GACHAGUA AONYA DHIDI YA ‘USALITI’ MLIMANI

Aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua amewahimiza viongozi na wakazi wa eneo la Mlima Kenya kudumisha mshikamano ili kufanikisha maendeleo. Gachagua ameonya kuwa huenda migawanyiko ya kisiasa ikasababisha kusambaratika kwa eneo hilo iwapo viongozi watakubali kutumiwa kisiasa kuendeleza migawanyiko hiyo. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

RUTO ABASHIRI USTAWI WA KENYA

Kenya itafikia viwango vya maendeleo ya mataifa ya Uchina na Singapore kufikia mwaka wa 2055. Haya ni kwa mujibu wa Rais William Ruto, akisema hayo yataafikiwa kupitia mshikamano wa nchi, hasa kutokana na juhudi zake za kuwajumuisha mahasimu wake wa kisiasa serikalini. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

UTEKAJI: RUTO ATAKIWA KUINGILIA KATI

Familia ya mwanaharakati Nicholas Oyoo aliyeripotiwa kutekwa nyara nchini Uganda akiwa na mwenzake Bob Njagi imemtaka Rais William Ruto sasa kushauriana na mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni ili kufanikisha kupatikana kwa wanaharakati hao. Wawili hao wametoweka kwa siku 12 sasa bila kujulikana waliko, wanaharakati wenza nchini wakitishia kufanya maandamano kote nchini siku ya Alhamisi iwapo […]

UBINAFSISHAJI WA KENYA PIPELINE 

Serikali imeanzisha rasmi mchakato wa kuhamisha Kampuni ya Kenya Pipeline (KPC) kuwa ya binafsi kupitia toleo la awali la umma (IPO) katika Soko la Hisa la Nairobi. Hili ni moja wapo ya tofauti kuu za serikali nchini Kenya katika miaka ya hivi karibuni. Katika tangazo kwa umma lililochapishwa katika magazeti ya kila siku, Tume ya Ubinafsishaji, wakala unaohusika na […]

“HASARA YA UKOSEFU WA CHAKULA CHA GMO”

Kenya imepoteza zaidi ya Ksh.20 bilioni katika kipindi cha miaka mitano pekee kutokana na kucheleweshwa kwa kuidhinisha aina za hali ya juu za mazao ya GMO ambazo zinaweza kuimarisha usalama wa chakula na mapato ya wakulima. Ripoti mpya inaonya kwamba habari potofu na vikwazo vya udhibiti vinaweka teknolojia zinazobadilisha maisha kutoka kwa mikono ya wakulima […]

NIPO UNITED, BRUNO FERNANDES

Kiungo wa klabu ya Manchester United Bruno Fernandes ameweka wazi kwamba hana nia ya kuhamia ligi ya Saudi Pro mwishoni mwa msimu ujao, na badala yake analenga kusalia United. Duru zilizo karibu na mchezaji huyo wa Ureno zimesema kwamba alikatalia mbali ofa kutoka kwa klabu za Al-Hilal na Al-Ittihad  mwishoni mwa msimu jana, ili kuendelea […]

SHUJAA IKO TAYARI, NAHODHA

Nahodha mwenza wa kikosi cha raga cha Shujaa, George Ooro anaamini kwamba mashindano ya Safari Sevens yatakayofanyika wikendi hii hii yatakuwa maandalizi mazuri kwa michuano ya “Dubai Invitational” mwishoni mwa Novemba mwaka ujao. Mshambuliaji huyo amesema kuwa timu itajiandaa ipasavyo katika maandalizi, siyo tu kwa ajili ya mashindano ya Dubai, bali pia kwa duru ya pili ya World Seven Series (WSS) inayotarajiwa […]

KIZAAZAA CHA TIKETI KUNDI C

Katika mechi za kufuzu mashindano ya kombe la dunia mwaka ujao, kizaazaa kinatarajiwa katika kundi C wakati Benin walio na alama sawa na South Africa, watakuwa ugenini dhidi ya Rwanda hii leo, siku ambayo pia South Africa watakuwa ugenini dhidi ya Zimbabwe. Nigeria ambao pia wana nafasi ya kufuzu kwa kombe hilo, watashuka dimbani dhidi […]

HARAMBEE STARS WAJIANDAA KUAGA

Timu ya taifa Harambee Stars inajiandaa kwa mechi yao ya mwisho dhidi ya Ivory Coast Jumanne wiki ijayo baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Burundi hapo jana kwenye mechi za kuwania kufuzu kwa kombe la dunia mwaka ujao. Mshambulizi wa klabu ya Wolfsberger Ryan Ogam aliyeingia kama nguvu mpya, aliifungia Stars bao la […]

DCP YATETEA UAMUZI WAKE MALAVA

Chama cha DCP kinachoongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua kimetetea uamuzi wake wa kumwasilisha mgombeaji kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika eneo la Malava Edgar Busiega, licha pingamizi kutoka kwa chama tanzu cha muungano wa upinzani DAP-K. Naibu kinara wa DCP Cleophas Malala, amesema uamuzi huo hautishii umoja wa upinzani, anaosema utasalia imara kuelekea […]