WAPITA NJIA, BODA BODA 6 WAUAWA KERICHO-KISUMU

Watu 6 wamefariki papo hapo huku wengine 4 wakijeruhiwa baada ya kugongwa na lori katika soko la Kipsitet kwenye barabara ya Kericho kuelekea Kisumu usiku wa kuamkia leo. Kamanda wa polisi kaunti ndogo ya Sigowet/Soin Lawrence Kisini amesema lori hilo lilikuwa likielekea upande wa Kisumu kabla ya kupoteza mwelekeo na kuwagonga wapita njia na wahudumu […]

ARSENALI WAANZA VYEMA KWA LIGI YA MABINGWA

Wachezaji wa akiba wa Arsenal Gabriel Martinelli na Leandro Trossard walitinga katika hatua ya mwisho na kupata ushindi wa 2-0 dhidi ya Athletic Bilbao katika mechi yao ya ufunguzi ya Ligi ya Mabingwa Jumanne. Waliofuzu kwa nusu fainali msimu uliopita walianza kwa ushindi katika nchi hiyo ya Basque walipokabiliana na mchezo mkali katika uwanja wa […]

QUEENS WATAWAZWA WASHINDI WA CECAFA

JKT Queens ya Tanzania ilitawazwa washindi wa kombe la CECAFA kwa Wanawake siku ya Jumanne baada ya kuifunga Rayon Sports ya Rwanda kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Michezo wa Moi, Kasarani, Nairobi. Pambano hilo gumu liliifanya JKT Queens kutawala mpira, na kufanya majaribio kadhaa lakini akili nzuri ya kipa wa Rayons Sports […]

KENYA YATAWALA KWA JUKWA LA USHINDI

Ushindi wa kikosi cha Kenya katika Mashindano ya Riadha ya Dunia huko Tokyo ulishika kasi huku nyota watatu wa masafa ya kati-Emmanuel Wanyonyi, Kelvin Kimutai Loti, na Nicholas Kiplangat Kebenei-walifuzu kwa nusu-fainali ya mita 800 wanaume. Wanyonyi, mmoja wa wawaniaji wa medali ya dhahabu, alinyakua nafasi ya kwanza baada ya kudumisha utulivu. Kelvin Kimutai Loti […]

SHA IMEVUNJA REKODI YA NHIF, MWANGANGI

Shilingi bilioni 70 zimekusanywa chini ya mamlaka ya afya ya jamii SHA tangu kuanzishwa kwake, ikilinganishwa na shilingi bilioni 45 zilizokusanywa katika muda wote wa bima ya zamani ya afya NHIF. Haya ni kulingana na afisa mkuu mtendaji wa SHA Dakta Mercy Mwangangi, akihojiwa na runinga moja nchini ambako ameweka wazi kwamba shilingi bilioni 8 […]

FAHARI YA KENYA JAPAN, ULIMWENGUNI

Kenya inaendelea kusherehekea ushindi wa mwanariadha Faith Kipeygon aliyeishindia nchi nishani ya dhahabu hapo jana katika mbio za mita 1,500 kwenye mashindano ya ubingwa wa dunia jijini Tokyo Japan. Kipyegon ambaye sasa ameshinda ubingwa huo mara 4, alimwongoza mkenya mwenzake Dorcus Ewoi aliyemaliza katika nafasi ya 2 na hivyo kufikisha jumla ya medali 5 kwa […]

USAJILI WA MAKURUTU WA POLISI KUANZA

Zoezi la kuwasajili makurutu watakaojiunga na vitengo mbali mbali vya polisi inatarajiwa kuanza muda wowote baada ya mwafaka kupatikana kufuatia mazungumzo kati ya bunge, idara ya polisi NPS na tume ya huduma kwa polisi NPSC. Akizungumza baada ya mkutano wa faragha, mwenyekiti wa kamati ya utekelezaji wa katiba bungeni Caroli Omondi, amesema wana ufahamu kuhusu […]

MGOMO WA WAHADHIRI WAANZA

Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma nchini zinatarajiwa kusambaratika kuanzia leo kufuatia mgomo wa wahadhiri ambao umenza rasmi usiku wa manane baada ya makataa yao kwa serikali kukamilika. Katibu mkuu wa muungano wao UASU Dakta Constantine Wasonga, amesema juhudi zao kufanya mazungumzo na serikali zimefeli, mwenzake wa KUSU Charles Mukhwana, akisema hawatarejea kazini […]

MTOTO WA MIAKA 6 ATEKETEA KAKAMEGA

Polisi katika kaunti ya Kakamega wanachunguza kisa ambapo mvulana mwenye umri wa miaka 6 ameteketea hadi kufa katika nyumba yao mtaani Bukura eneo bunge la Lurambi. Wakazi wamesema mamake mwathiriwa alimwacha mvulana huyo katika nyumba hiyo na kuelekea katika soko la Bukura kwa biashara zake za kila siku kabla ya kufahamishwa kuhusu kuteketea kwa nyumba […]

JIANDAE KWA MVUA KUBWA, UTABIRI

Maeneo kadhaa nchini yametakiwa kujiandaa kwa vipindi vya mvua kubwa wiki hii huku maeneo mengi yakishuhudia vipindi vya ukame. Katika ripoti yake kuhusu kipindi cha kati ya leo na Jumatatu wiki ijayo, idara ya utabiri wa hali ya anga imesema maeneo kama vile Nairobi, ukanda wa Ziwa Victoria, Rift Valley na Magharibi mwa nchi yatashuhudia […]