MENEJA WA U17 ATAJA KIKOSI CHA MWISHO

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 William Muluhya ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 25 kitakachoiwakilisha Kenya katika mashindano ya AFCON ukanda wa CECAFA yatakayoandaliwa nchini Ethiopia baadaye mwezi huu. Vijana hao wa Junior Stars wamewekwa kwenye Group A, Pamoja na wenyeji Ethiopia, South Sudan, […]

GOR WATAMBA MBELE YA SERIKALI

Washikilizi wa rekodi ya ubingwa wa ligi kuu nchini KPL Gor Mahia, walichukua uongozi wa ligi hiyo hapo jana baada ya kutamba mbele ya Serikali walipowacharaza mabingwa watetezi Police FC kibano cha mabao 2-0 ugani Nyayo. Pambano hilo lililokuwa limepewa jina la Sirkal Derby, lilitarajiwa kutifua kivumbi ila likageuka fedhaha kwa maafande, ambao ni maajuzi […]

MURKOMEN: TOA HONGO UKAMATWE

Vijana wanaolenga kujiunga na vikosi vya polisi kwenye usajili ambao umeratibiwa wiki ijayo wamehakikishiwa kwamba zoezi hilo litaendeshwa kwa uwazi na usawa na watakaopatikana wakijihusisha na ufisadi watawajibishwa kisheria. Akizungumza katika kaunti ya Bomet, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen amewataka wananchi kuwaripoti watakaohusika na visa hivyo ili kuhakikisha uadilifu wa zoezi la usajili […]

SAMIA ASAKA SULUHU TANZANIA

Macho yameelekezwa kwa mrengo wa upinzani nchini Tanzania kuona iwapo utakubali wito wa serikali nchini humo kufanya mazungumzo kufuatia maafa makubwa ambayo yameshuhudiwa baada ya uchaguzi mkuu. Katika kikao na wanahabari, makamu wa rais wa Tanzania Emmanuel Nchimbi amesema mazungumzo hayo yanelenga kuimarisha maridhiano na mshikamano wa taifa hilo. Wito huu unajiri siku moja baada […]

PVK YALALAMIKIA UKIUKAJI WA HAKI ZA WAKENYA

Muungano wa Pentecostal Voice of Kenya PVK umeitaka serikali kutenga eneo maalum kuwawezesha wakenya kupiga ripoti kuhusu wenzao waliojeruhiwa au kuuawa nchini Tanzania wakati wa machakafuko ya uchaguzi, kufuatia ripoti kuhusu kuhangaishwa kwa raia wa Kenya nchini humo. Mwenyekiti wa PVK Apostle Peter Manyuru ambaye pia ni kiongozi wa kanisa la JTM, amelalamikia ukiukaji wa […]

WALIMU MAGHARIBI KUSUSIA KCSE KUFUATIA MAUAJI

Mtihani wa kitaifa wa kidato cha 4 KCSE unaingia wiki ya pili hii leo huku walimu kutoka eneo la Magharibi wakitishia kususia kusimamia mtihani huo kushinikiza uchunguzi katika mauaji ya mwalimu mkuu wa shule ya Munyuki Simon Isiaho. Mwili wa mwalimu huyo aliyetoweka kwa siku 6, uliopolewa katika Mto Kipkaren ukiwa na majeraha na dalili […]

RUTO AAHIDI “NEW SINGAPORE”, UPINZANI WAMKEJELI

Rais William Ruto amesisitiza kwamba angali na mpango wa kuimarisha Kenya kiuchumi na kuifanya iwe miongoni mwa mataifa yaliyostawi ulimwenguni, akiwataka wakenya kuwapuuza walio na shauku kuhusu mpango huo. Akizungumza katika eneo la Maralal kaunti ya Samburu, Rais Ruto ametetea hoja hiyo, akisema ana mpango maalum wa kufanikisha ndoto hiyo. Wakati uo huo, viongozi wa […]

6 stratégies essentielles pour choisir le meilleur casino en ligne avec Reseau Obepine.Fr

6 stratégies essentielles pour choisir le meilleur casino en ligne avec Reseau Obepine.Fr Choisir un casino en ligne n’est pas toujours simple. Le marché regorge d’offres alléchantes, mais toutes ne sont pas fiables. Reseau Obepine.Fr a passé au crible des dizaines de sites pour vous offrir une sélection sûre et transparente. Dans cet article, nous […]

ODM YASHINIKIZA HAKI KWA WAATHIRIWA

Tukiwa bado katika masuala ya haki, chama cha ODM kimeitaka serikali kuharakisha fidia kwa familia zilizowapoteza wapendwa wao wakati wa maandamano nchini jinsi ilivyokubalika katika mkataba wa maelewano ya kisiasa baina ya chama hicho na UDA. Wito huo ulitolewa kwenye hafla ya kumkumbuka aliyekuwa kinara wa ODM Raila Odinga, viongozi wakiitaka mahakama kuweka mbele haki […]

RIPOTI YA IMLU KUHUSU MAUAJI VITUONI

Watu 17 walifariki katika seli za polisi huku vifo vingine 59 vikihusishwa na na polisi kutumia nguvu kupita kiasi katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Katika ripoti yake, shirika huru la kimatibabu IMLU limeitaka serikali kuchukua hatua, ikizingatiwa kuwa nyingi ya familia za waathiriwa bado zinasaka haki. Haya yanajiri huku seneti ikijadili hoja kuhusu sheria […]