OLEKSANDR USYK AWEKA WAZI KICHOCHEO CHAKE

Bingwa wa masumbwi ulimwenguni Oleksandr Usyk amesema anachochewa pakubwa na nidhamu na wala si motisha kuendelea kucheza mchezo huo, baada ya kumbwaga Daniel Dubois katika uwanja wa Wembley jijini London Uingereza kwenye pigano la Jumamosi. Ufanisi huo wa Jumamosi umemfanya raia huyo wa taifa la Ukraine mwenye umri wa miaka 38 kuwa bingwa dunia kwa […]

KVF YAIMARISHA MAANDALIZI YA UBINGWA WA AFRIKA

Shirikisho la mchezo wa voliboli nchini KVF limeimarisha maandalizi kwa ajili ya mashindano ya bingwa wa voliboli ya akina dada bara Afrika yatakayoanza tarehe 2 mwezi ujao nchini Cameroon. Miongoni mwa mikakati iliyowekwa na shirika hilo ni mageuzi katika usimamizi wa timu ya wanawake ya voliboli kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20, ambako mchezaji […]

DCP KUSAIDIA KUONDOA VIJANA WANAOZUILIWA

Chama cha Dcp kitaongoza mchango wa kukusanya fedha za kuwasaidia vijana wanaozuiliwa maeneo tofauti baada ya kushiriki katika maandamano. Haya ni kwa mujibu wa kiongozi wa Dcp Rigathi Gachagua akihojiwa huko Boston Marekani na kusema kuwa wataendesha mchango huo kwa kuwashirikishia wasamaria wema. Ameongeza kuwa mawakili wao pia watashughulikia masuala yote ya kisheria yanayohusu mamia […]

MHUDUMU WA MPESA ADUNGWA KISU KISUMU

Polisi huko Kisumu wanachunguza kisa ambapo mhudumu mmoja wa duka la Mpesa anadaiwa kudungwa kwa kisu akiwa kwenye duka lake sehemu ya Shauri Moyo. Mercy Muthoni alishambuliwa na mshukiwa mmoja aliyeingia kwenye duka lake kwa kutumia mlango wa nyuma kabla ya kumdunga kwa kisu. Mshukiwa huyo kwa jina Justine Otieno anashambuliwa na wenyeji waliokuwa na […]

ATWOLI AONYA KUHUSU VURUGU NCHINI

Katibu wa vyama vya wafanyikazi nchini Cotu Francis Atwoli amewataka vijana kuwa na subira na kuipa serikali nafasi ya kutekeleza miradi itakayowapa nafasi za ajira. Atwoli ambaye amewataka pia wanasiasa kujizuia kutoa matamshi ya chuki anasema vurugu na hali inayoshuhudiwa nchini imetishia waekezaji. Imetayarishwa na Maureen Mukhobe

MOSHI MWEUPE KWA MBEUMO

Manchester United wamefikia makubaliano na Brentford kumsajili mshambuliaji Bryan Mbeumo.Baada ya mazungumzo ya wiki kadhaa, dili la thamani ya hadi £71million ($95.5m) hatimaye limepigwa. – Mwanariadha Imetayarishwa na Nelson Andati

TSC KUWAPA WALIMU MAFUNZO YA CBE

Walimu wa shule za upili za juu yaani Senior Secondary, wameratibiwa kupokea mafunzo upya kuhusu mtaala wa umilisi CBE katika maandalizi ya kuanzishwa kwa mtaala huo katika shule hizo. Kulingana na tume ya kuwaajiri walimu TSC, mafunzo hayo yatatolewa kuanzia tarehe 28 mwezi huu hadi tarehe 15 mwezi ujao kwenye maeneo yatakayoteuliwa kwenye kaunti zote […]

UTATA WAENDELEA KUZINGIRA MGAO WA SHULE

Kauli kinzani kutoka kwa Wizara ya Elimu na Hazina ya Kitaifa zimezua sintofahamu kuhusu hali ya utoaji wa fedha kwa ajili ya shule za umma, na kuibua wasiwasi kuhusu ucheleweshaji wa fedha na athari zake katika uendeshaji wa shule. Katibu Mkuu wa Elimu ya Msingi Julius Bitok amesema kwamba shule za umma zilipokea asilimia 60 […]

MANCHESTOR UNITED WAONGEZA KIWANGO CHA PESA KWA JILI YA MBEUMO

Manchester United wamewasilisha dau la tatu la uhamisho wa mshambuliaji wa Brentford Bryan Mbeumo lenye thamani ya £65m pamoja na £5m za nyongeza. Brentford wanazingatia ofa hiyo na bado hawajafanya uamuzi.Mbeumo ametaka kujiunga na United kwa zaidi ya mwezi mmoja tu, na klabu hiyo inafahamika kuwa imetiwa moyo na azma yake ya kujiunga nao. Mchezaji […]

KCB RFC YAFANYA USAJILI KUJIANDAA KWA MSIMU UJAO

Mabingwa mara nane wa Kombe la Kenya KCB Rugby wameonyesha nia yao ya kurejea kilele cha raga ya Kenya walipotangaza msururu wa usajili wiki hii. Wanabenki waliimarisha safu yao ya mbele kwa kutangaza kumnunua Hafidh Mohamed maarufu kwa jina la Baby Rhino kutoka maharamia wa Pwani Kusini. Klabu hiyo yenye maskani yake Kwale ilitangaza kuondoka […]