KITHURE AWAONYA WAPINZANI

Naibu rais Kithure Kindiki amewahakikishia wakenya kuwa serikali inaangazia pakubwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo badala ya kujitosa katika kampeni za uchaguzi mkuu ujao. Kithure ameyasema haya kwenye mkutano na viongozi wa kaunti ya Nyandarua katika makazi yake rasmi mtaani Karen jijini Nairobi. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAWEKEZAJI WA SUKARI KUKABILIWA NA UHAKIKI WA MIKATABA

Mikataba ya wawekezaji binafsi waliokabidhiwa kusimamia viwanda vya sukari huenda ikafutiliwa mbali endapo hawatatekeleza wajibu wao ipasavyo. Afisa Mkuu Mtendaji wa Bodi ya Sukari, Judy Chesire, amesema kuwa wawekezaji hao wanapaswa kuhakikisha wanalipa wakulima wa miwa kila wiki, kuendeleza kilimo cha miwa, pamoja na kutumia mitambo ya kisasa katika usagaji wa miwa. Ameongeza kuwa mikataba […]

PIGO ZAIDI KWA WASHUKIWA WA MAUAJI YA WERE

Washukiwa 2 katika kesi ya mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kasipul Ong’ondo Were, akiwemo mkurugenzi wa mamlaka ya ustawi wa eneo la Ziwa Ebel Ochieng, wamepata pigo baada ya hakimu mkuu Irene Gichobi kukataa kujiondoa kwenye kusikiliza kesi hiyo. Ombi hilo lililowasilishwa wiki jana wakimtuhumu hakimu huyo kwa upendeleo, ni pigo la pili kwao baada […]

KENYA YALENGA KUONGEZA MAUZO YA CHAI KUFIKIA 2030

Wakulima wa zao la chai watanufaika na mpango mpya wa serikali kupitia Wizara ya Kilimo wa kuongeza mauzo ya chai ya Kenya kwenda China kwa zaidi ya mara nne ifikapo mwaka 2030. Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo, Mutahi Kagwe, amesema lengo ni kuongeza mauzo kutoka kilo milioni 12.42 mwaka […]

MAHAKAMA YASITISHA KAMATI YA UKAGUZI WA MADAI YA NHIF

Mahakama Kuu ya Eldoret imesitisha kwa muda shughuli za Kamati ya Ukaguzi wa Madai ya Matibabu ya NHIF hadi kesi ya kupinga uhalali wake itakaposikilizwa na kuamuliwa. Jaji Nyakundi ametoa agizo la kuizuia kamati hiyo kuendelea na kazi yoyote, akisema waombaji wameonyesha hoja za msingi. Kesi hiyo iliwasilishwa na Dkt. Benjamin Magare na wengine, wakidai […]

FARMERS PARTY YAPANGA MAANDAMANO KUMREJESHA GACHAGUA

Chama cha Farmers kimesema kitafanya maandamano kuelekea makazi rasmi ya Naibu Rais, Rigathi Gachagua, huko Karen, Nairobi, baada ya Mahakama ya Rufaa kufutilia mbali uamuzi wa Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu wa kuunda jopo la majaji kusikiliza ombi la kumng’atua Gachagua. Gachagua aliondolewa serikalini Oktoba 18 kupitia pendekezo la Seneti, na Kindiki aliteuliwa kama mrithi […]

KOOME ATAKA USHIRIKIANO KUKOMESHA DHULUMA ZA KIJINSIA

Katika juhudi za kumaliza dhuluma za kijinsia, Wakenya wametakiwa kushirikiana na mahakama na mashirika ya serikali kukabili ongezeko la visa hivyo. Jaji Mkuu Martha Koome amesema dhuluma za kijinsia ni janga la kijamii na zinaweza kutokomezwa tu kwa ushirikiano wa jamii na taasisi husika. Akizungumza mjini Kisumu wakati wa uzinduzi wa mahakama maalum ya kushughulikia […]

TAIWO AWONIYI AFANYIWA UPASUAJI WA DHARURA

Mshambulizi wa Nottingham Forest Taiwo Awoniyi amefanyiwa upasuaji wa dharura baada ya kuumia tumboni alipogongana na mlingoti wakati wa mechi dhidi ya Leicester. Awoniyi alijaribu kuendelea kucheza baada ya matibabu ya awali, lakini jeraha lake lilithibitishwa kuwa kubwa siku iliyofuata. Tukio hilo lilizua hasira kwa mmiliki wa klabu Evangelos Marinakis aliyemkabili kocha Nuno kwa kumwacha […]

OKWEMBA ATAKA UWEKEZAJI KWA CHIPUKIZI KUINUA SOKA

Kiungo wa zamani wa AFC Leopards, Charles Okwemba, anawataka wadau wa soka nchini kuwekeza kwa wachezaji chipukizi ili kuwawezesha kuwa na ushindani kwenye ngazi ya kimataifa. Wito wake unajiri siku chache baada ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20, Rising Stars, kuondolewa kwenye mashindano ya AFCON U20 nchini Misri bila kushinda mechi […]

SENENDE YASHANGAZA NA KUTWAA TAJI LA U19 BLACK ROCK

Timu ya wavulana walio na umri wa chini ya miaka 19 kutoka Shule ya Upili ya Senende iliibuka mabingwa wa wavulana U19 baada ya kuishinda Kakamega High 12-10 katika fainali ya mwisho ya mashindano ya Western Black Rock yaliyofanyika Kakamega. Mwaka huu mashindano hayo yalihusisha timu 33 katika makundi manne. Kinale Girls waliibuka mabingwa kwa […]