UCHUKUZI JOGOO WATATIZWA

Shughuli za uchukuzi zimetatizika kwa muda katika barabara ya Jogoo jijini Nairobi kufuatia maandamano ya wafanyabiashara waliofunga barabara hiyo na kuwasha moto karibu na makutano ya Likoni Road kulalamikia madai ya kuwepo kwa mpango wa kubomoa vibanda vyao. Kulingana na wafanyabiashara hao, hawajapewa eneo mbadala la kuendeleza shughuli zao wakati ambapo vibanda vipya vitakuwa vikijengwa. […]

KENYA MBIONI KUIMARISHA KILIMO

Katika juhudi za kuimarisha utoshelevu wa chakula, serikali ya Kenya imesema iko tayari kushirikiana na serikali ya Uholanzi ili kupiga jeki sekta ya kilimo nchini. Katika kikao na wawekezaji Zaidi ya 50 wa Uholanzi waliomtembelea jijini Nairobi, katibu katika wizara ya biashara na viwanda Juma Mukhwana, amesema baadhi ya juhudi hizo ni ujenzi wa vituo […]

KENYA, UHOLANZI ZASHIRIKIANA

Setkta ya kilimo nchini inatarajiwa kuimarika kufuatia udhabiti wa ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Uholanzi, mataifa hayo mawili yakitia Saini mikataba kadhaa ya ushirikiano ikiwemo kilimo. Kutiwa Saini kwa mikataba hiyo kumewekwa wazi na Rais William Ruto katika Ikulu ya Nairobi ambako mfalme wa Uholanzi Willem Alexander na mkewe Malikia Maxima wamepokelewa. Kwa […]

WAKULIMA WA NG’OMBE WA MAZIWA KUNUFAIKA NA ONGEZEKO LA MAUZO YA NJE YA NCHI

Wakulima wa ng’ombe wa maziwa watanufaika baada ya Kenya kutangaza mpango wa kuongeza mauzo ya nje ya maziwa hadi KSh bilioni 9 ifikapo 2025, kutoka KSh bilioni 7.3 mwaka 2023. Mwenyekiti wa Bodi ya Maziwa Kenya (KDB), Genesio Mugo, amesema nchi inalenga masoko kama Mashariki ya Kati, Sudani Kusini na Somalia. Serikali inapanga kusindika zaidi […]

CS KAGWE ATAKA UFUMBUZI WA KIFEDHA KUIMARISHA KILIMO

Katika juhudi za kufufua uchumi, Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe amesisitiza umuhimu wa ufadhili shirikishi kwa sekta ya kilimo barani Afrika. Akizungumza katika mkutano wa AfDB, amehimiza uwekezaji katika uchambuzi wa udongo, mbolea, hifadhi ya mazao, na viwanda vya kilimo. Mkutano huo umehudhuriwa na Makamu wa Rais wa AfDB, Beth Dunford, na wadau wengine. Imetayarishwa […]

DCI YACHUNGUZA MAUAJI YA MWANAMKE EMBAKASI

Maafisa wa DCI wanachunguza mauaji ya mwanamke anayedaiwa kunyongwa na wanaume wawili eneo la Jua Kali, Embakasi kaunti ya Nairobi. Kisa hiki kinaangazia ongezeko la mauaji ya wanawake, huku visa 97 vikiripotiwa ndani ya miezi mitatu. Mwili wake umepelekwa kwenye hifathi ya maiti kwa uchunguzi. Imetayarishwa na Janice Marete

LIVERPOOL KARIBU KUTWAA UBINGWA LICHA YA WIKI NGUMU

Liverpool wapo karibu kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza, lakini hali ya sintofahamu imetanda baada ya wiki ngumu. Walipoteza fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Newcastle, siku chache baada ya kutolewa na PSG kwenye Ligi ya Mabingwa. Newcastle walitawala mchezo na kushinda taji lao la kwanza baada ya miaka 70. Hata hivyo, Slot […]

MUFUTU APONGEZA USHINDI WA ULINZI WARRIORS

Kocha wa Ulinzi Warriors, Benard Mufutu, amepongeza ushindi wa 62-26 dhidi ya Eldonets Platinum, akitaja mshikamano wa timu kuwa nguzo kuu. Katika mechi hiyo, Ulinzi ilitawala kila robo huku Brans Nzioka akifunga alama 12 na Derrick Ochieng 11.Strathmore Swords pia iliibuka na ushindi wa 44-33 dhidi ya The Swish, ingawa kocha Ronnie Owino hakuridhishwa na […]

RACHIER KUWANIA TENA UENYEKITI WA GOR MAHIA

Mwenyekiti wa Gor Mahia, Ambrose Rachier, atawania tena kiti chake katika uchaguzi wa klabu utakaofanyika Aprili 13, 2025, sambamba na Mkutano Mkuu wa Mwaka (AGM) katika Uwanja wa Nyayo. Amesema ana haki ya kugombea kwa mujibu wa katiba ya klabu na uamuzi wa Mahakama ya Michezo, huku akipuuza wakosoaji wake. Uchaguzi huo, uliocheleweshwa kwa migogoro […]

VIHIGA QUEENS KUJIPANGA KWA BUNYORE STARLETS

Kocha wa Vihiga Queens, Boniface Nyamuhnyamuh, anaamini mapumziko ya kimataifa yatasaidia timu yake kujiandaa kwa mechi yao dhidi ya Bunyore Starlets Jumamosi katika Uwanja wa Mumboha. Vihiga wanashikilia nafasi ya tatu kwa pointi 30, tatu nyuma ya vinara Kenya Police Bullets. Ushindi utawapandisha hadi nafasi ya pili. Nyamunyamuh anafanyia kazi safu ya ushambuliaji, huku FKF […]