ALIYEKUWA WAZIRI MKUU RAILA AFARIKI

Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 80. Kiongozi huyo wa chama cha ODM amefariki mapema leo katika hospitali moja jijini Kochi nchini India, alikokuwa akitibiwa kwa siku 5 zilizopita. Odinga ambaye amekuwa kiongozi wa upinzani na mbunge wa Lang’ata hadi mwaka 2013, atakumbukwa kwa harakati zake za kuleta […]

JESHI LATWAA MADAGASCAR 

Kundi la maafisa wa kijeshi nchini Madagascar limechukua uongozi wa taifa hilo la Kusini mwa Afrika baada ya Rais Andry Rajoelina kubanduliwa na bunge. Hii ni baada ya Rajoelina aliyedinda kujiuzulu licha ya shinikizo za waandamanaji kuhusu tuhuma za uongozi mbaya na ufisadi, kuelekea mafichoni mapema wiki hii. Kwa mujibu wa afisa wa jeshi aliyeongoza […]

MGOMO WA WAHADHIRI WAFIKA MAHAKAMANI

Macho yote sasa yameelekezwa kwa mahakama kutoa mwelekeo kuhusu mgomo wa wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma ambao umedumu kwa mwezi mmoja sasa, baada ya kikao cha mazungumzo kati ya wahadhiri na serikali kufeli. Katibu mkuu wa UASU Dakta Constantine Wasonga, ameilaumu serikali kwa madai ya kukwamisha utekelezaji wa mkataba wa maelewano wa mwaka wa […]

“MUUAJI” WA IKULU KUZUILIWA KWA SIKU 14

Mshukiwa wa mauaji ya afisa wa GSU nje ya Ikulu ya Nairobi Kithuka Musyimi, atazuiliwa kwa siku 14 zaidi ili kuruhusu polisi kukamilisha uchunguzi katika kifo cha afisa huyo aliyeuawa kwa kudungwa mshale. Sehemu ya uchunguzi inahusisha ukaguzi wa mienendo ya mshukiwa na mawasiliano ya simu yake, duru zikiarifu kuwa Musyimi na afisa huyo kwa […]

WABUNGE, DUALE WARUSHIA MANENO

Kikao cha kupata maelezo kuhusu utendakazi wa mamlaka ya afya ya jamii SHA kimesambaratika baada ya wanachama wa kamati ya afya bungeni kuanza majibizano na Waziri wa afya Aden Duale, aliyewatuhumu wabunge hao kwa madai ya kumshurutisha atoe hongo. Kamati hiyo chini ya uwenyekiti wa mbunge wa Seme Dakta James Nyikali hata hivyo, imemshutumu Waziri […]

MAHAKAMA UGANDA YAAMURU SERIKALI KUWAWASILISHA WANAHARAKATI

Serikali ya Uganda imepewa siku 7 kuweka wazi waliko wanaharakati wa Kenya Bob Njagi na Nicholas Oyoo walioripotiwa kutekwa nyara nchini humo takribani wiki 2 zilizopita na watu wanaoaminika kuwa maafisa wa usalama. Kwenye uamuzi wake katika kesi inayohusu haki ya washukiwa kuwasilishwa mahakamani ndani ya saa 24 baada ya kukamatwa, hakimu Peter Kinobe ameiagiza […]

WAUGUZI ISIOLO WASITISHA MGOMO

Wakazi wa kaunti ya Isiolo wamepata afueni baada ya wauguzi kutia Saini mkataba wa kurejea kazini na hivyo kutamatisha mgomo wao uliokuwa umesambarataisha huduma za matibabu kwa miezi 2. Mgomo huo umesitishwa kufuatia mazungumzo kati ya muungano wa wauguzi, bodi ya uajiri wa umma na saerikali ya kaunti hiyo, wauguzi wakitakiwa kurejea kazini kufikia Alhamisi […]

SERIKALI KUUNDA HAZINA YA MIUNDOMBINU YA KSH4 TRILIONI KWA MIRADI MBALI MBALI

Rais William Ruto ametangaza mipango ya kuunda Hazina ya Kitaifa ya Miundombinu ya Ksh4 trilioni ili kufadhili miradi mikubwa ya nishati, barabara na mabwawa. Akiongea wakati wa kuanzishwa kwa Awamu ya Kwanza ya Konza Technopolis katika Kaunti ya Makueni, Ruto amesema hazina hiyo itakusanya rasilimali kutoka kwa bajeti, sekta ya kibinafsi, na ubinafsishaji ili kuendeleza […]

DE BRUYNE AIPEPETA UBELGI KILELENI KWA KUNDI

Kiungo wa Napoli Kevin De Bruyne alifunga mara mbili kupitia mikwaju ya penalti na kuiweka timu yake ya taifa ya Ubelgiji katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa kombe la dunia mwaka ujao, walipopata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Wales. Ubelgiji wanaonolewa na Rudi Garcia, walijipata nyuma ya Wales katika uwanja wa Cardiff kupitia goli […]

TUNISIA YAWEKA HISTORIA SAFARINI KUELEKEA KOMBE LA DUNIA

Timu ya taifa ya Tunisia ilihitimisha kampeni yake ya kusaka tiketi ya kushiriki kombe la dunia mwaka ujao bila kufungwa bao walipoicharaza Namibia mabao 3:0 kwenye mechi yao ya mwisho ya kundi H hapo jana. Tunisia walimaliza kampeni yao kwa kushinda mechi 9 kati ya 10, wakifunga mabao 22 kushiriki fainali hizo. Bao la kwanza […]