MICHEZO YA SHULE ZA UPILI ZIMESHIKA KASI

Michezo ya shule za sekondari muhula wa pili, ambayo inajumuisha Raga ya wachezaji saba (Rugby 7’s),kandanda, mpira wa vikapu 3×3, voliboli, mpira wa pete (netball) miongoni mwa mingine,imeng’oa nanga katika ngazi za kanda katika maeneo mbalimbali nchini. Kocha mkuu wa mabingwa wa zamani wa raga ya wachezaji saba ya Koyonzo Boys, EliudOkwemba, ametaja kuwa ana […]

POLICE FC WASUASUA KUBEBA LIGI KUU

Nguvu ya Kenya Police FC kwenye kilele cha Ligi Kuu ya FKF (FKF-PL) ilidhoofika Jumatano baada ya kupokea kichapo cha 2-1 kutoka kwa Kakamega Homeboyz katika mchuano wa nguvu nyingi katika uwanja wa Mumias Sports Complex. Homeboyz waliweka wazi nia yao mapema, huku Moses Shumah akifunga bao hilo dakika ya nane. Hata hivyo, vinara wa […]

BOLGNA WAWAPIKU AC MILAN

Wachezaji wa Bologna wamemaliza kiu chao cha miaka 51 cha Kombe la Italia baada yakuchukua ushindi wa bao 1 dhidi ya AC Milan mjini Rome. Kocha mkuu wa klabu hiyo, Vincenzo Italiano, aliyechukua usukani kutoka kwa ThiagoMotta, ameonyesha juhudi zake kwa kuleta utofauti wa historia hii iliyoanza kunakiliwa mwawa 1974 tangu kuanzishwa kwa mashindano ya […]

HOJA YA KUTOKUA NA IMANI NA SASHA IMEWASILISHWA

Chama cha Raga ya Kenya (KRU) kwa mara nyingine tena kimekumbwa na mzozo, huku hoja mpya ya kutokuwa na imani dhidi ya mwenyekiti Alexander “Sasha” Mutai ikitarajiwa kuwasilishwa kwenye Mkutano Mkuu Maalumu ujao (SGM). Vyanzo vya habari vinadokeza kuwa juhudi mahususi zinaendelea kumwondoa Mutai, ambaye muda wake wa umiliki tangu 2023 umebadilika kati ya kupata […]

KESI YA GACHAGUA YAAHIRISHWA IKISUBIRI MWELEKEO WA KOOME

Mahakama Kuu imeahirisha kesi ya kikatiba dhidi ya Rigathi Gachagua baada ya Mahakama ya Rufaa kubatilisha uteuzi wa jopo la majaji waliopaswa kusikiliza kesi hiyo, likisema ni Jaji Mkuu pekee mwenye mamlaka ya kufanya uteuzi huo. Hata hivyo, katika taarifa iliyotolewa na Naibu Msajili Msaidizi Mheshimiwa Beja Nduke, pande zote ziliarifiwa kuwa kesi hiyo imeahirishwa […]

ADA ‘DHALIMU’ ZAWAFUKUZA WAWEKEZAJI- KNCCI

Rais wa Chama cha Wafanyabiashara na Wenye Viwanda nchini Kenya (KNCCI), Dkt. Erick Rutto, amekosoa ongezeko la ada na masharti mengi yanayowakabili wajasiriamali wanapotaka kuanzisha biashara, akisema hali hii inakatisha tamaa wawekezaji na kuathiri mazingira ya biashara nchini. Akitolea mfano wa kampuni moja ya upakiaji wa chakula inayopanga kuanzisha shughuli zake katika Kaunti ya Kajiado, […]

SERIKALI YAKARIRI SHARTI ILIPWE

Serikali imesema inafanya kila iwezalo kuhakikisha wakopaji wote wa fedha kutoka hazina ya Hustler Fund wanalipa mikopo hiyo ili kuhakikisha hazina hiyo inawainua kiuchumi wakenya. Akizungumza mbele ya seneti, waziri wa mashirika na biashara ndogo ndogo na vya kadri Wycliffe Oparanya, amesema kufikia sasa shilingi bilioni 70 zimekopwa na wakenya milioni 25. Kufikia Oktoba mwaka […]

IPOA YASEMA WATEKAJI NYARA HAWAJULIKANI

Kitendawili cha utekaji nyara nchini kitasalia bila kuteguliwa kwa muda zaidi kufuatia kukiri kwa mamlaka inayoangazia utendakazi wa polisi IPOA kwamba hadi sasa wanaoendeleza uhalifu huo hawajafahamika ila uchunguzi unaendelea. Akiwa mbele ya kamati ya utawala na usalama wa kitaifa bungeni, mwenyekiti wa mamlaka hiyo Issak Hassan amesema kikwazo kikuu kwenye uchunguzi huo ni waathiriwa […]

KINDIKI ATETEA ‘UCHUNGU’ WA SUKARI

Huku hayo yakijiri, naibu Rais Kithure Kindiki ametetea mageuzi yaliyofanywa katika sekta ya kilimo cha miwa ikiwemo kukodishwa kwa viwanda 4 vya kusaka miwa kuwa mojawapo ya mikakati ya kuimarisha sekta hiyo. Ameyasema haya baada ya kupokea ripoti kuhusu sekta ya sukari, akitolea mfano wa kiwanda cha Mumias anachosema tayari matunda ya kukodishwa kwake yameanza […]

UCHUNGU WA SUKARI WAENDELEA KUJITOKEZA

Wabunge kutoka Magharibi mwa nchi wametishia kuelekea mahakamani ili kushinikiza kubatilishwa kwa mchakato wa kukodishwa kwa kiwanda cha miwa cha Nzoia, wakidai serikali imekiuka sheria katika kumkabidhi mwekezaji wa kibinafsi usimamizi wa kiwanda hicho. Wakizungumza na wanahabari jijini Nairobi, viongozi hao wameishutumu serikali kwa wanachosema kukosa uwazi katika mchakato huo. Miongoni mwao ni seneta wa […]