RUTO: AFRIKA HAITAKUBALI KUBAGULIWA UN

Rais William Ruto amewahimiza viongozi wa Afrika kuungana katika juhudi zao za kushinikiza mageuzi katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa. Rais ambaye yuko jijini New York kuhudhiria kikao cha 80 cha baraza kuu la umoja wa mataifa maarufu kama UNGA, amesema haitakubalika kwa Afrika kuendelea kubaguliwa katika baraza hilo. Amewataka viongozi hao kushinikiza […]

WAVINYA AKANA KUWA ‘KIZUIZI’ CHA MAENDELEO

Muungano wa magavana 3 kutoka kaunti za Ukambani umepuzilia mbali madai kwamba ndio wamekuwa wakiizuia serikali kuu kutekeleza miradi ya maendeleo eneo hilo. Mwenyekiti wa muungano huo Wavinya Ndeti ambaye pia ni gavana wa Machakos, ameyataja madai hayo kuwa yasiyo na msingi, akisema waliwasilsha mapendekezo ya miradi kwa serikali kuu jinsi walivyotakiwa ila hadi sasa […]

MARTINELI AIOKOLEA ARSENAL ALAMA, MAN U WAANGUKA NA CHELSEA

Bao la Gabriel Martinelli lilifufua matumaini ya Arsenal kupigania taji la ligi kuu ya Uingereza EPL baada ya kuwahakikishia sare ya bao 1 nyumbani Emirates dhidi ya Manchester City. City walikosa adabu ya mgeni kunako dakika 9 baada ya mshambulizi wao Erling Haaland kuwaweka kifua mbele kutokana na shambulizi la kushtukiza alilolianzisha katikati ya uwanja […]

SHABANA FC WAANZA LIGI KWA KISHINDO

Kocha mkuu wa klabu ya soka ya Shabana Peter Okidi, ameelezea kuridhishwa na ushindi wa mabao 4:2 dhidi ya limbukeni APS Bomet kwenye mechi ya ufunguzi iliyoandaliwa katika uwanja wa Gusii, akisema ni mwanzo mwema kwa msimu mpya wa 2025-26 Shabana walitawala kipindi kirefu cha mchuano huo, na kuchukua uongozi katika dakika ya 3 kupitia […]

CAF: POLICE FC WAWATIA PINGU WAGENI, NAIBOIS WAAMBULIA SARE

Mabingwa watetezi wa ligi kuu nchini KPL Kenya Police wameanzisha kampeni yao ya kusaka ubingwa wa bara Afrika kwa ushindi mnono wa mabao 3:1 dhidi ya Mogadishu City Stars wa Somalia katika mkondo wa kwanza kwenye mashindano ya klabu bingwa barani Afrika CAF Championship. Maafande hao ambao wanashiriki mashindano ya bara kwa msimu wa 2 […]

WANARIADHA WA KENYA WATIA FORA WAC

Wakenya walitia fora na kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Marekani kwenye mashindano dunia ya ubingwa wa riadha duniani yaliyokamilika hapo jana jijini Tokyo nchini Japan. Kenya ilipata jumla ya medali 11, zikiwemo dhahabu 7, fedha 2 sawa na shaba, nyuma ya Marekani waliojizolea jumla ya medal 26. Wakenya waliopata dhahabu ni Beatrice Chebet […]

WAGONJWA WALIOPONA WAZUILIWA MTRH

Akina mama 27 waliojifungua maajuzi wameendelea kuzuiliwa katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Moi jijini Eldoret baada ya kushindwa kulipa ada za matibabu. Kwenye kanda ya video iliyosagaa kwenye mitandao ya kijamii, akina mama hao, baadhi wakidai kuzuiliwa kwa zaidi ya miezi 3 licha ya kuwa katika hali nzuri, wameibua madai ya kupitishiwa katika […]

RUPHA YASITISHA HUDUMA ZA SHA HOSPITALINI

Wagonjwa wanaotegemea kulipiwa huduma za matibabu na mamlaka ya afya ya jamii SHA katika hospitali za kibinafsi watalazimika kulipa pesa taslimu baada ya hospitali hizo kukataa kutumia bima ya SHA. Kupitia taarifa, muungano wa hospitali hizo RUPHA umesema agizo hilo linaanza kutekelezwa hii leo, ukisema umechukua hatua hiyo baada ya SHA kuchelewesha malipo yao na […]

UPINZANI: HAKI KWA WAATHIRIWA KABLA YA FIDIA

Muungano wa upinzani umebuni kamati maalum itakayoangazia masuala ya waathiriwa wa maandamano watakaorodheshwa kufidiwa na jopokazi lililoteuliwa na Rais William Ruto. Haya ni kulingana na kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka akizungumza katika kaunti ya Kajiado, akiongeza kuwa muungano huo utahakikisha kwamba waathiriwa wanapata haki mwanzo kabla ya fidia. Alikuwa ameandamana na Waziri wa zamani Fred […]

WAUGUZI WASITISHA MGOMO TRANS NZOIA

Huduma za matibabu katika hospitali za umma kaunti ya Trans Nzoia zinatarajiwa kurejelea hali ya kawaida hii leo kufuatia kusitishwa kwa mgomo wa wauguzi ambao umedumu kwa zaidi ya mwezi mmoja. Hatua hiyo imejiri kufuatia mazungumzo ya kina kati ya muungano wa wauguzi KNUN na serikali ya kaunti hiyo, KNUN ikiongozwa na katibu mkuu tawi […]