA POLISI

Rais William Ruto amsalimu amri na kuamuru vikosi vya usalama kuachia huru wakenya wote waliokamatwa wakati wa maandamano kutokana na shinikizo za Wakenya. Katika taarifa kwa Wakenya kutoka Ikulu ya Nairobi, Ruto aidha ameamuru mashtaka yote dhidi ya waandamanaji kuondolewa. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAKENYA MAHAKAMANI WAKITAKA RUTO, GACHAGUA NJE

Wakenya 14 wamewasilisha kesi mahakamani wakitaka kuandaliwa kwa kura ya maoni ili kuwaondoa afisini kwa Rais William Ruto na naibu wake Rigathi Gachagua, wakisema wawili hao wameshindwa kuendesha nchi hasa kutokana na jinsi walivyoshughulikia maandamano. Kwenye kesi hiyo ambapo Ruto na Gachagua ndio washtakiwa, walalamishi wanahoji kuwa washtakiwa wameshindwa kudhibiti msukosuko wa kisiasa kwa mujibu […]

ORODHA YA MAWAZIRI WAPYA

Rais William Ruto amefanya uteuzi wa kundi la pili la mawaziri, na kuwateua mawaziri wengine 10 kuhudumu katika baraza lake la mawaziri. Katika uteuzi mpya, Rais amependekeza mbunge mteule John Mbadi kuhudumu kama Waziri wa fedha, wizara ya michezo Kipchumba Murkomen, Wizara ya Mashirika Wycliffe Oparanya, wizara ya masuala ya kijinsia Stella Lang’at, wizara ya […]

NYONGEZA YA MISHAHARA KWA POLISI, MAAFISA WA MAGEREZA WAANZA MWEZI HUU

Rais William Ruto amesisitiza kujitolea kwa serikali kutimiza ahadi yake ya nyongeza ya mishahara kwa maafisa wa magereza na maafisa wa polisi kuanzia mwezi huu. Akizungumza Ikulu wakati wa hafla ya kuapishwa kwa Kamishna Mkuu mpya aliyeteuliwa wa Jeshi la Magereza, Ruto ameapa kuwa serikali yake itatekeleza ahadi yake kwa watumishi hao.Mwanzoni mwa mwaka, serikali […]

DCI YAONDOA WITO WA BABU OWINO KUHUSU MADAI YA UCHOCHEZI

Idara ya Upelelezi wa Jinai imefutilia mbali wito wa Babu Owino kuhusu madai ya uchochezi.Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino alishiriki picha ya skrini ya mawasiliano ya DCI akionyesha kwamba hakuhitajika tena kujinufaisha. Katika mpini wake wa X, Babu amesema alikuwa amepanga kuhudhuria wito huo akiandamana na mawakili wake, Wabunge kadhaa na wafuasi kutoka kote […]

SARAFU

Na katika ubadilishanaji fedha dola moja ya Marekani kwa sasa inanunuliwa kwa shilingi 128.50 na kuuzwa kwa shilingi 133.50 huku Euro moja ikinunuliwa kwa shilingi 138.75 na kuuzwa kwa shilingi 149.14 Shilingi moja ya Kenya dhidi ya Uganda inanunuliwa kwa shilingi 29.41 na kuuzwa kwa shilingi 27.03 huku shilingi moja ya kenya dhidi ya Tanzania […]

KENYA INATARAJIWA KUAGIZA SUKARI ZAIDI KUTOKA NJE

Kenya inatarajiwa kurekodi ongezeko la uagizaji wa sukari kutoka nje, huku athari za kupiga marufuku usindikaji wa miwa ambayo haijakomaa zikianza, Ripoti iliyotolewa na Kampuni ya Fitch Solutions BMI na Idara ya Kilimo ya Marekani inaonyesha kuwa nchi inapaswa kutarajia uzalishaji kupungua kwa asilimia 32.9 mwaka 2023/24 hadi tani elfu 530,000 kutoka tani 790,000 mwaka […]

IMF HUENDA IKAIDHINISHA MPANGO MPYA WA FEDHA WA KENYA AGOSTI – MUDAVADI

Kenya imewasilisha mpango mpya wa kifedha kwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) baada ya maandamano ya wiki nzima nchini kote kulazimisha Rais William Ruto kuondoa Mswada wa Fedha wa 2024. Mswada huo tata ambao umezusha wimbi la maandamano nchini umependekeza hatua kadhaa mpya za ushuru ambazo zingeweza kuifanya serikali kukusanya angalau Shilingi bilioni 347 […]

HATUFADHILI MAANDAMANO

Mashirika mbali mbali katika kaunti ya Transnzoia yamepinga madai yaliyoibuliwa kwamba mashirika ya kutetea haki za binadamu yamekuwa yakifathili maandamano ya vijana kupitia fedha wanazopokea kutoka kwa wakfu wa Ford Foundation. Mashirika hayo yamesema kuwa serikali inapaswa kutilia maanani malalamishi yaliyoibuliwa na vijana wa humu nchini badala ya kuyalaumu mashirika hayo. Imetayarishwa na Janice Marete