KIJANA MWENYE UMRI WAMIAKA 14 APATIKANA AMEFARIKI NAKURU

Kijana mmoja mwenye umri wa miaka kumi na minne amepatikana akiwa amefariki na mwili wake ukiwa umetupwa kando ya barabara katika kijiji cha sunrise eneo bunge la njoro kaunti ya Nakuru . Mamake kijana huyo amesema kwamba kijana wake alimuaga hapo jana akieleka kanisani akiwa na babake ila hakujerea nyumbani na baadae mwili wake kupatikana mapema hii leo. Kwa […]

RAIS RUTO AKATAA KUJIHUSISHA NA UCHAGUZI WA TANZANIA

Rais William Ruto amechagua kutojihusisha na  uchaguzi uliokumbwa na utata nchini Tanzania ambao ulipelekea kuchaguliwa tena kwa rais Samia Suluhu huku   maandamano makali yakishuhudiwa nchini humo. Hata hivyo ametoa maoni kwamba kama demokrasia ingedumishwa, ushindi mkubwa wa samia haungeshuhudiwa Rais Ruto hata hivyo amewataka viongozi kukumbatia   demokrasia ili kuruhusu uwakilishi wa haki na sawa katika michakato ya uchaguzi, akisema kuwa ghasia haipaswi kuwa chaguo bora. Imetayarishwa na Jones Koikai

RUTO ATETEA AMRI YA “RISASI MIGUUNI’

Sijutii kuwaamuru polisi wawapige risasi za miguu wakenya waliokuwa wakishiriki maandamano ya hivi majuzi ya kupinga sera za serikali. Ndiyo kauli ya Rais William Ruto kwenye mahojiano na shirika la habari la kimataifa la Aljazeera, akisema sheria inawaruhusu polisi kupitia nguvu kupita kiasi kuwakabili waandamanaji wanaozua vurugu. Kulingana na rais, wahuni waliingilia maandamano hayo. Imetayarishwa […]

MAKAZI YA BEI NAFUU: KENYA YATAMBULIWA KIMATAIFA

Kenya imetambuliwa rasmi kimataifa kwa miradi yake ya makazi ya kijamii kwa watu wasiojiweza na wale wa kadri wa mijini na Mpango wa Kukuza Upya wa Mito ya Nairobi, ambayo imesifiwa kama mipango yenye athari kubwa ya kustahimili hali ya hewa kusini mwa dunia. Akizungumza katika Kongamano la COP 30 mjini Belem, Brazili, Naibu Rais […]

MASHARTI MAPYA YA WORLD BANK KWA MKOPO WA KENYA

Baada ya mazungumzo ya miezi kadhaa, Benki ya Dunia sasa inataka Kenya kupunguza nakisi ya bajeti yake kabla ya kupokea shilingi bilioni 96.9 kama mkopo. Ripoti inaonyesha kuwa deni la mwaka huu wa kifedha unaoisha Juni mwaka ujao inafikia shilingi bilioni 901. Hii inaipa Hazina ya kitaifa fursa ya kupunguza matumizi au kuongeza mapato ili kupunguza upungufu. Hali hiyo mpya ya Benki ya Dunia inaweza kuifanya serikali kuamua kuongeza ushuru […]

MAGENDO YA KAHAWA SIRISIA

Serikali inapoteza mamilioni ya pesa za ushuru kufuatia ongezeko la biashara za magendo ya kahawa kutokana na utepetevu wa maafisa wa upelelezi DCI katika eneo la Sirisia kaunti ya Bungoma ambao wamehishindwa kuwanasa wahusika. Ni kauli ya mbunge wa eneo hilo John Waluke, akidai maafisa hao wanajihusisha kwenye magendo hayo na wafanyabiashara katika taifa jirani […]

MUSYOKA KWA RUTO: NJOO ILA NI “WANTAM”

Wakazi wa eneo la Ukambani wametakiwa kumkaribisha Rais William Ruto wakati wa ziara yake eneo hilo kuanzia Jumatano wiki hii licha ya kuegemea mirengo tofauti ya kisiasa. Akizungumza katika eneo la Lukenya kaunti ya Makueni, kinara wa Wiper Kalonzo Muysoka amesisitiza kuwa ni haki ya kila mkenya akiwemo rais kuzuru eneo lolote na taifa. Amefichua […]

MWANABLOGU MAHAMANI KWA ‘KUMCHAFULIA JINA MCA

Mwanablogu Boniface Ohindo aliyekamatwa kwa tuhuma za kumchafulia jina mwakilishi wadi wa Yimbo East eneo bunge la Bondo Francis Otiato anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii. Afisa wa DCI eneo la Bondo Reuben Onchoka, amesema maafisa wa DCI walimkamata Ohindo baada ya mwakilishi wadi huyo kupiga ripoti akilalamikia madai ya mshukiwa kuchapisha habari potovu kuhusu utekelezaji wa […]

HATRICK YA LEWANDOWSKI YAWAINUA BARCA

Robert Lewandowski alifunga mara 3 na kuisaidia Barcelona kupata pointi 3 muhimu katika ushindi wao wa mabao 4-2 dhidi ya Celta Vigo, na kupunguza mwanya wa pointi baina ya mabingwa hao na viongozi Real Madrid ambao waliandikisha sare ya kutofungana na Rayo Vallecano. Kinda Lamine Yamal pia alifunga bao jingine, Marcos Rashford akitoa assists 2 […]

CITY WAWADHALILISHA WEKUNDU WA ANFIELD

Meneja wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola aliadhimisha mechi yake ya 1,000 kama mkufunzi kwa mtindo wa aina yake, baada ya vijana wake kuwatia darasani wekundu wa Anfield Liverpool kwa kichapo cha mabao 3-0 ugani Etihad. Kwenye mechi hiyo ambapo timu zote 2 zililenga kupunguza mwanya wa pointi na viongozi Arsenal, City walifanya ufungaji […]