USALAMA KUIMARIKA KERIO VALLEY

Juhudi za serikali za kurejesha utulivu katika eneo la Kerio Valley zimeendelea kuzaa matunda, baada ya jamaa mmoja aliyekiri kuwa mhalifu sugu kujisalimisha kwa polisi akitangaza kwamba ameasi Maisha ya uhalifu. Mwanaume huyo, kwa jina la Arthur Komen mwenye umri wa miaka30, alijiwasilisha katika kituo cha polisi cha Tot kaunti ya Elgeyo Marakwet alikopeana bunduki na risasi kabla ya kukabidhiwa kwa viongozi […]

KRA YAOKOA MAMILIONI YA FEDHA MOMBASA

Mamlaka ya ya ukusanyaji wa ushuru nchini KRA imezuia jaribio la kulaghai serikali zaidi ya shilingi milioni 123 za kodi kupitia uidhinishaji usiofaa wa Konteina 161 ya mchele katika kituo cha Konteina cha Mombasa. Kupitia taarifa, KRA imesema kuwa ulaghai huo uliofanyika kati ya tarehe 1 na 23 Agosti mwaka huu ulitambulika wiki jana baada ya ukaguzi ambao huratibiwa na kwamba uchunguzi […]

COMOROS KWENYE UKINGO WA HISTORIA, STARS WAZIMWA

Katika mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la soka mwaka wa 2026, timu ya taifa ya Morocco ndio timu pekee kati ya 9 zinazotarajiwa kufuzu barani Afrika, ambayo imefuzu kushiriki mashinadano hayo huku ikifuatiwa kwa ukaribu na timu ya Misri. Comoros nao hapo jana wameongeza matumaini yao ya kushiriki mashindano ya kombe hilo kwa mara ya kwanza mwaka ujao baada […]

POLICE FC WAJIANDAA KWA KAGAME CUP

Mabingwa wa ligi kuu ya Kenya, Kenya Police wameelzea matumaini yao ya kupata ushindi katika robo fainali ya kombe la CECAFA Kagame dhidi ya ya klabu ya Ethiopian Coffee FC, mechi ambayo imeratibiwa kuchezwa leo jijini Dar-es-Salaam, Tanzania. Akizumgumza kuhusu mechi hiyo, Nahodha wa Police FC David Ochieng maarufu kama Cheche amesema kuwa wamejiandaa vilivyo na wana matarajio makubwa ya […]

KCB RFC NDIO MABINGWA WA KABEBERI 7S

Klabu ya raga ya KCB RFC imevikwa taji la kombe la Kabeberi 7s hapo jana baada ya ushindi wao wa mabao 20-10 dhidi ya Daystar Falcons katika uwanja wa RFUEA. KCB ambao walionyesha ukakamavu wao uwanjani kwa kulinda ushindi wao, sasa wamjiongezea alama 22 na wanaongoza kwa alama 104 ambazo ni alama 9 zaidi ya wanaoshikilia nambari ya pili, Strathmore Leos. […]

WAKENYA WAMWOMBOLEZA MBUNGE WA ZAMANI

Viongozi na wakenya kutoka matabaka mbali mbali wameendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa mbunge wa Rongo na Waziri Dalmas Otieno aliyefariki hapo jana akiwa na umri wa miaka 80 baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kupitia ujumbe, Rais William Ruto amemwomboleza Otieno kama kiongozi mwenye maono aliyelitumikia taifa kwa maadili, huku kinara wa ODM Raila Odinga […]

SIKU KUBWA YA MUUNGANO WA UPINZANI

Muungano wa upinzani umeratibiwa kutangaza jina na nembo yake rasmi hii leo utakaotumia katika chaguzi ndogo za mwezi Novemba na uchaguzi mkuu ujao huku ukisisitiza kuwa utamteua mgombeaji mmoja atakayemenyana na Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu ujao. Kulingana na viongozi wa muungano huo wakiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, mashauriano yanaendelea katika juhudi […]

MAAFISA 8 NAKURU KUHOJIWA NA EACC

Tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC imewaagiza maafisa 8 wa sasa na wa zamani katika serikali ya kaunti ya Nakuru kufika mbele yake hii leo ili kuhojiwa kuhusu madai ya matumizi mabaya ya fedha za umma. Miongoni mwa maafisa hao ni mwanasheria wa kaunti hiyo Caleb Nyamwage na afisa mkuu katika wizara ya utumishi […]

SHULE 29 ZAFUNGWA GATUNDU KUTOKANA NA MOTO

Shughuli za masomo katika shule 29 za bweni katika eneo la Gatundu South kaunti ya Kiambu zimekwama baada ya shule hizo kufungwa kwa muda usiojulikana kutokana na msururu wa visa vya moto, zikiwa ni wiki chache tangu kuanza kwa muhula wa 3. Wanafunzi wasiopungua 25 wanaohusishwa na uchomaji wa shule hizo wamekamatwa, washikadau mbali mbali […]

MABADILIKO YA GHAFLA YAHOFIWA KUATHIRI BIASHARA

Mabadiliko ya sera yasiyotabirika nchini Kenya huenda yakapunguzaimani ya wawekezaji licha ya kuwepo kwa masoko yenye nguvu kifedha narufaa ya kikanda.Mwenyekiti wa chama utoaji mtaji kwa wawekezaji wa kibinafsi David Owinoamesema kuwa ijapokuwa Afrika Mashariki inasalia  kuwa pahali penyekuwavutia wawekezaji wenye mtaji binafsi, kanuni za kighafla zimetishiakuondoa uaminifu wa wawekazaji .Aidha, Owino amesisitiza kuwa serikali inafaa kuimarisha kanuni ilikuwahakikishia wawekezaji […]