Wabunge Nairobi wateta kuhusu uteuzi wa KDF

Jumla ya wabunge 18 kutoka kaunti ya Nairobi wamekosoa ratiba ya usajili wa makurutu wa kujiunga na jeshi la ulinzi KDF, wakisema ratiba hiyo inakiuka sheria kuhusu usawa na ujumuishaji jinsi ilivyo kwenye katiba. Kupitia waraka, wabunge hao wamesema kuwa vituo 3 pekee vya usajili ambavyo ni uwanja wa Nyayo, Kasarani na jamhuri Grounds ni […]

UASU, KUSU KIBABII WAGOMA

Mgomo wa wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma umelemaza masomo katika vyuo hivyo kwa siku ya pili, wahadhiri wakishinikiza kutekelezwa kwa mkataba wao na serikali kabla ya kurejea kazini. Katika kaunti ya Bungoma, wahadhiri wa chuo kikuu cha Kibabii wamejiunga na wenzao kote nchini, wakisema serikali imekuwa ikiwahadaa kurejea kazini ila inakosa kutekeleza makubaliano. Wafanyakazi […]

KENYA KUFANYA VYEMA KATIKA MASHINDANO YA KUOGELEA YA BARA

Kenya inatazamiwa kufanya vyema katika hatua ya bara wakati Mashindano ya Kuogelea ya Afrika Aquatics Zone 3 yatakapofika kwenye Uwanja wa Aquatic wa Kasarani mnamo Oktoba 16-19, 2025. Miongoni mwa wanaobeba matumaini ya taifa ni Alex Kaindi, kocha wa Genesis Sports Limited ambaye anaamini waogeleaji wake wako tayari kukabiliana na changamoto hiyo. Kaindi, mkufunzi aliyeidhinishwa […]

CHELSEA YARAMBWA HUKU LIVERPOOL IKINAWIRI

Harry Kane alifunga mabao mawili huku  Bayern Munich ikiilaza Chelsea 3-1 nyumbani kwenye mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Jumatano. Michael Olise alimshinikiza Trevoh Chalobah kujifunga dakika 20 kabla ya Kane kushinda na kufunga penalti dakika saba baadaye. Cole Palmer alimaliza shambulizi la kipekee la timu dakika mbili tu baadaye na kuirejesha Chelsea mchezoni. […]

NSL KWANZA MWISHONI MWA SEPTEMBER

Kuanza kwa Ligi Kuu ya Kitaifa ya FKF (NSL) ya 2025/26 kumeahirishwa kwa wiki moja hadi wikendi ya Septemba 27-28 baada ya vilabu na maafisa wa ligi kufikia uamuzi wa pamoja kufuatia mkutano jijini Nairobi Jumatano. Mkutano huo ulileta pamoja Kamati ya Ligi na Mashindano ya FKF (LCC) na wawakilishi wa klabu kukagua utendakazi wa […]

OJAL AJIVUNIA LICHA YA KUSHINDWA

Kocha mkuu wa Strathmore Leos, William Ojal ameelezea kufadhaika kwake baada ya timu yake kukosa taji la kitaifa la saba na kupoteza kwa KCB RFC katika fainali. Licha ya masikitiko hayo, Ojal alisema anajivunia kujitolea na uthabiti wa wachezaji wake katika msimu wote wa saba. Mtaalamu huyo amesifu kazi ya pamoja kuwa ndiyo chanzo cha […]

IEBC YALALAMIKIA UKOSEFU WA FEDHA

Chaguzi ndogo 8 zinazotarajiwa kuandaliwa mwezi Novemba mwaka huu ziko katika hatari ya kuahirishwa kutokana na ukosefu wa fedha za kufanikisha maandalizi ya chaguzi hizo. Akizungumza alipofika mbele ya kamati ya uhasibu katika bunge la kitaifa, mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC Erastus Ethekon, amesema hazina ya kitaifa haijatoa fedha za kutosha, […]

WANAFUNZI HEWA WAIPUNJA SERIKALI

Zaidi ya wanafunzi hewa 50,000 wamekuwa wakinufaika na mgao wa serikali wa shilingi elfu 15, uchunguzi ukionyesha kwamba baadhi ya shule ziliongeza idadi ya wanafunzi ili kuilaghai serikali. Haya ni kwa mujibu wa katibu mkuu katika elimu ya msingi Julius Bitok, akisema Sakata hiyo imesababisha kufujwa kwa mamilioni ya pesa. Bitok aliyasema haya akiwa mbele […]

MGOMO WA WAHADHIRI WAINGIA SIKU YA 2

Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma zinatarajiwa kusambaratika kwa siku ya 2 hii leo kufuatia mgomo wa wahadhiri licha ya serikali kutoka shilingi bilioni 2.5 kutatua malalamishi ya wahadhiri. Wahadhiri kupitia kwa miungano yao ya UASU na KUSU, wameshikilia kuwa hawatarudi kazini hadi makubaliano yao yam waka 2021-2025 na serikali yatakapotekelezwa kikamilifu. Walioathirika […]

Mastering Multi‑Currency Gaming and Mobile Payments at Top Online Casinos

Mastering Multi‑Currency Gaming and Mobile Payments at Top Online Casinos When you want to play on the go, you need more than a flashy interface. You need a safe site, fast deposits, and games that work in any currency. This guide shows you how to pick an online casino that meets those needs, step by […]