USIMAMIZI MBAYA WA MECHI WAKOSOLEWA KPL

Washikadau katika sekta ya kabumbu nchini wamelalamikia madai ya uendeshaji mbaya wa mechi za ligi kuu ya soka nchini, KPL, wakilitaka shirikisho la soka FKF kuwachukulia hatua marefa wanaokiuka sheria za kandanda. Miongoni mwao ni mwenyekiti wa klabu ya Gor Mahia Ambrose Rachier, akisema mwenendo huo unaiharibia jina soka ya Kenya. Rachier amehusisha usimamizi huo […]

MURKOMEN AWATETEA POLISI DHIDI YA UVAMIZI NYERI

Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, ameitetea idara ya polisi kuhusiana na uvamizi wa kanisa moja kaunti ya Nyeri wakati wa ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua mapema mwaka huu. Akiwa mbele ya bunge, Murkomen amesema uvamizi huo ulisababishwa na uhasama wa kisiasa miongoni mwa viongozi wa kisiasa wa eneo hilo, […]

MATUMIZI YA FEDHA IKULU YAWASHANGAZA WACHANGANUZI

Hofu imeibuliwa kuhusu ongezeko la matumizi ya fedha katika afisi ya Rais William Ruto, ikibainika kuwa kufikia mwezi Juni mwaka huu, afisi hiyo itakuwa imetumia takribani shilingi bilioni 100, kiasi cha fedha zinazotumika kuendesha afisi yake, ile ya naibu rais, afisi ya mkuu wa mawaziri na wizara mbali mbali. Kwa mujibu wa takwimu, kuna ongezeko […]

MIANYA YA UFADHILI WA MASOMO

Maswali yameibuka kuhusu gharama ya kufadhili masomo katika shule za umma, ikibainika kuwa wanafunzi milioni 3.4 walikosa ufadhili katika kipindi cha kati ya mwaka 2020-2024 kufuatia hatua ya serikali kukosa kutuma mgao wa shilingi bilioni 117 kufanikisha masomo ya bila malipo. Kulingana na ripoti ya mkaguzi wa hesabu za serikali, serikali inaendelea kulemewa na mzigo […]

SHA YAAHIDI BIMA BORA KWA WALIMU KUEPUSHA MGOMO

Huenda mgomo wa walimu wa shule za sekondari msingi JSS uliokuwa ukitishia kusambaratisha masomo kuanzia wiki ijayo, ukasitishwa, kufuatia hatua ya bima ya SHA kuahidi kushughulikia malalamishi ya walimu hao kuhusiana na huduma za matibabu chini ya bima hiyo. Kwenye mkutano na viongozi wa miungano ya kutetea maslahi ya walimu, KNUT na KUPPET, SHA imesema […]

WINGU LA UFUSADI LATANDA BUNGENI

Idara ya bunge sasa inakabiliwa na wakati mgumu kujitakasa kutokana na madai ya ufisadi dhidi yake, tuhuma kwamba maseneta hupokea rushwa kutoka kwa magavana zikiingia katika bunge la kitaifa. Wa hivi punde kuhusishwa na ufisadi ni mbunge wa Bumula Jack Wamboka, ambaye ametimuliwa kutoka wadhifa wa mwenyekiti wa kamati ya uwekezaji wa umma kutokana na […]

GUARDIOLA ASEMA HANA PRESHA MSIMU HUU

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amesema hana wasiwasi wowote msimu huu akieleza kuwa hali ni tofauti kabisa na ilivyokuwa msimu uliopita Amesema msimu uliopita ulikuwa na presha kubwa kwani alihofia kushindwa kuipeleka timu katika mashindano ya Ulaya lakini sasa mambo yako shwari zaidi Guardiola ameongeza kuwa kwa sasa timu iko tulivu na yenye kujiamini […]

LIVERPOOL KARIBU KUMALIZANA NA KONATE KUHUSU MKATABA MPYA

Klabu ya Liverpool iko karibu kufikia makubaliano kamili na beki Ibrahima Konate kuhusu kusaini mkataba mpya baada ya mazungumzo kuendelea vizuri Mazungumzo hayo yamepata msukumo mpya kufuatia kusimama kwa mawasiliano yaliyokuwa yakihusisha Real Madrid mwezi Novemba hatua iliyofungua nafasi kwa Liverpool kuendelea na mazungumzo Ingawa makubaliano hayajakamilika rasmi bado klabu hiyo ina imani kubwa kuwa […]

RACHIER AHOJI VIWANGO VYA MAREFA KABLA YA MASHEMEJI DERBY

Mwenyekiti wa Gor Mahia Ambrose Rachier ameibua wasiwasi kuhusu viwango vya uamuzi wa marefa katika ligi kuu ya soka nchini siku chache kabla ya dabi ya Mashemeji inayotarajiwa kufanyika Jumapili Aprili ishirini na sita Rachier amehoji uthabiti wa maamuzi ya waamuzi akionya kuwa makosa katika hatua hii ya msimu yanaweza kuathiri pakubwa mbio za ubingwa […]

BANDARI FC YATULIZA TAHARUKI BAADA YA KISA KASARANI

Klabu ya Bandari FC imejitokeza kutuliza hali kufuatia tukio la mvutano lililoshuhudiwa katika mechi yao dhidi ya Gor Mahia uwanjani Kasarani mwishoni mwa wiki Kocha mkuu Bernard Mwalala amekiri kuwa mwitikio wa wachezaji wake baada ya uamuzi tata wa penalti haukuwa wa kawaida akisisitiza kuwa nidhamu na heshima ni misingi muhimu ya klabu hiyo Mwalala […]