MAUAJI YA WAKILI YAIBUA MASWALI

Polisi jijini Nairobi wanachunguza mauaji ya kikatili ya wakili Kyalo Mbobu, aliyepigwa risasi na kuuawa papo hapo kwenye barabara ya Langa’ata na mtu aliyekuwa akitumia pikikipiki usiku wa kuamkia leo. Walioshuhudia wanasema wakili huyo alikuwa pekee yake kwenye gari hilo, mauaji hayo yakikosolewa na chama cha wanasheria nchini LSK ambayo imeyataja kuwa tishio kwa utendakazi […]

NIIA PANDA YA MAKURUTU 10,000

Huenda wakenya wanaolenga kusajiliwa kama makurutu wa kujiunga na idara ya polisi wakasubiri zaidi kutokana na mvutano kati ya idara ya polisi NPS na tume ya huduma za polisi NPSC. Licha ya idara ya polisi kulenga kuwasajili makurutu 10,000, mvutano umeibuka kati yake na NPSC hasa kuhusu ni nani mweney mamlaka ya kuendesha zoezi hilo, […]

GAVANA NDETI AWATIMUA MAAFISA ‘FISADI’

Gavana wa Machakos Wavinya Ndeti amewasimamisha kazi maafisa 33 wa idara ya kukusanya mapato kwa madai ya kuhusika na ufisadi. Hatua ya Ndeti inajiri kufuatia ongezeko la hofu kuhusu shughuli za udanganyifu, huku gavana huyo akiapa kusambaratisha shughuli hizo ili kuimarisha utoaji huduma kwa wakazi. Miongoni mwa hulka za udanganyifu ni madai ya maafisa hao […]

ALVAREZ APIGWA MARUFUKU MIEZI KUMI

Beki wa Athletic Bilbao Yeray Alvarez amepigwa marufuku ya miezi 10 baada ya kupatikana na dawa iliyopigwa marufuku kufuatia pambano la Ligi ya Europa dhidi ya Manchester United msimu uliopita, shirikisho la soka barani Ulaya UEFA lilisema Jumatatu. Uchambuzi wa sampuli iliyotolewa na mchezaji huyo baada ya mchezo mwezi Mei “ulifichua uwepo wa Canrenone,” dawa […]

HJULMAND ACHUKUA USUKANI BAYER LEVERKUSEN

Bayer Leverkusen Jumatatu ilimteua Dane Kasper Hjulmand kama kocha, akichukua nafasi ya Erik ten Hag, ambaye alifutwa kazi baada ya mechi mbili pekee za ligi. Kocha huyo wa zamani wa Denmark ameteuliwa kwa kandarasi hadi 2027. Uteuzi huo unamaliza siku mbili za machafuko kwa Leverkusen, ambayo ilimtimua meneja wa zamani wa Manchester United Ten Hag […]

HARAMBEE STARS WAREJEA UWANJANI

Harambee Stars itawakosa mabeki Alphonse Omija na Aboud Omar katika mechi ya leo ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya Ushelisheli. Haya mi kwa mujibu wa  kocha Benni McCarthy . Katika kikao na wanahabari Jumatatu katika uwanja wa moi Kasarani, McCarthy ameelezea matumaini yake kwamba timu hiyo itajikomboa kutokana na kichapo cha 3-1 dhidi […]

MAHAKAMA YATIA BREKI JOPO, E-GP

Serikali imepata pigo mara 2 mahakamani baada ya mahakama kuu ya Nairobi kusitisha kwa muda utekelezaji wa mfumo wa utoaji wa tenda za serikali wa e-GP, huku ile ye Kerugoya ikisitisha kwa muda utendakazi wa jopo la kuwafidia waathiriwa wa maandamano nchini. Katika uamuzi wao, majaji hao wamesema kuwa serikali haikufuata utaratibu katika kubuni jopo […]

KESI YA ‘ALIYEMUUA” RAIS YAENDELEA

Kesi ya mwanafunzi wa chuo kikuu David Mokaya anayetuhumiwa na mashtaka ya kulidanganya taifa kwa kuchapisha picha zinazoashiria kifo cha rais William Ruto inaendelea katika mahakama ya Milimani jijini Nairobi ambako mshtakiwa alikana mashtaka. Mwanafunzi huyo anadaiwa kuchapisha picha ya jeneza lenya bendera ya taifa na maandishi yanayoashiria mazishi ya rais, madai ambayo mawakili wanaomwakilisha […]

JUHUDI ZA SERIKALI BADO, WAKENYA

Kupungua kwa mapato miongoni mwa wakenya kupitia ushuru wa juu wanayotozwa kwenye mishahara yao ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili wakenya chini ya utawala wa Rais William Ruto ambaye anaadhimisha miaka 3 tangu kuingia madarakani. Kulingana na wakenya waliokuwa wakiangazia uongozi wa Kenya Kwanza, mipango ya serikali ya kulinda uchumi ikiwemo mbolea ya ruzuku na udhibiti […]

MSAKO WAIMARISHWA NAIROBI

Washukiwa wa wizi wa kimabavu zaidi ya 300 jijini Nairobi ambao wamekamatwa kufikia sasa wanatarajiwa mahakamani hii leo kufunguliwa mashtaka mbali mbali, baada ya kukamatwa wakati wa operesheni maalum iliyoagizwa na serikali. Polisi wamewataka waathiriwa wa uhalifu huo katikati mwa jiji la Nairobi kuandikisha taarifa ili kusaidia katika uchunguzi na kufanikisha mashtaka dhidi ya washukiwa. […]