CHELSEA KUKUTANA NA PSG KWENYE FAINALI

Paris St-Germain iliibomoa Real Madrid na kuandaa fainali ya Kombe la Dunia la Klabu ya Fifa dhidi ya Chelsea Jumapili. Mchezo huu wa nusu-fainali kwenye Uwanja wa MetLife ulikamilika kama shindano ndani ya dakika 24 huku washindi wa Ligi ya Mabingwa waliporarua timu ya Uhispania. Fabian Ruiz alifunga bao la kwanza dakika ya sita kufuatia […]

ULINZI STARS YAPATA MWENYEKITI MPYA

Timu ya FKF ya Ligi Kuu ya Ulinzi Stars imetangaza kumteua Luteni Kanali David Nganga kama mwenyekiti mpya wa klabu hiyo, na kuanzisha enzi mpya ya uongozi baada ya hali mbaya ya 2024. Timu hiyo ya kijeshi, ambayo mara ya mwisho ilinyakua taji la Ligi Kuu ya Kenya mwaka wa 2010, ilivumilia kampeni ngumu, ikimaliza […]

MUSINGU YAPATA PIGO KWA KUPATIKANA NA HATIA

Timu ya soka ya Shule ya upili ya wavulana ya Musingu High imepata pigo baada ya kupatikana na hatia ya kuwachezesha wanafunzi wasiofaa kisheria na kubanduliwa kutoka kwa michezo hiyo. Hii ni baada ya mahasimu wao Kakamega High kuwasilisha kesi ya rufaa dhidi yao wakidai Musingu walitumia Wachezaji ambao wamepitisha umri hitajika wa Wachezaji wasiozidi […]

DUALE AIMBA WIMBO WA RAIS RUTO

Waziri wa afya Aden Duale amekariri kauli ya Rais William Ruto kwamba utawala wa Kenya Kwanza hautaruhusu vitisho kutoka kwa wapinzani wake, akisema mambo sasa yatachukua mkondo tofauti kuenda mbele. Katikia mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini, Duale ametetea kauli ya Rais Ruto ya kuwataka polisi kuwafyetulia risasi miguuni wanaovamia mali wakati wa maandamano. […]

TAIFA LAUGUA SERIKALI, UPINZANI WAKILAUMIANA

Wakenya wameachwa gizani kuhusu lengo na wahusika wa mauaji na uharibifu wa mali wakati wa maandamano, serikali na upinzani zikiendelea kurushiana lawama bila kukubali kuwajibika. Kulingana na Rais William Ruto, upinzani una njama ya kuipindua serikali, akiapa kwamba kamwe serikali yake haitaruhusu jaribio hilo kufanyika. Hata hivyo, mrengo wa upinzani ukiongozwa na aliyekuwa naibu Rais […]

SABA SABA YAVUNJA HISTORIA

Maandamano ya kuadhimisha siku ya Saba Saba yametangazwa kuwa yenye maafa makubwa zaidi kuwahi kutokea katika maandamano humu nchini, idadi ya waliouawa ikipanda hadi watu 32. Kulingana na mashiirika ya kutetea haki za kibinadamu ikiwemo tume ya KNHCR, jumla ya watu 115 wameuawa kwenye maandamano kati ya Juni mwaka jana hadi sasa, familia katika maeneo […]

NYAMBUA LENGO LAKE NI KUSHINDA

Nahodha wa timu ya Kenya 15s George Nyambua anasema lengo pekee la timu hiyo katika Kombe la Afrika la Raga wiki hii ni kufuzu kwa Kombe lijalo la Dunia linalotarajiwa kuchezwa Australia mnamo 2027. Timu ya Kenya Simbas itashiriki katika mechi za kufuzu zinazohusisha timu nane katika mashindano ya Kombe la Raga la Afrika 2025. […]

VILABU VINANE VIAJIANDAA KWA MSURURU WA KITAIFA WA RAGA

Kabla ya Msururu wa Kitaifa wa raga ya wachezaji saba kila upande ulioratibiwa kuanza wiki mbili zijazo, vilabu vinane vikiongozwa na mabingwa watetezi Kenya Harlequin vitajiandaa kwa mashindano hayo kwa mchuano wa siku moja uliopewa jina la “RUFF N TUFF” Jumamosi katika Uwanja wa Ngong Racecourse. Michuano hiyo inayoandaliwa na wenyeji Nondescripts RFC na kufadhiliwa […]

CHELSEA WAWABWANGA FLUMINENSE

The mighty Blues Chelsea ilitinga fainali ya Kombe la Dunia la Klabu huku mabao mawili ya mchezaji mpya Joao Pedro yakisaidia kuzamisha Fluminense ya Brazil. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, akicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya klabu yake ya utotoni, alipachika bao la kwanza dakika ya 18 baada ya mlinzi wa zamani […]

KIBWAGE AITWA KWNYE KIKOSI CHA HARAMBEE STARS

Beki wa Tusker FC anayetatizika, Michael Kibwage ana furaha baada ya kujumuishwa katika kikosi cha muda cha kocha Benni McCarthy cha wachezaji 30 kwa ajili ya Michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN). Kibwage amekuwa na msimu mgumu, baada ya kukosekana kwa miezi miwili kwenye mzunguko wa pili wa ligi kuu kutokana na jeraha la paja […]