ATWOLI AWASUTA WANAOIBUA MADAI KUHUSU KIFO CHA RAILA

Katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli amewasuta baadhi ya viongozi wanaoibua madai kuhusiana na kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga. Atwoli amesema kuwa Raila hakuwa mtu wa kawaida na alikuwa na heshima zake kisiasa na hivyo kuibua madai yasiyo na msingi kuhusiana na kifo chake ni kutofanyia haki familia yake. Aidha, amewaomba wale wanaosema […]

WIZARA YA AFYA YAONYA KUHUSU MLIPUKO WA MAGONJWA KISA TAKATAKA

Wizara ya afya imesema kuwa wakenya wengi wako katika hatari ya maambukizi ya magonjwa kutokana na ongezeko la taka zinazotupwa ovyo ovyo. Katibu mkuu katika wizara ya afya Mary Muthoni amesema kuwa kwa sasa wakenya hasa walio katika maeneo ya miji ndio walio katika hatari kubwa ya mlipuko wa magonjwa hayo. Aidha takwimu zimeonyesha kuwa […]

SERIKALI YATOA FEDHA ZA UFADHILI KWA MUHULA WA PILI

Serikali imetoa shilingi bilioni ishirini na tatu nukta nne za ufadhili kwa shule za umma kabla ya kufunguliwa kwa muhula wa pili Jumatatu ili kuhakikisha shughuli za masomo zinaendelea bila usumbufu Katibu Mkuu wa Elimu ya Msingi Julius Bitok amesema fedha hizo zitaingia katika akaunti za shule kufikia Ijumaa ili kuwapa wasimamizi muda wa kujiandaa […]

IEBC: HATUTARUHUSU WANASIASA WANAOTUMIA WAHUNI KWENYE UCHAGUZI

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imewaonya wanasiasa wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi nchini dhidi kuwatumia vijana kuvuruga mikutano ya kisiasa. Akizungumza kwenye mkutano na washikadau kaunti ya Turkana, Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon amesema wanasiasa watakaopatikana wakijihusisha na kutumia wahuni hawataruhisiwa kuwania wadhifa wowote nchini. Kauli hiyo inajiri huku kukiwa na shinikizo la […]

RUTO AHOJI UFANISI WA UMOJA WA MATAIFA

Rais William Ruto ameibua wasiwasi kuhusu ufanisi na uaminifu wa Umoja wa Mataifa akisema chombo hicho kinakabiliwa na changamoto katika kudhibiti mivutano ya kisiasa duniani Akizungumza katika chuo kikuu cha LUISS nchini Italia Rais amesema mfumo wa kimataifa wa amani na usalama unaoongozwa na Umoja wa Mataifa unaonekana kudhoofika huku nguvu za mataifa makubwa zikichukua […]

GHARAMA YA MAFUTA: IMF YAONYA HALI YA UCHUMI WA KENYA

Shirika la fedha duniani (IMF) limerekebisha mtazamo wake wa kiuchumi kwa mataifa ya kusini mwa Jangwa la Sahara kushuka, ikiwa ni pamoja na makadirio ya Kenya, kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta hivi majuzi ambayo inaangazia kudorora kwa uchumi. Katika mtazamo wake wa hivi punde wa uchumi wa Kikanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, IMF imebainisha kuwa ingawa […]

BRIGHTON YAIDUWAZA CHELSEA EPL

Timu ya Brighton iliikalifisha Chelsea kwa kichapo cha mabao 3-0 na kuiruka kwenye msimamo wa jedwali la ligi kuu nchini Uingereza, EPL, na hivyo kuweka hai matumaini ya kushiriki michezo ya bara Ulaya msimu ujao huku ikimpalia makaa meneja wa Chelsea Liam Rosenior. Mabao ya Ferdi Kadioglu, Jack Hinshelwood na Danny Welbeck yaliipandisha Brighton hadi […]

LEICESTER CITY WASHUSHWA LEAGUE ONE

Klabu ya Leicester City imeshushwa daraja kutoka Championship hadi League One, miaka 10 baada ya kushinda ligi kuu ya Uingereza, EPL, miaka 5 tangu kushinda taji la FA, na msimu mmoja tu baada ya kushushwa daraja kutoka EPL. Hatma yao ilitiwa muhuri jana usiku baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Hull City, […]

HARAMBEE STARLETS WAPANDA NGAZI YA FIFA

Timu ya taifa ya soka ya wanawake, Harambee Starlets juu kwa nafasi 5 na kufikia nafasi ya 128 duniani katika jedwali la FIFA kutokana na mchezo mzuri walioonyesha katika mashindano ya FIFA Series yaoliyokamilika wiki jana jijini Nairobi. Kupanda huko kumetokana na ushindi dhidi ya India waliokuwa wameorodheshwa katika nafasi ya 69, na kufungwa mabao […]

CAVB: KCB KUPEPERUSHA BENDERA YA KENYA FAINALI

Klabu ya voliboli KCB itaiwakilisha Kenya katika fainali za mashindano ya ubingwa wa klabu za voliboli za wanawake barani Afrika jijini Cairo, Misri, kufuatia ushindi dhidi ya wenzao kutoka nchini, Kenya Pipeline seti 3-1 katika semi fainali za mashindano hayo hapo jana. Wanabenki hao walikabiliwa na ushindani mkali, wakikabana seti 1-1 kabla ya KCB kushinda seti za […]