RUTO ATANGAZA PUNGUZO LA BEI YA DIESEL KUANZIA MWEZI UJAO

Rais William Ruto ametangaza kuwa bei ya dizeli itapungua kwa shilingi 10 kwa lita katika marekebisho yajayo ya bei ya mafuta ya Juni–Julai. Akihutubia taifa kutoka Ikulu ya Mombasa, Rais amesema hatua hiyo inalenga kupunguza makali ya gharama ya maisha kwa wananchi, wafanyabiashara na sekta ya usafiri. Amesema serikali tayari imetumia shilingi bilioni 13.7 katika […]

ARTETA AELEZA FURAHA YA KUTWAA UBINGWA

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta amesema kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England ni moja ya hisia bora kuwahi kupata maishani mwake. Arteta amesema hakuweza kutazama mechi ya Manchester City lakini alikuwa akisikia kelele kutoka ndani kabla mwanawe kufungua mlango na kumkimbilia huku akilia. Kocha huyo amesema mwanawe alimwambia kuwa Arsenal wametwaa ubingwa wa EPL kauli iliyogusa wengi baada ya Arsenal kutwaa ubingwa huo […]

RONALDO ASHINDA TAJI LAKE LA KWANZA SAUDI ARABIA

Cristiano Ronaldo ameshinda taji lake la kwanza la ligi nchini Saudi Arabia baada ya kuiongoza Al-Nassr kupata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Damac FC katika mechi ya mwisho ya msimu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 41 alifunga mabao mawili muhimu katika ushindi huo uliowapa taji la muda mrefu ambalo alikuwa akilikosa katika misimu miwili iliyopita […]

MBIO ZA KUPANDA LIGI KUU ZAPAMBA MOTO NSL

Mbio za kupanda moja kwa moja hadi Ligi Kuu ya FKF zimezidi kupamba moto katika Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza huku timu tatu zikifungana kileleni zikiwa zimesalia mechi tano pekee. 3K FC, Migori Youth na Mombasa United zote zina alama 68 baada ya kucheza mechi 33, huku 3K FC wakiongoza kwa tofauti ya mabao. […]

NAIROBI CITY MARATHON YAVUNJA REKODI YA WASHIRIKI

Mashindano ya tano ya Nairobi City Marathon yatakayofanyika Juni 7 yamevutia rekodi ya washiriki 17,000 kutoka nchi 75 duniani, yakionyesha ukuaji mkubwa wa umaarufu wa tukio hilo Mashindano hayo yatakuwa na vipengele vinne ambavyo ni marathon ya kilomita 42, nusu marathon, mbio za kilomita 10 na 5, zikiwapa fursa wanariadha wa viwango tofauti kushiriki Mratibu […]

KRU YAWEKA MKAKATI WA KUIMARISHA RAGA YA WANAWAKE

Mwenyekiti wa chama cha Raga nchini Harriet Okach amesema kuwa kujenga utamaduni imara na endelevu wa rugby ya wanawake ni kipaumbele cha muda mrefu, huku akilenga kuinua mchezo wa wa wachezaji 15s kufikia kiwango cha mafanikio ya Sevens nchini Amesema mashindano ya Rugby Africa Cup yanayofanyika jijini Nairobi yanatoa nafasi muhimu ya ushindani na maendeleo, yakishirikisha Kenya, mabingwa watetezi […]

BIASHARA HARAMU YA NYAMA YA PUNDA YAENDELEA KAJIADO

Biashara haramu ya nyama na ngozi za punda imeendelea kushamiri nchini licha ya serikali kupiga marufuku uchinjaji wa kibiashara wa wanyama hao mwaka 2020. Katika eneo la Kimuka, wakazi walinasa lori lililokuwa likisafirisha nyama inayoshukiwa kuwa ya punda pamoja na ngozi zake kabla ya kuwashambulia watu wawili waliokuwa ndani ya gari hilo. Kamanda wa Polisi […]

WADAU WAPINGA BAADHI YA VIPENGELE VYA MSWADA WA FEDHA 2026

Wadau wanaoshiriki vikao vya maoni kuhusu Mswada wa Fedha 2026 wameilaumu serikali kwa kushindwa kurekebisha viwango vya ushuru wa mishahara maarufu kama PAYE pamoja na kuanzisha ushuru mpya kwa miamala ya fedha kupitia simu. Wakizungumza mbele ya Kamati ya Fedha na Mipango ya Bunge la Taifa la Kenya, Taasisi ya Wahasibu Walioidhinishwa Kenya (ICPAK) pamoja na Muungano […]

RUTO KULIHUTUBIA TAIFA HII LEO

Rais William Ruto anatarajiwa kulihutubia taifa wakati wowote kuanzia sasa huku Wakenya wakisubiri kwa hamu kauli yake kuhusu changamoto za kiuchumi zinazoendelea nchini. Tangazo hilo limetolewa na msemaji wa Ikulu Hussein Mohamed ambaye amesema Rais atazungumza na wananchi lakini hakufafanua ajenda kamili ya hotuba hiyo. Hotuba hiyo inajiri wakati nchi ikikabiliwa na shinikizo la kupanda kwa bei […]

NAULI ZAPANDA LICHA YA MAZUNGUMZO

Wasafiri kote nchini wanakabiliwa na gharama kubwa za usafiri baada ya nauli kupanda licha ya wadau wa sekta ya matatu kuahidi kutopandisha bei wakati mazungumzo yanaendelea. Hapa  jijini Nairobi baadhi ya nauli zimeongezeka kwa hadi asilimia 50 kufuatia matamshi ya awali ya waendeshaji wa usafiri wa umma. Serikali imetakiwa kushughulikia suala la bei ya mafuta huku baadhi ya viongozi […]