KMPDU YAPENDEKEZA UCHUNGUZI WA MADAI YA UFISADI KATIKA SEKTA YA AFYA KUFANYWA

Muungano wa madaktari nchini Kenya KMPDU unapendekeza uchunguzi wa wazi kufanyika kuhusu madai yaliyoibuliwa ya ufisadi katika sekta ya afya. Katibu mkuu katika muungano wa KMPDU Dkt Davji Atella ametilia shaka jinsi kandarasi zinavyotolewa kwa kampuni za kigeni ambazo zinalaumiwa kwa kusambaza vifaa duni na kusababisha wizara ya afya kupoteza mamilioni ya fedha. Imetayarishwa na Janice Marete

MASENGELI: WALINZI WA WA JAJI MUGAMBI WALIHUDHURIA KOZI ZA USALAMA ZA VIP

Huduma ya Polisi ya Kitaifa (NPS) imefafanua kuwa kuondolewa ghafla kwa maelezo ya usalama ya Jaji Lawrence Mugambi, siku chache baada ya kumhukumu kaimu Inspekta Jenerali wa Polisi Gilbert Masengeli gerezani, kulikuwa chini ya uamuzi wa inspekta generali wa polisi. Masengeli katika taarifa yake amesema kuwa aliwateua maafisa hao wawili “kwa madhumuni ya kuhudhuria kozi […]

RUTO ABADILI MSIMAMO, ATEUA JOPOKAZI KUANGAZIA UFADHILI WA ELIMU

Rais William Ruto amebadili msimamo wake kuhusiana na mfumo wa kufadhili elimu ya juu na kubuni jopokazi la watu 129 kuangazia upya mfumo huo, ambao huenda ukarekebishwa baada ya kupokea pingamizi kutoka kwa wakenya wa matabaka mbali mbali. Kupitia chapisho kwenye gazeti rasmi la serikali, Ruto amesema jopokazi hilo litakuwa na kamati ndogo 4 chini […]

KASI MAHAKAMANI YAPUNGUA, KOOME

Huenda utoaji haki mahakamani ukatatizika kutokana na ukosefu wa fedha, jaji mkuu Martha Koome akisema mahakama hazina uwezo wa kutekeleza majukumu yake kikamilifu baada ya mgao wa mwaka wa kifedha wa 2024-25 kupunguzwa. Akizungumza katika mkutano na mabalozi na wawakilishi wa mataifa ya kigeni, Koome amesema kasi ya utoaji huduma imepungua kufuatia kupunguzwa kwa bajeti. […]

WAKENYA KUTOA SAUTI KUHUSU ADANI

Wakenya wameratibiwa kupata fursa ya kuamua iwapo serikali itakodisha uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKIA kwa kampuni ya Adani au la, baada ya wizara ya kawi kupanga kuanza kuandaa vikao vya kuchukua maoni ya Kenya kuhusu mpango huo ambao umezua pingamizi kali. Kwa mujibu wa serikali, lengo la kukusanya maoni ni kupata mitazamo tofauti […]

MAANDALIZI YA KCSE DAGORETTI KUTATIZIKA, SHULE YAFUNGWA

Huenda maandalizi ya mtihani wa kitaifa KCSE katika shule ya upili ya Dagoretti jijini Nairobi yakaathirika baada ya shule hiyo kufungwa kwa muda usiojulikana kufuatia mzozo baina ya makundi mawili ya wanafunzi ambapo wanafunzi 11 wanatibiwa kwenye hospitali mbali mbali baada ya kujeruhiwa. Kwa mujibu wa maafisa wa elimu, hatua ya kufungwa kwa shule hiyo […]

HUKUMU YA JAJI YAMUACHA BILA WALINZI

Huenda mzozo ukashuhudiwa baina ya serikali tendaji na idara ya Mahakama baada ya jaji wa mahakama kuu Lawrence Mugambi kupokonywa walinzi wake, siku moja baada ya kumpa hukumu ya miezi 6 gerezani kaimu inspekta mkuu wa polisi Gilbert Masengeli. Akiwahutubia wanahabari, jaji mkuu Martha Koome amesema walinzi hao waliopokonywa bunduki na kuondolewa wikendi iliyopita, na […]

WIZARA YA AFYA KUZINDUA MAFUNZO NCHINI KOTE KABLA YA KUANZISHWA KWA SHA

Wizara ya Afya inazindua mafunzo kote nchini kabla ya kuanzishwa rasmi kwa huduma za Mamlaka ya Afya ya Jamii. Uzinduzi huo utaongozwa na Waziri wa Afya Deborah Barasa ambapo ataungana na katibu wa Huduma za Matibabu Harry Kimtai, Mkurugenzi Mkuu wa Afya Patrick Amoth, na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Afya ya Jamii na Mkurugenzi Mtendaji. […]

BARAZA LA WATU WANAOISHI NA ULEMAVU LAANZISHA KAMPENI KUWASAIDIA WALEMAVU

Baraza la kitaifa la watu wanaoishi na ulemavu limeanzisha kampeni ya kuwasaidia watu wanaoishi na tawahudi au autism, Cerebral Palsy, kifafa na down syndrome. Mkurugenzi mtendaji Aron Hassan anasema kuwa tayari wamewatambua wagonjwa 18000 waliokuwa wakiishi na autism jambo ambalo kulingana naye ni garama kubwa kuwatibu. Imetayarishwa na Janice Marete

OMTATA: KUNA SIRI NYINGI KATIKA MRADI WA KUPEANA JKIA KWA ADANI

Mwanaharakati Okiya Omtata ameibua madai kwamba mradi wa kukodisha uwanja wa ndege wa kimataifa JKIA ni sakata ambayo inakiuka sheria za miradi ya binafsi kati ya serikali ya kenya na mashirika ya binafsi. Kulingana na Omtata wahusika walio kwenye stakabadhi za mkataba huo hawakuzingatia utaratibu unaopaswa kuzingatia na kwamba kuna siri nyingi katika mradi huo. Imetayarishwa na […]