WANGA A ANDIKA BARUA YA HISIA KWA ORENGO

Gavana wa Kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga ameandika barua ya wazi yenye hisia kwa Gavana wa Kaunti ya Siaya James Orengo akisema kauli zake za hivi karibuni zilimuumiza na kumfedhehesha. Katika taarifa hiyo, Wanga amesema anaongea kama mtu binafsi na si kama Gavana wa Homa Bay wala kama mwenyekiti wa chama cha ODM. Amesema alikaa […]

ORENGO ASEMA MAISHA YAKE YAKO HATARINI

Gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo amesema maisha yake yako hatarini baada ya serikali kuondoa walinzi wake bila maelezo. Akizungumza na kituo kimoja humu nchini, Orengo amesema Inspekta Jenerali wa Polisi anapaswa kuwajibika iwapo jambo lolote litamtokea. Orengo amesema maafisa wake tisa wa usalama waliokuwa wakimhudumia katika kaunti za Siaya na Nairobi waliondolewa ghafla Jumatano jioni bila sababu […]

RUTO KUKUTANA NA WADAU WA SEKTA YA USAFIRI

Rais William Ruto ameanza ziara ya maendeleo ya wiki moja katika eneo la Pwani huku shinikizo likiongezeka la kuzuia mgomo mpya wa kupinga bei ya mafuta. Ruto aliyerejea nchini kutoka ziara rasmi katika mataifa ya Azerbaijan na Kazakhstan, anatarajiwa kukutana na wadau wa sekta ya usafiri kujadili ongezeko la gharama za mafuta na athari zake kwa uchukuzi. Wawakilishi wa […]

UEFA YAPANGA MFUMO MPYA WA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2030

UEFA imetangaza mfumo mpya wa kufuzu kwa kombe la dunia mwaka 2030 utakaoiga mfumo unaotumika katika UEFA Champions League. Mfumo huo utakuwa na ngazi mbili ambapo mataifa 36 bora yatawekwa katika Ligi ya Kwanza na kugawanywa kwenye makundi matatu yenye timu 12 kila moja. Timu zitacheza mechi sita dhidi ya wapinzani tofauti, huku mataifa yatakayomaliza juu yakifuzu […]

AUSTIN ODHIAMBO AAMINI HARAMBEE STARS WAKO TAYARI

Kiungo Austin Odhiambo amesema Harambee Stars iko tayari kukabiliana na mataifa makubwa barani Afrika katika kufuzu kwa AFCON 2027. Kenya imepangwa kundi moja na Afrika Kusini , Guinea pamoja na Eritrea katika kundi linalotajwa kuwa gumu. Licha ya Kenya kufuzu moja kwa moja kama mwenyeji pamoja na Uganda na Tanzania, timu hiyo itashiriki mechi za kufuzu ili kujiweka […]

APS BOMET YAICHAPA BANDARI KWA MABAO MAWILI

Mshambuliaji Hillary Juma aliiongoza APS Bomet FC kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bandari FC katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Kwale. Mechi hiyo ndiyo pekee ya ligi kuu kuchezwa baada ya FKF kuahirisha michezo mingine kutokana na changamoto za usafiri zilizosababishwa na vurugu za sekta ya uchukuzi. Juma alifunga bao la kwanza dakika ya […]

OKIDI AAMINI MOMBASA UNITED ITASHINDA DERBY

Kocha wa Mombasa United Peter Okidi amesema ana imani kubwa timu yake itaibuka na ushindi dhidi ya Mwatate United katika mechi ya derby itakayochezwa Jumapili katika Uwanja wa Wundanyi. Okidi amesema ushindi wao wa mabao 2-1 dhidi ya Nairobi City Stars umeongeza morali na kuimarisha mshikamano ndani ya kikosi. Kocha huyo pia amewataka washambuliaji kutumia […]

TUJU ASALIA MASHAKANI

Mahakama kuu imesitisha ombi la aliyekuwa  Waziri wa zamani na katibu mkuu wa chama cha Jubilee  Raphael Tuju la kusimamisha mnada wa  baadhi ya mali zake zilizopo Karen jijini Nairobi, Mahakama hiyo inasema haiwezi kubatilisha uhamisho wa mali ambao tayari ulikuwa umefanyika kisheria katika mchakato wa kurejesha deni analodaiwa na Benki. Katika uamuzi huo, Jaji Moses Ado […]

MSHUKIWA WA  KIFO CHA RECHAEL ATAENDELEA KUSALIA KOROKORONI KWA SIKU 21

Wachunguzi wa kesi za jinai DCI wanaopeleleza kesi ya mauaji ya mwanamziki Rechael Wandeto wameomba mahakama kuwapa siku 21 kuendelea kumzuilia mshukiwa Josiah Njeru Njiri aliyekamatwa jana kwa kuhusishwa na tukio la kuchomwa moto kwa mwanamziki huyo aliyeaga dunia  alipokuwa akipokea matibabu  katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta. Njiru ambaye ni dereva wa teksi amefikishwa […]

RAIS RUTO AONGOZA HAFLA YA KUGAWANYA HATI MILIKI ZA ARDHI MOMBASA

Rais William Ruto amekitaja kifo cha  mwanamziki wa injili Rechael Wandeto kuwa kilichangiwa na siasa za ukabila na chuki  nchini. Akizungumza katika kaunti ya Mombasa wakati wa kugawanya hati miliki za ardhi Ruto amekosoa upinzani kwa kuendeleza siasa ambazo amesema zinachangia migawanyiko na chuki niongoni mwa wakenya akisema wote waliohusika kwa mauaji ya Wandeto watakabidhiwa […]