NPS YAENDELEZA AFYA YA KIAKILI

Idara ya huduma za polisi NPS imeanzisha juhudi za kuimarisha afya ya kiakili ya maafisa wake kupitia mafunzo yanayotolewa kwa washikadau wakwemo wataalam wa ushauri nasaha na wanasaikolojia ambao hushughulikia afya ya kiakili ya maafisa hao. Mafunzo hayo ya siku 4, yanatolewa kwa ushirikiano na shirika la International Justice of Kenya, yakiwalenga watu 43 walio na jukumu la kutoamsaada kwa […]

SERIKALI YAWATAFUTIA SOKO WAKULIMA MAREKANI

Wakulima nchini sasa wanatarajia kufaidika kutokana na kupanuakwa fursa za mauzo ya nje baada ya waziri wa Kilimo na maendeleo yamifugo Mutahi Kagwe kuanza ziara yake ya wiki moja yenye dhamira yabiashara nchini Marekani. Kwenye ziara hiyo, Waziri Kagwe analenga kuwatafutia wakulima soko la moja kw amoja nchini Marekani na kuwaondoa maawakala ambao huwapuinja wakulima. Tayari Kagwe na ujumbe wake […]

BULLETS KUZIDUA KAMPENI YA CECAFA

Timu ya Kenya Police Bullets wanatazamiwa kuzindua harakati zao za kuwania tiketi ya kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya CAF mwaka huu katika Mashindano ya Kanda ya CECAFA yatakayoanza Alhamisi katika uwanja wa Nyayo. Mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Wanawake ya FKF watamenyana na Kampala Queens ya Uganda kuanzia saa kumi jioni […]

KIKOSI CHA TIMU YA WAVU CHAZINDULIWA

Shirikisho la Mpira wa Wavu la Kenya (KVF) limezindua kikosi cha muda cha timu ya taifa ya mpira wa wavu ya wanaume walio na umri wa chini ya miaka 20 kabla ya Mashindano ya 22 ya Mpira wa Wavu ya Mataifa ya Afrika, yanayopangwa Septemba 11-21, 2025, Cairo, Misri. Michuano hiyo itatumika kama mchujo wa […]

OWINO APIGIA UPATO HARAMBEE STARS

Mchezaji wa kimataifa wa Kenya Sylvester Owino anasema Harambee Stars iko katika nafasi nzuri zaidi ya kukusanya pointi nyingi zaidi kutoka kwa mechi mbili za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Gambia na Ushelisheli. Owino ambaye pia alijumuishwa katika kikosi cha Harambee Stars katika kinyang’anyiro cha CHAN kilichomalizika hivi majuzi anasema kiwango cha wachezaji waliochaguliwa […]

FAMILIA YA AFISA  ALIYEFARIKI HAITI YAOMBOLEZA

Familia ya afisa wa polisi aliyefariki kwenye ajali nchini Haiti Kennedy Mutuku imetoa wito kwa serikali kuisaidia katika kuurejesha nchini mwili wa afisa huyo ili kufanikisha mazishi nyumbani kwao katika kaunti ya Machakos. Kulingana na Sera Ndung’e ambaye ni mamake Mutuku, kifo cha mwanawe wa pekee kimesababisha pigo kwa familia, akisema mwanawe alikuwa amepanga kuwatembelea […]

IEBC YATANGAZA TAREHE YA CHAGUZI NDOGO

Maandalizi ya chaguzi ndogo 23 nchini yameshika kasi huku tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC ikitangaza mikakati ya kuzifanikisha, katika juhudi za kuhakikisha uwazi kwenye uchaguzi huo. Mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethekon ametangaza kuwa chaguzi hizo zitaandaliwa tarehe 27 mwezi Novemba mwaka huu, huku kampeni zikiratibiwa kuanza tarehe 8 mwezi ujao, siku ambayo […]

MAGAVANA WAENDELEA KUMULIKWA

Magavana zaidi nchini wameendelea kujipata chini ya darubini ya vyombo vya uchunguzi kuhusiana na sakata za ufisadi katika kaunti zao, wa hivi punde akiwa gavana wa Nakuru Susan Kihika. Akiwa mbele ya kamati ya uhasibu katika bunge la seneti hapo jana, Kihika alikuwa na wakati mgumu kueleza madai ya ufujaji wa zaidi ya shilingi milioni […]

NITAVURUGA MIFUMOMKINICHAGUA, KIGAME

Uongozi wangu kama rais utakuwa wenye kuvuruga mifumo iliyoko ili kubadilisha jinsi siasa na uongozi unavyoendeshwa humu nchini. Ni kauli ya mwaniaji wa urais kwenye uchaguzi mkuu ujao na mwimbaji Reuben Kigame, akizungumza kwenye mahojiano na wanahabari. Kigame amesisitiza haja ya kuifanya elimu tena kama suala la kipaumbele, akirejelea enzi ya rais wa tatu Mwai […]

14 WAKAMATWA KITALE

Maafisa wa polisi kutoka vitengo mbali mbali wamewakamata washukiwa 14 wa msururu wa visa vya uhalifu mjni Kitale. Kulingana na idara ya upelelezi wa jinai DCI, washukiwa wamekamatwa katika maeneo ya Umoja, Kisumu Ndogo, Tuwan, Bondeni na Mitume kufuatia operesheni iliyoratibiwa vyema. Aidha, imesema inawahoji washukiwa kabla ya kuwafikisha mahakamani. Imetayarishwa na Antony Nyongesa