KENYA POLICE WAZAMISHA GARDE YA DJIBOUTI

Kenya Police FC ilitangaza kuwasili kwa makala ya 23 ya Kombe la Kagame la CECAFA kwa mtindo, na kuibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Garde Cotes FC ya Djibouti kwenye Uwanja wa Major Isamuhyo Jumanne alasiri. Mchezo huo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu uliashiria kusajiliwa kwa wachezaji watano wapya kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi […]

ACHA LALAMA MTOE SULUHU, SERIKALI

Viongozi wanaoegemea mrengo wa Kenya Kwanza wamewataka wenzao wa upinzani kusitisha shutuma dhidi ya serikali na badala yake kushirikiana ili kutatua changamoto zinazolikabili taifa. Miongoni mwa viongozi hao ni naibu rais Kithure Kindiki, akizungumza kwenye kikao na mamia ya vijana nyumbani kwake katika kaunti ya Tharaka Nithi. Kindiki amewahakikishia vijana kuwa serikali inaendelea na mikakati […]

WAHUDUMU WA UHC WAPATA AFUENI

Hatimaye mustakabali wa wahudumu wa afya walio chini ya mpango wa afya ya wote UHC umepata suluhu baada ya serikali kuu kusitisha zoezi la kuwahamishia kwa serikali za kaunti na badala yake kukubali kuwalipa mishahara yao kulingana na viwango vya tume ya SRC kwa mwaka mmoja ujao. Makubaliano hayo yalijiri kufuatia mazungumzo ya dakika za […]

SAKAJA APONEA MJELEDI WA BUNGE

Ni afueni kwa gavana wa Nairobi Johnson Sakaja baada ya wawakilishi wadi katika bunge la kaunti hiyo kusitisha kwa muda wa siku 30 mchakato wa kumbandua kutoka mamlakani waliokuwa wameanzisha. Hii ni kufuatia wito wa Rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga kwa wawakilishi wadi hao, katika mikutano miwili tofauti ambako viongozi hao […]

SHULE ZATISHIA KUWAREJESHA WANAFUNZI NYUMBANI

Wakuu wa shule za upili nchini wameonya kuhusu uwezekano wa masomo kutatizika muhula huu wa mwisho kutokana na ukosefu wa fedha za kufanikisha uendeshaji wa shughuli shuleni. Kulingana na wakuu hao, serikali haijatuma asilimia 20 iliyosalia ya mgao wa shule, na huenda wakalazimika kuwarejesha nyumbani wanafunzi. Sera ya mgao wa masomo inaishinikiza serikali kutoa asilimia […]

SENNE AJIUNGA NA MANCHESTER UNITED 

Manchester United imemsajili mlinda mlango wa Ubelgiji Senne Lammens kutoka Royal Antwerp kwa euro 21m za awali (£18.1m) pamoja na nyongeza. Lammens, 23, ambaye bado hajashinda mechi ya wakubwa kwa taifa lake, anawasili Old Trafford kwa kandarasi ya miaka mitano. Lammens amecheza mechi 64 akiwa na Royal Antwerp na kuwasaidia kushinda Kombe la Ubelgiji Super […]

CITY WAPATA KIPA MPYA 

Manchester City ilithibitisha kumsajili mlinda mlango wa Italia Gianluigi Donnarumma kutoka Paris Saint-Germain Jumanne baada ya kumuuza Ederson wa muda mrefu kwa Fenerbahce. Donnarumma, 26, amesaini mkataba wa miaka mitano Etihad kwa ada iliyoripotiwa ya pauni milioni 26 ($35 milioni). Donnarumma, ambaye atavaa jezi ya 99, alikuwa sehemu muhimu ya timu ya PSG iliyoshinda Ligi […]

GRIMSBY YAPIGWA FAINI

Mchezaji wa kimataifa wa Kenya, Clarke Sydney Omondi Oduor ametiwa machoni baada ya klabu yake, Grimsby Town, kutozwa faini ya Ksh 3.5 milioni (£20,000) kwa kumchezesha kama mchezaji asiyestahili katika ushindi wao wa Kombe la Carabao dhidi ya Manchester United. Ligi ya Soka ya Uingereza (EFL) ilithibitisha Jumanne kwamba Grimsby ilikiuka sheria za mashindano walipomsajili […]

MAGEUZI KATIKA USIMAMIZI WA WAOGELEAJI

Michezo ya waogeleaji wa Kenya unaingia katika enzi mpya baada ya Mkurugenzi wa Kiufundi wa Kenya Aquatics, Omar Omari, kutangaza mageuzi makubwa yaliyolenga kuimarisha mchezo huo kitaaluma, kuinua viwango na kulinda uadilifu huku nchi ikitazama mafanikio kwenye hatua kubwa zaidi. Marekebisho hayo yataanzisha viwango vilivyopangwa kwa makocha na maafisa. Kwa makocha, mfumo wa madaraja manne […]

OGAM AHAMIA WOLFSBERGER

Mshambulizi anayekuja kwa kasi Kenya Ryan Ogam amekamilisha uhamisho kutoka Tusker FC hadi Wolfsberger AC ya Bundesliga ya Austria, na kuashiria hatua kubwa katika maisha yake ya soka. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, alizaliwa Nairobi Desemba 2004, ataungana na wachezaji wenzake wapya baada ya mapumziko ya kimataifa. Wolfsberger, ambaye alimaliza katika nafasi ya […]