TRAVERS ASAJILIWA NA EVERTON

Everton ilimsajili kipa wa Ireland Mark Travers kutoka Bournemouth kwa mkataba wa thamani ya pauni milioni 4 ($5.3 milioni) siku ya Jumanne. Travers walikubali kandarasi ya miaka minne na klabu hiyo ya Ligi Kuu, ambayo itafungua uwanja wao mpya mwanzoni mwa msimu ujao. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alisema: “Ninajivunia sana na kufurahia […]

CITY WATIA KANDARASI NA PUMA

Manchester City wametia saini kandarasi mpya ya jezi mpya na Puma yenye thamani ya pauni bilioni 1 [Ksh 178 bilioni] katika kipindi cha miaka 10 ijayo. Upanuzi wa City wa mkataba wao na Puma unakuwa kama ushirikiano mkubwa zaidi wa kutengeneza jezi katika historia ya Ligi Kuu. Wakiwa wamekubali mkataba wa pauni milioni 65 kwa […]

OKWEMBA ANA MATUMAIANI YA KUNYAKUA TAJI LA RAGA

Kocha mkuu wa timu ya raga ya 7 ya Koyonzo Eliud Okwemba hana shauku ya kunyakua taji lao la kitaifa mwaka huu licha ya kupoteza taji la kanda wikendi iliyopita. The Stormers walishangazwa na mabingwa walioibuka washindi St. Peter’s Boys Mumias 19-12 huku Okwemba akighairi kupoteza kwao kwa makosa ya kibinafsi. Hata hivyo, mshindi wa […]

STARS WAIMARISHA MAANDALIZI YA CHAN

Nahodha msaidizi wa Harambee Stars, Boniface Muchiri amecheza chini ya kiwango huku Kenya ikiimarisha maandalizi ya mechi yao ya kwanza kwenye michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024. Kenya iko katika Kundi ‘A’ na mabingwa mara mbili DR Congo, wababe wa Afrika Kaskazini Morocco, pamoja na Angola na Zambia, washindani wawili wa Afrika wanaoshindana zaidi […]

HESHIMU MAHAKAMA, KOOME AWAAMBIA WAKOSOAJI

Jaji mkuu Martha Koome amelalamikia uingiliaji wa shughuli za idara ya mahakama na mashambulizi dhidi ya maafisa wa idara hiyo, akisema mwelekeo huo utaathiri utoaji haki kwa umma. Koome ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la kitaifa kuhusu haki, amewataka maafisa hao kusalia imara na kutekeleza majukumu yao bila upendeleo. Haya yanajiri huku waziri wa […]

RIPOTI YAFICHUA SHULE HEWA

Zaidi ya shule hewa 20 zimekuwa zikipokea mamilioni ya pesa katika kipindi cha miaka 4 iliyopita, mkaguzi wa hesabu za serikali Nancy Gathungu akiibua hofu kuhusu uwezekano wa wizara ya elimu kutumia mbinu hizo kufuja fedha za wakenya. Kwenye ripoti ya uchunguzi ulioendeshwa katika shule 400 nchini, mkaguzi huyo aidha amebaini kuwa shule hizo hazimo […]

HOFU YA UTEKAJI NYARA WEST POKOT

Hofu imetanda katika kaunti ya West Pokot baada ya wakazi kuibua madai kwamba kuna watu wanaolenga kuwateka nyara watoto eneo hilo kwa kutumia magari yasiyo na nambari za usajili na pikipiki. Wakiongozwa na mwakilishi wa wadi ya Kapenguria Richard Mastaluk, wakazi wamesema kuwa washukiwa wamekuwa wakiwalenga watoto majira ya asubuhi. Haya yanajiri wiki moja baada […]

MARAGA ATAKA POLISI WAFUNZWE KUHUSU HAKI

Pana dharura ya kuwapa maafisa wa polisi mafunzo kuhusu haki za kimsingi za kibinadamu ili kukabili ukiukaji wa haki hizo wakati wa maandamano nchini. Ni kauli ya aliyekuwa jaji mkuu David Maraga, akizungumza kwenye mahojiano na runinga moja nchini, ambako amekosoa hatua ya polisi kumrushia vitoza machozi alipojitokeza kudai haki kwa familia zilizowapoteza wapendwa wao […]

SERIKALI YACHUNGUZA UGONGWA HATARI MOMBASA

Serikali imewaondolea hofu wakazi wa Migadini kaunti ya Mombasa na taifa kwa jumla kuhusiana na mlipuko wa ugonjwa usiojulikana ambao umewaua wakazi 4 tayari, serikali ikisema inaendesha uchunguzi ili kubaini ugonjwa huo. Ugonjwa huo unaosababisha kuvimba kwa miili ya waathiriwa mbali na majipu yenye usaha, umezua hofu katika eneo hilo, wakazi wakiitaka wizara ya afya […]

NACADA YATAKA UMRI WA KUNYWA POMBE KUONGEZWA

Huenda umri wa kuanza kubugia pombe ukaongezwa kutoka miaka 18 hadi 21 iwapo mapendekezo yaliyotolewa na mamlaka ya Nacada yatapitishwa. Nacada pia inataka kupigwa marufuku kuwekwa kwa vituo vya kuuza pombe karibu na shule na kuzuia kuuzwa kwa pombe kupitia njia ya mtandao ambapo wanununuzi wanapelekewa nyumbani. Nacada pia inapendekeza kubuniwa kwa hazina ya kuwasaidia […]