KENYA KUOKOA MABILIONI YA PESA KWA KUBADILISHA PESA YA MIKOPO YA SGR

Kenya inatazamiwa kuokoa shilingi bilioni 27.79 kila mwaka baada ya kubadilisha mikopo ya reli ya kiwango cha dola ya Standard Gauge Railway (SGR) kuwa Yuan ya Uchina. Kama ilivyoripotiwa, Kenya itaanza kulipa kwa sarafu mpya kuanzia Januari mwaka ujao. Waziri wa Hazina ya kitaifa John Mbadi amesema mikopo mingi inayodaiwa na China tayari imebadilishwa, na kuruhusu Kenya kuepuka viwango vya juu […]

HOFU YA USALAMA YAKUMBA MECHI ZA ISRAEL

Hofu ya kiusalama imeendelea kukumba mechi za timu ya taifa ya Israel dhidi ya Norway na Italia, mayor wa jimbo la Udine lililoko kaskazini mwa Italia akionya kuhusu hali ya usalama mechi hiyo inapoandaliwa wiki ijayo. Israel itasafiri kuelekea Norway kwa mechi ya Jumamosi, kabla ya kumenyana na Italia Jumanne katika mechi za kundi I, […]

KRU YATAJA VIKOSI VYA SHUJAAS, MORANS

Shirikisho la raga nchini KRU liemzundua rasmi vikosi vya Shujaa na Morans kwa mashindano yam waka huu ya Safari Sevens 2025, yatakayoanza tarehe 10 na kukamilika tarehe 12 mwezi huu katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi. Mashindano hayo ya kila mwaka yatayashirikisha mataifa kutoka maeneo mbali mbali ya bara la Afrika, Ulaya na pembe zote, […]

STARS WAENDELEA KUJIFUA BURUNDI

Timu ya taifa ya Soka Harambee Stars inaendeleza mazoezi yake kabla ya mechi dhidi ya Burundi hapo kesho baada ya kuondoka nchini hapo jana. Stars ambao tayari walibanduliwa nje ya safari ya kuelekea katika mashindano ya kombe la dunia mwaka ujao, watakuwa wakitumia mechi hiyo kujiimarisha kabla ya mashindano ya ubingwa wa mataifa barani Afrika […]

DENI KUATHIRI MASOMO YA GREDI YA 10

Huenda masomo ya wanafunzi wa gredi ya 10 mwaka ujao yakatatizika kutokana na ukosefu wa vitabu, ambavyo wachapishaji wanasema hawajachapisha hadi sasa kutokana na deni la shilingi bilioni 11.4 wanalodai serikali. Kupitia kwa muungano wao, wachapishaji wamesema deni hili litaathiri uchapishaji na usambazaji wa vitabu hivyo, wakiitaka serikali kulipa deni hilo. Nakala milioni 7 za […]

ODM: BABA YUKO SAWA

Uongozi wa chama cha ODM umewataka viongozi wa kisiasa kukoma kutumia suala la afya ya kinara wa chama hicho Raila Odinga katika majukwaa ya kisiasa. Wakiongozwa na katibu mkuu Edwin Sifuna, manaibu wa kinara Abdulswamad Nassir na Godfrey Osotsi, vionghozi hao wameshikilia kwamba Odinga yuko sawa kiafya kinyume na madai ya baadhi ya viongozi. Imetayarishwa […]

MASHIRIKA YALALAMIKIA ONGEZEKO LA MIKOPO

Zaidi ya nusu ya mapato ya taifa hutumika kulipia madeni na hivyo kuacha nje sekta muhimu za uchumi wa taifa. Haya ni kwa mujibu wa shirika la Okoa Uchumi, likisema shilingi 7 kati ya 10 hulipa madeni, huku likiongeza kuwa mikopo ya ndani imekuwa rahisi kufujwa kutokana na ukosefu wa ufuatiliaji. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KENYA YALENGA KUPATA MAUZO ZAIDI YA NJE KUPITIA EU NA COMESA

Serikali kuu iko mbioni kuongeza juhudi za kufufua mauzo ya nje ya kilimo hadi Ulaya na hata katika masoko mapya ya Afrika kwa kuoanisha viwango vya bidhaa, kuondoa vizuizi visivyo vya ushuru, na kuboresha usafiri wa kikanda. Waziri wa Biashara Lee Kinyanjui, akizungumza katika Kongamano la COMESA Horticulture Connect jijini Nairobi, aMEsema serikali inashirikiana na Soko la Pamoja la Mashariki […]

FIDIA YA MAANDAMANO: MAHAKAMA YAZUIA JOPOKAZI, TENA

Mahakama kuu mjini Kerugoya imeongeza agizo linaloifutilia mbali utendakazi wa jopokazi lililoteuliwa na rais William Ruto kuweka mfumo wa kuwafidia waathiriwa wa maandamana na ghasia zilizotokea wakati wa maandamano. Hakimu Edward Muriithi ametoa uamuzi wa kuzuia utendakazi wa jopokazi hilo ukisubiri malalamishi ya wahusika katika kesi hiyo yatakaposikilizwa tarehe 21 mwezi huu. Uamuzi huo unajiri […]

MEMPHIS DEPAY AIBIWA PASPOTI BRAZIL

Huku taifa la Uholanzi likilenga kuzidisha uongozi wa kundi G katika kinyang’anyiro cha kufuzu mashindano ya kombe la dunia mwaka ujao, hofu imeibuka kuhusu uwepo wa nyota wao mahiri Memphis Depay ambaye ameripoti kwamba paspoti yake iliibiwa nchini Brazil. Depay anayeichezea klabu ya Corinthians nchini Brazil, alikuwa ameratibiwa kusafiri Jumapili kujiunga na wenzake wa timu […]