MURKOMEN ATETEA ‘JUKWAA LA USALAMA’

Serikali imeendeleza juhudi zake za kuwahamasisha wakenya kuhusu jukumu lao la kuhakikisha usalama nchini mbali na kuchukua malalamishi ya wakenya kuhusu changamoto za kiusalama. Kwa sasa Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen yuko katika kaunti ya Kisii ambako anafanya kikao maarufu kama jukwaa la usalama, akitetea vikao hivyo dhidi ya shutuma kwamba vinatumika kufuja fedha za […]

RAIS RUTO AFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA TURKANA

Rais William Ruto ameendeleza vikao vyake vya mara kwa mara na viongozi wa mashinani kutoka maeneo mbali mbali nchini, ambako analenga kuwafahamisha kuhusu utendakazi wa serikali yake na miradi ya maendeleo ambayo serikali yake imetekeleza katika maeneo hayo. Mapema leo, rais amekutana na viongozi wa mashinani kutoka kaunti ya Murang’a, muda mfupi baada ya kuwaalika […]

DCI YAKANA ‘KUIBA’ DETA ZA WAKENYA

Idara ya upelelezi wa jinai DCI imepuzilia mbali taarifa zilizochapishwa kwenye gazeti moja nchini hii leo zikidai kwamba idara hiyo inatumia program maalum kupata deta za siri kwenye simu za wakenya. Kwenye taarifa, gazeti hilo limedai kwamba DCI iliweka program hiyo inayofahamika kama FlexiSpy kwenye simu za watengenezaji wa Makala ya Blood Parliament ya shirika […]

DABI YA MANCHESTER

Na hatimaye baada ya likizo ya kimataifa kwa ligi kuu ya uingereza wafuasi wa ligii hii wanasubiria weekend hii kwa mvuto mkubwa wakisubiria vilabu wanavyo enzi. Lakini mchezo mkubwa mabao unasubiriwa ni kati wa miamba wa wawili Manchester United na Manchester City almaarufu kama manchester derby  jumapili hii katiaka uwanja wa etihad. Miamba hawa Wawili […]

AKONNOR KUTUMIA MCHEZO WA SIMBA KUREKEBISHA KIKOSI

Kocha mkuu wa Gor Mahia Charles Akonnor anasema mechi ya Simba iliwapa mabingwa hao wa zamani wa Ligi Kuu ya FKF picha kamili ya walipo na nini cha kurekebisha kuelekea msimu mpya. Mchezo huo uliochezwa Jumatano kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, kuadhimisha siku ya Simba Day, ulishuhudia K’Ogalo wakiwachabangwa 2-0 kupitia kw amabao ya wachezaji […]

FAINALI YA DALA SEVENS

Itakua ni weekend ya kusisimua kwa wapenzi wa raga huku Mzunguko wa Kitaifa wa Saba 2025 wa Dala Sevens ukibisha lango katika kauti ya kisumu katika Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, Mamboleo, kuanzia Septemba 13-14. Huku KCB RFC na Strathmore Leos zikiwa kwenye vita vikali vya kuwania taji la jumla, macho yote yataelekezwa Kisumu […]

E-GP SI TAFADHALI, RUTO AONYA

Rais William Ruto amesisitiza kuwa mfumo wa utoaji zabuni za serikali kwa njia ya kielektroniki yaani e-Procurement ni lazima, licha ya pingamizi kutoka kwa viongozi mbali mbali wakiwemo magavana na maseneta wanaosema shughuli za kaunti zimekwama kutokana na mfumo huo. Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Rais Ruto amewakosoa wanaopinga mfumo huo, anaoutaja kuwa wenye kuhakikisha […]

USHAHIDI UNAOCHUNGUZWA NA DCI KWENYE MAUAJI YA WAKILI

Ripoti ya upasuaji wa maiti ya wakili Kyalo Mbobu iliyotolewa hapo jana ikionyesha kuwa alipigwa risasi mara 8 ni miongoni mwa vifaa vitakavyosaidia katika kuendesha uchunguzi kwenye mauaji ya wakili huyo. Mwanapatholojia mkuu wa serikali Johansen Oduor aliyeongoza upasuaji huo, amesema risasi 2 kati ya 8 zilikuwa zimekwama kwenye mwili wa mwendazake, na kwamba zimekabidhiwa […]

RUTO, WAKUU WA WALIMU IKULU

Viongozi wa miungano ya walimu nchini wameratibiwa kufanya kikao na Rais William Ruto hii leo katika Ikulu ya Nairobi ambako viongozi hao watapata fursa ya kuwasilisha malalamishi yao kwa rais moja kwa moja ikiwemo kucheleweshwa kwa mgao wa shule. Viongozi hao wamekariri kuwa mkutano huo utajikita kujadili matatizo yao kama vile suala la kupandishwa vyeo […]

BODA WAANGUKIWA NA MASHARTI MAGUMU

Wahudumu wa boda boda watahitaji usajili mpya unaoonyesha maeneo wanakohudumu, sare tofauti kulingana na kaunti ndogo wanazotoka miongoni mwa masharti mengine katika juhudi za kuidhibiti sekta hiyo ambayo imedhaniwa kuwa maficho ya wahalifu. Katika mkutano wa washikadau, iliafikiwa kwamba kila anayesajiliwa atahitajika kuwa na leseni ya uendeshaji wa magari, cheti cha tabia njema miongoni mwa […]