TUSKER YATEMA WACHEZAJI TISA

Tusker FC imetangaza rasmi kuachana na wachezaji tisa huku klabu hiyo ikianza kukisuka upya kikosi chake kabla ya msimu mpya. Wachezaji wanaoondoka katika kikosi cha Ruaraka ni pamoja na John Byamukama, James Kibande, Luke Namanda, David Odoyo, Boban Zirintusa, Deogratious Ojok, Mike Oduor, na Lawrence Luvanda, ambao wote wanaondoka baada ya kandarasi zao kuisha. Zaidi […]

SENEGAL KUCHEZA CECAFA

Shirikikisho la mpira la (CECAFA) limethibitisha kuwa Senegal itachukua nafasi ya Congo Brazzaville katika michuano ijayo ya CECAFA ya Mataifa Nne ya Pre-CHAN itakayofanyika Julai 21-27, 2025, Arusha, Tanzania. Mechi hizo zitafanyika kwenye Uwanja wa Karatu, kwa kushirikisha timu shiriki zikiwemo Kenya, Uganda, Tanzania na Senegal. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa CECAFA, Auka Gecheo, […]

MSHUKIWA MKUU WA MAUJAJI KNH AKAMATWA

Maafisa wa idara ya upelelezi DCI wamemkamata mshukiwa mkuu katika mauaji ya mgonjwa wa pili aliyepatikana akiwa ameuawa katika wodi ya wagonjwa kwenye hospitali ya kitaifa ya Kenyatta, ikiwa ni chini ya miezi 5 baada ya mgonjwa mwingine kuuawa katika wodi iyo hiyo. Mgonjwa huyo wa kiume Edward Maingi mwenye umri wa miaka 54, alipatikana […]

MBUNGE KIHARA KUFIKISHWA MAHAKAMANI

Mbunge wa Naivasha Jayne Kihara anatarajiwa kufikishwa mahakamani asubuhi hii baada ya maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai DCI kumkamata hapo jana kuhusiana na tuhuma kuchochea vurugu wakati wa maandamano. Polisi waliokuwa wamejihami walivamia makazi yake katika eneo la Maraigushu na kumkamata, baada yake kudaiwa kupuuza agizo la kufika mbele ya idara ya DCI […]

WAKULIMA WA MIWA MAGHARIBI WAPATA AFUENI

Wakulima wa miwa katika eneo la Magharibi wamepata afueni baada ya Mahakama Kuu mjini Busia kufutilia mbali uamuzi wa kufungwa kwa muda viwanda 7 vya sukari katika ukanda huo, baada ya wakulima hao wakiongozwa na mkulima shupavu wa miwa Apostle Peter Manyuru wa kanisa la JTM, kuwasilisha kesi mahakamani. Kupitia wakili Ruth Kimani, Wakulima wamesisitiza […]

RAIS AZURU EMBAKASI

Rais William Ruto amezidi kuwapuuzilia mbali wapinzani wake anaosema hawana sera zozote kwa wakenya na lengo lao pekee na kutaka kumwondoa mamlakani. Akiongea huko Embakasi Mashariki ambako ameshuhudia miradi tofauti ya ujenzi wa barabara rais ameelezea mpangilio alio nao kuhakikisha kuwa vijana wanapata ajira. Imetayarishwa na Maureen Muhkobe

PETROVIC AJIUNGA NA BOURNEMOUTH

Mlinda mlango wa Chelsea Djordje Petrovic alijiunga na Bournemouth kwa mkataba wa thamani ya pauni milioni 25 ($33 milioni) siku ya Jumatano. Petrovic alikubali mkataba ambao utamweka kwenye Uwanja wa Vitality hadi Juni 2030. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alikuwa Chelsea tangu ajiunge nayo akitokea klabu ya MLS ya New England Revolution mwaka […]

BELLINGHAM KUKOSA MICHEZO KUMI NA MIWILI

Kiungo wa kati wa Real Madrid, Jude Bellingham anatarajiwa kukosa hadi wiki 12 ili kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa bega baada ya wababe hao wa Uhispania kusema Jumatano kwamba amefanikiwa kufanyiwa upasuaji.Wakati Madrid haikutaja muda uliotarajiwa wa muda wake wa kupona, vyombo vya habari vya Uhispania vimeripoti kuwa itamchukua takriban wiki 12 kurejea […]

MABONDIA WA KENYA KUKUTANA KATIKA MICHUANO YA NDONDI

Nyota wa hapa nchini, Kombo Mwinyifaki na Shaffi Bakari nao watajitokeza kwa wingi ulingoni. Katika kujiandaa na mashindano hayo, mabondia 20 bora wa Mombasa wamefanya mazoezi makali na Franck Petitjean, Bingwa mara nne wa Ufaransa na bingwa wa Uropa, na mkufunzi mashuhuri wa viungo Valentino Gargiulo. Imeidhinishwa na Shirikisho la Ndondi la Kenya, hafla hiyo […]

MKONDO WA PILI WA NDONDI KUANDALIWA MOMBASA

Chama cha Ndondi cha Kaunti ya Mombasa, kwa ushirikiano na Alliance Française de Mombasa, wanatazamiwa kuandaa mkondo wa pili wa Ligi ya Kitaifa ya Ndondi ya Kenya kuanzia Alhamisi, Julai 17 -19, 2025, katika uwanja wa Alliance Française, Nyali. Mapambano hayo yenye shughuli nyingi yatafanyika kila siku kuanzia saa mbili usiku, huku mchuano wa mwisho […]