GACHAGUA: MIMI NDIYE KIGOGO WA UPINZANI

Aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua ametanagaza kuwa ndiye yuko katika nafasi nzuri ya kuwa kigogo wa upinzani na kumenyana na Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu ujao. Akizungumza katika jimbo la Boston nchini Marekani, Gachagua amesema ana uwezo wa kumfanya Rais Ruto kutochaguliwa kwa muhula wa pili. Aidha, amefichua kuwa upinzani utaweka wazi atakayepeperusha bendera […]

BONIFACE MWANGIAACHILIWA KWA BONDI

Mahakama imemwachilia kwa bondi ya shilingi milioni 1 mwana harakati Boniface Mwangi aliyekamatwa siku ya jumamosi kwa madai ya kufadhili shughuli za kigaidi. Mwangi alikamatwa nyumbani kwake eneo la Lukenya kwa madai ya kupatikana na vitoa machozi ,risasi na vifaa vingine kinyume na sheria. Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 19 mwezi ujao. Imetayarishwa na Maureen […]

MAHAKAMA YATAKA STAKABADHIZA MATIBABU YA KALOMcBOTOLE

ImetayarishwaMahakama imeagiza Hospitali ya kitaifa ya Kenyatta kuwasilisha stakabadhi za matibabu ya mshukiwa wa mauaji ya mgonjwa katika hospitali hiyo Kennedy Kalombotole. Hakimu Daisy Mutai ameitaka KNH Pamoja na hospitali ya Nairobi Womens kuwasilisha stakabadhi zinazoonyesha ugonjwa anaotibiwa mshukiwa huyo. Kennedy ambaye anahusishwa na kifo cha mgonjwa huyo kwa jina Edward Maingi Ndegwa atazuiliwa kwa […]

KABRAS SUGAR KUJITOSA UBABENIWA KUBEBA MATAJI MATANO MFULULIZO

Kabras Sugar italenga kunyoosha ubabe wao wa Kombe la Kenya hadi mataji matano msimu wa 2025/2026 itakapoanza mnamo Novemba, Kulingana na kocha Achayo, wachezaji wa Millers’s 15s wanarejea kujiandaa na msimu ujao ili kuanza maandalizi yao kabla ya msimu mpya unaotarajiwa kuanza Novemba Kabras walinyanyua taji lao la nne la Kenya Cup mfululizo mnamo Aprili […]

SURA MPYA YA NOC-K

Shadrack Maluki, bosi wa Shirikisho la Judo la Kenya, amechaguliwa kuwa rais mpya wa NOC-K, katika uchaguzi uuliofanyika mapema hii leo. Maluki ambaye awali aliwahi kuwa makamu wa kwanza wa rais wa kamati hiyo alishinda kwa wingi wa kura 15 akimshinda Katibu Mkuu anayemaliza muda wake Francis Mutuku aliyepata kura 12. Maluki anachukua nafasi kutoka […]

HARAMBEE STARS NJE YA CECAFA

Harambee Stars imejiondoa kwenye Mashindano ya CECAFA ya Mataifa manne nchini Tanzania kufuatia tathmini ya kiufundi. Timu sasa inajiandaa kwa ajili ya CHAN 2024 Imetayarishwa na Nelson Andati

SERIKALI YATOA CHANGAMOTO KWA SMES

Seŕikali imetoa wito kwa biashara ndogo ndogo na ya kati (SMEs) kutafuta fuŕsa zinazoibukia za biashaŕa katika Pembe ya Afŕika, ikitaja ushirikiano wa kikanda kama kichocheo kikuu cha ukuaji wa uchumi. Akizungumza wakati wa Kongamano la Kimataifa la Wajasiriamali wa Kisomali jijini Nairobi, Katibu Mkuu wa Maendeleo ya biashara ndogo ndogo na za kati Susan […]

SHIDA HAZIANZI LEO, MBADI ASEMA

Waziri wa fedha John Mbadi, ametetea utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza akisema serikali hiyo inafanya kazi bora ikilinganishwa na serikali iliyiopita. Akizungumza katika eneo la Suba West, Mbadi amewashutumu wakosoaji wa serikali ya sasa, amekariri kuwa changamoto za kiuchumi za sasa zilishuhudiwa pia wakati wa utawala uliopita. Aidha, amesema serikali imetoa mgao wa kutosha […]

RAILA: NIKO NA RUTO HADI 2027

Nitamuunga mkono Rais William Ruto hadi akamilishe muda uliobaki wa muhula wake madarakani kufikia mwaka wa 2027. Ni kauli ya kinara wa ODM Raila Odinga, akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini ambako amesisitiza kuwa hakuna mazungumzo kati yake na chama cha UDA kuhusu uchaguzi mkuu ujao. Amesema ushirikiano wake wa kisiasa na […]

MWANGI KUFIKA MAHAKAMANI KAHAWA

Mwanaharakati wa humu nchini Boniface Mwangi ameratibiwa kufikishwa katika mahakama ya Kahawa jijini Nairobi ambako atafunguliwa mashtaka ambayo polisi wameyataja kuwa yanayohusiana na ugaidi. Mwangi alikamatwa siku ya Jumamosi nyumbani kwake kwenye kaunti ya Machakos kabla ya kusindikizwa hadi afisi yake jijini Nairobi ambako polisi wanasema walipata risasi bandia, vitoza machozi 2 ambavyo havijatumika miongoni […]