JUVENTUS KUMTIMUA THIAGO MOTTA, IGOR TUDOR KUCHUKUA NAFASI

Juventus inatarajiwa kumfuta kazi kocha Thiago Motta chini ya msimu mmoja na kumteua Igor Tudor kama mrithi wake. Tudor atakabiliwa na jukumu la kusaidia klabu kumaliza ndani ya nafasi nne za juu kwenye Serie A ili kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa. Juventus kwa sasa wanashikilia nafasi ya tano huku zikiwa zimesalia mechi tisa. Chini ya […]

EVANS ASHINDA SAFARI RALLY KENYA, AIMARISHA UONGOZI WRC

Elfyn Evans ameongoza Mashindano ya Dunia ya WRC baada ya kushinda Safari Rally Kenya. Dereva wa Toyota sasa anaongoza kwa alama 36 mbele ya Thierry Neuville baada ya raundi tatu. Evans aliepuka changamoto za Safari Rally na kumaliza na uongozi wa dakika 1 na sekunde 9 mbele ya Ott Tanak wa Hyundai. Neuville alimaliza wa […]

SHUJAA YASAFIRI KWA HONG KONG NA SINGAPORE 7S

Timu ya raga ya Kenya, Shujaa, imeondoka nchini kuelekea mashindano ya Hong Kong 7s (Machi 28-30) na Singapore 7s (Aprili 5-6) wakilenga kuboresha matokeo yao kwenye HSBC SVNS Series. Kocha Kevin Wambua ametangaza kikosi thabiti, akimjumuisha Festus Shiasi badala ya Jackson Siketi. Mchezaji mahiri Jone Kubu pia ameendelea kushiriki, huku Patrick Odongo akirejea baada ya […]

HARAMBEE STARS YACHAPWA 2-1 NA GABON

Timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, ilipata kichapo cha 2-1 dhidi ya Gabon katika mechi ya kufuzu Kombe la Dunia la FIFA 2026, iliyochezwa jana Jumapili kwenye Uwanja wa Nyayo, na kuzidi kudhoofisha matumaini yao ya kufuzu. Nyota wa zamani wa Arsenal, Pierre-Emerick, alifunga mabao mawili kwa Gabon, ambao sasa wamepanda kileleni mwa Kundi […]

WAHUDUMU WA UHC WAENDELEZA MGOMO NORTHRIFT

Huduma za matibabu katika vituo mbali mbali vya afya kwenye kaunti zote 7 za Northrift zimeendelea kusambaratika kufuatia mgomo unaoendelea wa wahudumu wa afya walioajiriwa chini ya mpango wa afya kwa wote UHC, ambao wamekongamana mjini Kapsabet kaunti ya Nandi kufanya maandamano. Wahudumu hao wanashinikiza kuajiriwa kwa kanadarasi ya kudumu, wakidai kwamba serikali imewapuuza. Wameapa […]

TULETEE MBOLEA KARIBU, WAKULIMA BUNGOMA

Wakulima wa mahindi katika kaunti ya Bungoma wameitaka serikali kuwasilisha mbolea ya ruzuku katika maeneo ya mashinani ikiwemo kwenye afisi za machifu badala ya maghala ya bodi za nafaka NCPB pekee, wakilalamikia mwendo mrefu wanaotembea kuchukua bidhaa hizo. Wakizungumza na wanahabari katika eneo bunge la Webuye magharibi, wakulima hao wakiongozwa na Nancy Nelima wamesema umbali […]

MGOMO: MATIBABU YALEMAZWA MTRH

Shughuli muhimu za matibabu zimekwama katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Moi jijini Eldoret kutokana na mgomo wa wauguzi ambao umeanza hii leo, wagonjwa wakisalia na mahangaiko. Miongoni mwa malalamishi ya wauguzi hao ni madai kwamba hospitali hiyo imekataa kununua vifaa vya matibabu na hivyo kufanya kazi yao kuwa ngumu. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

OLUNGA: WAKENYA WAVUMILIE KOCHA MPYA WA STARS

Nahodha wa Harambee Stars, Michael Olunga, amesema Wakenya wanapaswa kuwa na subira na timu wakati wanajifunza mbinu za kocha mpya. Mshambuliaji huyo anasema Benni McCarthy, aliyeteuliwa hivi karibuni kuwa kocha wa Stars kwa mkataba wa miaka miwili unusu, atakuwa na muda mfupi wa kuandaa kikosi kabla ya mechi ya kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya […]

NYORO: SIJUI KWANINI NILIFURUSHWA

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro amesema hajui sababu ya kutimuliwa kwake kutoka wadhifa wa mwenyekiti wa kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa, akisisitiza kuwa hajawahi kuzungumziwa na mtu yeyote kutoka mrengo wa Kenya Kwanza kuhusu wadhifa huo. Akizungumza na wanahabari afisini mwake katika majengo ya bunge, Nyoro vile vile amedinda kuzungumzia uhusiano wake na […]

SEKTA YA AFYA YAENDELEA KUATHIRIKA

Masaibu yanayoikabili sekta ya afya yameendelea kuongezeka kutokana na migomo ya mara kwa mara, hii leo viongozi wa muungano wa madaktari KMPDU wakiwaongoza wanachama wake kuandamana jijini Nairobi kuikosoa serikali kutokana na kudorora kwa sekta hiyo. Madaktari hao ambao wameungana na watumishi wengine wa umma, wameandamana kutoka hospitali ya kitaifa ya Kenyatta hadi katika makao […]