WAKENYA WAKIMBIA MIKOPO YA BENKI

Asilimia kubwa ya wakenya sasa imehamia kuchukua mikopo kutoka kwa watoa huduma za pesa kwa njia ya simu huku ukopaji wa benki ukipungua. Ripoti ya Global Findex 2025 ya Benki ya Dunia inaarifu kuwa mwaka wa 2024 ukopaji rasmi nchini ulirekodi ongezeko kutoka 2021, ambapo wengi walitafuta pesa kutoka kwa akaunti za pesa za rununu. […]

WAKULIMA WALINDWA DHIDI YA TABIA NCHI

Wakulima kote nchini wana kila sababu ya kutabasamu baada ya Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo kuzindua Mpango wa Bima ya Mbolea ili kuwakinga wakulima wadogo wadogo dhidi ya athari za hali ya hewa kama vile ukame na mafuriko. Mpango huo ulizinduliwa kwa ushirikiano na shirika la Pula, Bayer, Lemonade, SOMPO Digital Lab, na […]

WANARIADHA 50 KUELEKEA TOKYO JAPAN

Mwenyekiti wa Riadha Kenya tawi la Nairobi Barnaba Korir anasema wanapanga kupeleka wanariadha zaidi ya 50 kwenye Mashindano yajayo ya Riadha ya Dunia yanayopangwa Tokyo Japan. Akizungumza kabla ya Majaribio ya Kitaifa, yanayotarajiwa kuanza Jumanne katika Uwanja wa Ulinzi Sports Complex, Korir alisema idadi hiyo inaweza kuongezeka ikiwa wanariadha wengi zaidi watafuzu kwa mashindano hayo. […]

LIVERPOOL WAKUBALI KUMSAJILI HUGO

Liverpool wamekubali kumsajili mshambuliaji wa Eintracht Frankfurt Hugo Ekitike kwa mkataba wa awali wa pauni 69 kulingana na ripoti. Mabingwa hao wa Premier League walielekeza nguvu zao kwa Ekitike kufuatia Newcastle kukataa kumuuza mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa pauni milioni 150 na Magpies. Newcastle na Manchester United pia walikuwa na […]

KIPCHONGE AJIONDOAKWA MBIO ZA DUNIA

Aliyekuwa mshikilizi wa rekodi ya dunia ya mbio za marathon Eliud Kipchoge hatashiriki mashindano ya dunia, mkurugenzi wa Athletics Kenya Youth and Development Barnaba Korir amesema. Korir alisema mshikilizi huyo wa zamani wa rekodi ya dunia amechagua kutoshiriki ili kuwafungulia njia wanariadha wengine. Wito wa mwisho wa Kipchoge kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Paris ulipokelewa […]

GYOKERES BADO ANAWINDWA

Arsenal wanatazamiwa kuendeleza matumizi yao ya pesa msimu huu wa joto huku wakijaribu kupata dili la Viktor Gyokeres huku kukiwa na ushindani wa kuchelewa, huku Liverpool wakikaribia kukamilisha usajili wa Hugo Ekitike. Mabingwa hao wa Premier League pia wanajaribu kuzuia nia ya Bayern Munich kumnunua Luis Diaz, ambaye anataka kuondoka Anfield. Kwa upande wa Chelsea, […]

SHIKANGWA AFANYA MAZOEZI ULAYA BAADA YA KUACHANA NA SIMBA SC

Mshambulizi wa Harambee Starlets, Jentrix Shikangwa Milimu anasema uamuzi wake wa kuachana na wababe wa soka ya wanawake ya Tanzania, Simba Queens, umechochewa na nia ya kutafuta changamoto mpya. Shikangwa aliachana na timu hiyo yenye maskani yake Msimbazi wiki moja iliyopita na kuashiria mwisho wa sura nzuri katika soka la wanawake Tanzania. Shikangwa alikuwa miongoni […]

KENYA YAIDHINISHWA KUANDAA CHAN

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Veron Mosengo-Omba ameidhinisha Kenya akisema nchi hiyo iko tayari kuandaa Michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN). Akizungumza jijini Nairobi baada ya kukagua viwanja viwili vilivyopendekezwa—Kasarani na Nyayo—Mosengo-Omba, ambaye alizuru viwanja hivyo pamoja na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Michezo Salim Mvurya na Rais wa Shirikisho la […]

KESI YA REX KUENDELEA LEO

Uchunguzi katika mauaji ya mwanarika la Gen Z Rex Maasai umeratibiwa kuendelea hii leo mahakamani baada ya kikao hicho kuahirishwa hapo jana kufuatia hatua ya upande wa mashtaka kuishtumu idara ya polisi kwa madai ya kupuuza maagizo ya mahakama. Hii ni baada ya idara hiyo kukosa kuwasilisha kwa muda mwafaka rekodi zinazoonyesha jinsi maafisa wa […]

KESI YA MVUVI BRIAN YAAHIRISHWA

Kesi inayohusiana na mvuvi aliyetoweka katika eneo la Nakuru Brian Odhiambo itaendelea tarehe 1 mwezi Septemba baada ya kikao cha kusikilizwa kwa kesi hiyo kuahirishwa hapo jana. Wakati wa kikao hicho, mtaalamu wa deta za mawasiliano, Hassan Salado, alifichua kuwa simu ya Odhiambo ilionekana mara ya mwisho eneo sawa na zile za maafisa 4 wa […]