OCHIENG AFURAHISHWA NA UCHEZAJI WA TIMU YAKE

Kocha mkuu wa Strathmore Blades Tony Ochieng amefurahishwa na uchezaji wa timu yake wikendi katika mechi za Ligi Kuu ya Kikapu ya Kitaifa ya Kenya baada ya kushinda moja na kupoteza nyingine. Wanafunzi hao waliwashinda NBK Phoenix 70-55 kabla ya kuangukia 76-86 dhidi ya wenzao wa chuo kikuu cha UoN Terror wikendi. Wakati huo huo, […]

POLOKWANE WAKO MBIONI KUMSAJILI KAHIRO KUTOKA KCB

KLABU ya Polokwane City FC ya Afrika Kusini na vigogo wa Ligi Kuu ya Zambia, Nkana Red Devils, wanaongoza katika mbio za kuwania saini ya mshambuliaji wa KCB FC, Francis Kahiro. Vilabu vyote viwili vimempa mchezaji huyo mkataba wa miaka miwili lakini bado hajaamua ni wapi anapopendelea. Mshambulizi huyo alitumia wiki kadhaa nchini Afrika Kusini […]

BUYACHI ASEMA ANAPATA CHANGAMOTO KWA MAZOEZI

Kocha msaidizi wa Menengai Oilers, Lawi Buyachi anasema kuwa anakabiliwa na changamoto kubwa katika mazoezi ya kujiandaa kwa Mzunguko ujao wa Kitaifa wa Sevens. Kulingana na Buyachi, wavulana wake wamekuwa kambini kwa zaidi ya wiki sita sasa na wako katika hali ya kawaida, wiki tatu kabla ya mzunguko kuanza. Mtaalamu huyo wa zamani wa Kisumu […]

TUTATEUA KOCHA WA KIMATAIFA

Mwenyekiti wa Gor Mahia Ambrose Rachier amefichua kwamba mabingwa hao mara 21 wa Kenya hawana uwezekano wa kuteua kocha wa ndani, akitaja changamoto za zamani na shinikizo kubwa kutoka kwa mashabiki. Nafasi ya ukocha katika klabu ya K’Ogalo kwa sasa iko wazi baada ya kamati kuu ya klabu hiyo kuvunja benchi nzima ya ufundi hivi […]

MURKOMEN ATETEA KUSAMBARATIKA KWA SHUGHULI

Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen ametetea hatua ya polisi kufunga barabara na kuwazuia wakenya kuendelea na shughuli zao za kila siku hapo jana, akisema hatua hiyo ililenga kuwahakikishia wakenya hao usalama wao. Katika kikao na wanahabari, Murkomen vile vile amewasifia polisi walioshika doria hapo jana, akisema walijitolea katika kulinda mali na maisha ya […]

MAANDAMANO: ODINGA APENDEKEZA KURA YA MAONI

Kinara wa ODM Raila Odinga amependekeza mazungumzo ya kitaifa kufanywa yakiwaleta Pamoja wadau kutoka vizazi tofauti, ili kutatua masuala yanayoibuliwa na vijana wa kizazi cha Gen Z ambayo sasa yametishia mshikamano wa nchi. Akizungumza na wanahabari, Odinga amelalamikia changamoto zilizoko ikiwemo utendakazi wa polisi, licha ya maandamano ya Saba Saba ya mwaka 1990 kushinikiza mageuzi […]

WAFANYABIASHARA WAACHWA NA HASARA

Wafanyabiashara katika maeneo hasa Nairobi, Meru, Kirinyaga, Murang’a, Kiambu, Nakuru, Machakos na Kajiado wameendelea kukadiria hasara ya mamilioni ya pesa baada ya biashara zao kuporwa huku zingine zikiteketezwa na makundi ya wahundi waliotumia maandamano ya Saba Saba kutekeleza uhalifu. Miongoni mwa taasisi za serikali zilizochomwa ni afisi ya NG-CDF ya Kirinyaga Central, idara ya polisi […]

OJWANG KUZIKWA LEO

Viongozi mbali mbali wameratibiwa kujiunga na waombolezaji katika shule ya msingi ya Nyawango kaunti ya Homa Bay katika kumsindikiza mwendazake Albert Ojwang ambaye ni bloga na mwalimu aliyeuawa mikononi mwa polisi mwezi jana. Mwili wa Ojwang uliwasilishwa eneo hilo hapo jana, hafla iliyogeuka kuwa taharuki na ghadhabu baada ya waombolezaji kuchukua mwili wake kwa nguvu […]

WITO WA WANAHARAKATI MAKUENI KWA WABUNGE

Wanaharakati katika kaunti ya Makueni wamewataka wabunge kuutupilia mswada unaolenga kupiga marufuku maandamano karibu na baadhi ya taasisi za serikali uliowasilishwa bungeni na mwakilishi wa kike kaunti ya Nairobi Esther Passaris. Kulingana nao, mswada huo unakandamiza haki ya maandamano na ikiwa utapitishwa basi utalirejesha nyuma taifa. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KAUNTI ZAHIMIZWA KUWASILISHA PENSHENI YA WAFANYAKAZI

Katika juhudi za kuwaepushia mahangaiko wafanyakazi wa kaunti wanaostaafu, serikali za kaunti zimehimizwa kuwasilisha malipo ya pensheni kwa hazina ya pensheni ya serikali ili kuwawezesha wafanyakazi hao kujitegemea baada ya kustaafu. Akizungumza kwenye mkutano wa kitaifa wa hazina hiyo, katibu wa muungano wa wafanyakazi wa kaunti Roba Duba, amesema hadi sasa muungano huo unazidai kaunti […]