HATUA ZAPIGWA KATIKA UCHUNGUZI WA MAUAJI NAIROBI

Polisi wamesema wamepata kanda muhimu za video kutoka maeneo kadhaa yakiwemo majengo ya kibinafsi zinazoonyesha hatua za mwisho za wakili aliyeuawa jijini Nairobi Kyalo Mbobu, ambazo wanasema zitasaidia katika uchunguzi wa mauaji hayo. Kulingana na polisi, mwendazake alifanya mkutano kwa takribani saa 3 katika mkahawa mmoja kwenye barabara ya Milimani na watu ambao sasa wamejumuishwa […]

WAWAKILISHI WADI WA GUSII IKULU

Rais William Ruto anatarajiwa kuongoza kikao na wawakilishi wadi kutoka kaunti za eneo la Gusii ambazo ni Kisii na Nyamira, wakiongozwa na gavana Simba Arati kabla ya kuanza ziara yake katika eneo hilo. Mabunge ya kaunti hizo tayari yamesitisha vikao vyake ili kuwaruhusu wawakilishi wadi hao kuhudhuria kikao cha rais katika Ikulu ya Nairobi, huku […]

MASOMO YA VYUO VYA UMMA PEMBAMBA

Serikali ina muda wa siku 7 pekee kuingilia kati na kuangazia matakwa ya wahadhiri ili kuepusha kusambaratika kwa shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma nchini. Hii ni baada ya muungano wa wahadhiri nchini UASU kutoa notisi ya mgomo, ukiitaka serikali kutekeleza makataba wa maelewano la sivyo waanze mgomo kuanzia Septemba 17. Kulingana na […]

Why Win Diggers Slots Capture Players Better Than Other Online Casinos

Why Win Diggers Slots Capture Players Better Than Other Online Casinos Finding the right online casino can feel like digging for gold. Many sites promise huge jackpots, but few deliver an experience that truly sticks. One platform consistently rises above the rest: Win Diggers. It blends a massive 450% bonus, a deep game library, and […]

SERIKALI YA KIRINYAGA YATANGAZA AFUENI YA FIGO

Shughuli za matibabu katika hospitali ya Kerugoya kaunti ya Kirinyaga zinatarajiwa kurejelea hali ya kawaida baada ya kutatizika kutokana na kufeli kwa mashine za kuosha figo na kuwaacha wagonjwa taabani. Hii ni baada ya serikali ya kaunti hiyo kutangaza kwamba itaweka mashine mpya 25 katika hospitali hiyo na hospitali nyingine za kaunti hiyo, ikiwemo Sagana, […]

CAPEVERDE WALAZA CAMEROON

Cape Verde, taifa la visiwa vya Afrika Magharibi lenye wakaazi wasiozidi 550,000, liliishinda Cameroon 1-0 siku ya Jumanne na kuimarisha matumaini ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza. Blue Sharks wanahitaji pointi tatu mwezi Oktoba kutokana na mechi za ugenini dhidi ya Libya na nyumbani Eswatini kushinda Kundi D, ambalo Cameroon waliofuzu mara […]

MAONO YA MISRI KUFUZU KWA KOMBE LA DUNIA YASITISHWA

Jaribio la Misri la kufuzu kwa Kombe la Dunia lilisitishwa baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Burkina Faso katika mchezo wa Kundi A uliochezwa hapo jana. Kikosi cha Hossam Hassan ambacho hakijashindwa kilisonga hadi pointi 20 na kuongoza Kundi A kwa pointi tano mbele ya Burkina Faso, zikiwa zimesalia mechi mbili za kufuzu. Huku […]

ONYALA ANA MATUMAINI KUNYAKUA TAJI YA CIRCUIT

Nahodha wa KCB Rugby Vincent Onyala anasema shinikizo linapungua kwa upande wake wanapokaribia kutwaa taji la Taifa la 7s Circuit kufuatia ushindi mwingine wa kihistoria katika Kabeberi 7s. Wanabenki hao walikamilisha rekodi ya kutwaa taji la nne mfululizo la Kabeberi kwenye Uwanja wa RFUEA, ushindi huo uliwasukuma hadi kilele cha msimamo wa mzunguko wakiwa na […]

GOR MAHIA KUKUTANA NA SIMBA FC KWA MECHI YA KIRAFIKI

NAHODHA wa Gor Mahia, Philemon Otieno ametangaza kuwa kikosi chake kiko tayari mchezo wao wa hali ya juu wa kujiandaa na msimu mpya dhidi ya wababe wa Tanzania, Simba SC. Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wengi inatarajiwa kuchezwa  hii leo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Licha ya hali ya kutisha iliyotarajiwa jijini Dar, […]

WAMILIKI WA MAGARI WATAKA BODA BODA KUREKEBISHWA

Sekta ya boda boda imeendelea kujipata chini ya shinikizo zinazoitaka ifanyiwe mageuzi, wamiliki wa magari ya uchukuzi ikiitaka idara ya trafiki kuwawajibisha wahudumu wanaojihusisha na uhuni kwa kuwashambulia wenye magari yanayohusika kwenye ajali. Wito wa wamiliki hao unajiri baada ya magari 3 yaliyohusika kwenye ajali kuchomwa katika maeneo mbali mbali na watu wanaoaminika kuwa wahudumu […]