WAKAZI KUKWAMISHWA NA MCHEZO

Wakazi wa jiji la Nairobi wametatizika kusafiri kutoka na msongamano wa magari, uliosababishwa na kufungwa kwa baadhi ya barabara ili kuruhusu maandalizi ya mechi ya soka baina ya timu ya taifa Harambee Stars na the Gambia itakayochezwa leo katika uwanja wa Kasarani. Idara ya trafiki imetangaza kufunga barabara kadhaa, watumiaji ya barabara kuu ya Thika […]

NAOMI AZIDI KUTAMBA KATIKA MAONYESHO YA GOFU

Mkenya Naom Wafula alitimua raundi ya pili ya Mashindano ya Gofu ya SportsBiz Afrika kwa kishindo cha kuvutia kwenye shimo la sekunde 3 katika Kigali Golf Resort & Villas. Pengo la risasi saba linamtenganisha Nsanzuwera na wapinzani wake wa karibu. Waliofungwa kwa nafasi ya pili kwenye 6-under-par 138 ni Travis Procter wa Afrika Kusini na […]

FKF YASIFIA IDARA YA USALAMA

Vyombo vya usalama vya Kenya vimesifiwa kwa jukumu lao la kipekee la kuhakikisha uenyeji wa michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024 iliyomalizika hivi majuzi na yenye mafanikio. Katika taarifa iliyotolewa Alhamisi, Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Hussein Mohammed alikiri kujitolea, uratibu na weledi ulioonyeshwa na vikosi vya usalama vya nchi wakati […]

KENYA KUWASILISHA OMBI KUANDAA TOKYO 2029

Kenya itawasilisha rasmi ombi lake la kuandaa Mashindano ya Riadha ya Dunia ya 2029 au 2031 wakati wa toleo la mwaka huu la mashindano ya kimataifa huko Tokyo, rais wa Riadha Kenya (AK) Jackson Tuwei amethibitisha. Akizungumza wakati wa hafla ya kupeperusha bendera ya Timu ya Kenya iliyofanywa na Rais William Ruto katika Ikulu Jumatano, […]

MCCARTHY AHIMIZA KIKOSI CHAKE KUKAZA BUTI

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka ya HARAMBEE STARS Benni McCarthy amekiri kwamba safari ya kuelekea Kombe la Dunia la FIFA 2026 HAIJULIKANI , lakini akahimiza Harambee Stars kuendelea kuamini inapojiandaa kukaribisha Gambia katika mechi muhimu ya kufuzu Kasarani siku ya Ijumaa. Akizungumza wakati wa mkutano na wanahabari Alhamisi, McCarthy alikiri ugumu wa […]

KCB KUONYESHA UBABE WAO KWA MKONDO WA KABEBERI

KCB RFC itapania kudhihirisha ubabe wao katika Kabeberi Sevens wikendi hii huku awamu ya tano ya mzunguko wa Kitaifa wa Saba ikiendelea katika uwanja wa RFUEA jijini Nairobi. Wanabenki hao wamekuwa katika hali NZURI kutinga fainali ya awali na kunyanyua Driftwood Sevens mjini Mombasa pamoja na Christie Sevens jijini Nairobi. Uthabiti wao umewafanya wapande kileleni […]

WANAJESHI WAKOSESHA UTULIVU MANDERA

Utata kuhusu kuwepo kwa vikosi vya jeshi la Jubaland katika kaunti ya Mandera umeendelea kuibua mijadala nchini huku serikali ikikana kuwepo kwa vikosi hivyo. Kulingana na wakazi wa eneo la mpaka la Border One kwenye kaunti hiyo, shughuli za kila siku ikiwemo masomo zimetatizika kutokana na uwepo wa vikosi hivyo, hatua iliyowalazimu kufanya maandamano hapo […]

UPINZANI KUZINDUA JINA, NEMBO WIKI IJAYO

Muungano wa upinzani ukiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua na kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka umeratibiwa kuzindua jina lake rasmi na nembo Jumatatu wiki ijayo katika maandalizi ya chaguzi ndogo zijazo na uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Uzinduzi huo hata hivyo unajiri huku migawanyiko ikishuhudiwa kwenye muungano huo kuhusiana na uteuzi wa Waziri wa […]

OPERESHENI MAALUM YAAGIZWA JIJINI

Hali ya kawaida inatarajiwa kurejea katikati mwa jiji la Nairobi baada ya Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen kuagiza operesheni maalum kwa lengo la kukabili magenge ya uhalifu ambayo yameibua hofu jijini. Kulingana na Murkomen, wengi wa washukiwa hujifanya Watoto wa kurandaranda mitaani ambao baadaye huwashambulia wapita njia na wafanyabiashara na kuwaibia. Wakenya wametaja […]

CHELEWA CHELEWA ITAKAYOKUGHARIMU MABILIONI.

Wakenya watalazimika kulipa takribani shilingi bilioni 25.3 kama adhabu kugharamia riba ya madeni ya serikali ambayo yamechelewa kulipwa. Ni onyo iliyotolewa na mdhibiti wa bajeti ya serikali Margaret Nyakang’o, anayesema madeni ya serikali yaliongezeka kwa shilingi bilioni 9 katika kipindi cha mwaka wa kifedha uliopita pekee. Nyakang’o amesema wizara ya uchukuzi inaongoza kwa deni la […]