KAULI YA SHOLLEI

Naibu spika wa bunge la kitaifa Gladys Shollei amehoji kuwa uchaguzi ndogo unaotarajiwa kufanyika maeneo mbalimbali ni mtihiani muhimu kwa makamishina wapya wa  tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC walioteuliwa hivi karibuni. Akizungumza na kituo kimoja cha runinga nchini Shollei amependekeza kuwa chaguzi hizo zinawapa maafisa hao wa IEBC fursa ya kuimarisha utendekazi na […]

BENKI YA DUNIA YAPANDISHA MAKADIRIO YA UKUAJI WA UCHUMI KENYA

Benki ya Dunia imeinua makadirio ya ukuaji wa uchumi wa 2025 wa Kenya hadi asilimia 4.9, marekebisho ya juu kutoka asilimia 4.5 mwezi Mei, na kuweka historia mpya kabisa kwa nchi ya kenya. Katika ripoti yake ya Marekebisho ya Uchumi wa Kenya mjini Nairobi, mkopeshaji huyo wa kimataifa amesema kuwa mfumuko mdogo wa bei, kurahisisha sera […]

MAN U WAPIGWA NA WACHEZAJI 10

Matumaini ya Manchester United kushiriki dimba la klabu bingwa bara Ulaya msimu ujao yamepigwa breki na kichapo cha goli 1-0 na Everton ugani Old Trafford usiku wa kuamkia leo. Bao la pekee la mchezo lilifungwa na Kiernan Dewsbury-Hall dakika ya 29, baada ya Idrissa Gueye wa Everton kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 13, wakilazimika kulinda […]

GOR WALENGA KUDUMISHA UONGOZI

Mabingwa mara 21 wa ligi kuu ya Kenya KPL Gor Mahia, watalenga kuendeleza uongozi wa ligi hiyo watakapovaana na APS Bomet saa kumi alasiri hii leo. Gor walio na mechi 2 mkononi, wanaongoza ligi kwa pointi 19, 1 mbele ya Kakamega Homeboyz na 5 mbele ya mahasimu wao wa jadi AFC leopards walio katika nafasi […]

JUNIOR STARLETS ROBO FAINALI

Timu ya taifa ya soka kwa vijana wasiozidi umri wa miaka 17 Junior Stars wameweka guu moja ndani ya semifainali ya kipute cha kufuzu dimba la mataifa bingwa barani Afrika AFCON U17 mkondo wa CECAFA baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya South Sudan ugani Abebe Bikila nchini Ethiopia. Derrick Wanyonyi alianzisha ufungaji […]

DEAFLYMPICS: WAMBUI AVUNJA REKODI YA DUNIA

Mkenya Ian Wambui aliiletea nchi fahari katika mashindano ya wanariadha wasio na uwezo wa kusikia ya Tokyo 2025 Summer Deaflympics, akivunja rekodi ya dunia aliposhinda nishani ya dhahabu katika mbio za mita 5,000 kwa wanaume. Wambui alikamilisha mbio hizo kwa muda wa dakika 13, sekunde 52.83, na kuvunja rekodi ya dakika 14, sekunde 2.90 iliyowekwa […]

SERIKALI YAAHIDI USALAMA UCHAGUZINI

Serikali imewahakikishia wapiga kura kwamba usalama umeimarishwa katika maeneo yote ambako uchaguzi mdogo umeratibiwa kufanyika Alhamisi wiki hii ikiwemo eneo bunge la Mbeere North ambako vurugu zimekuwa zikishuhudiwa. Akizungumza kwenye msururu wa kampeni eneo hilo, naibu Rais Kithure Kindiki amekariri kuwa vitendo vya vurugu havitavumiliwa na serikali. Kindiki aidha ametetea utendakazi wa serikali eneo hilo. […]

IEBC YAKANA KUIBA UCHAGUZI

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imepuzilia mbali madai kuhusu uwepo wa udanganyifu katika uchaguzi mdogo wa Magarini kaunti ya Kilifi, ikitoa hakikisho kuwa uchaguzi huo utafanywa kwa njia ya uadilifu na uwazi. Kupitia taarifa, IEBC imekiri kupokea malalamishi rasmi kutoka kwa kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua kuhusu njama ya wizi wa […]

KAMPENI ZA CHAGUZI NDOGO KIKOMO

Kampeni za chaguzi ndogo katika maeneo mbali mbali ya taifa zimekamilika rasmi huku macho yote sasa yakielekezwa kwa tume ya IEBC kuona jinsi itakavyoendesha chaguzi hizo Alhamisi wiki hii, hasa kutokana na madai kwamba tume hiyo imeonyesha miegemeo ya kisiasa. Miongoni mwa maeneo kutakakofanyika chaguzi hizo ni wadhifa wa useneta kaunti ya Baringo, maeneo bunge […]

OMTATAH MAHAKAMANI KUPINGA KITUO CHA IEBC

Seneta wa Busia Okiya Omtatah amewasilisha kesi mahakamani akitanga mahakama itoe agizo kwamba tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imekuwa ikikiuka katiba kwa kuanzisha na kuendesha kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura, chenye uwezo wa kuhakiki, kubadilisha au kujumlisha upya matokeo ya urais. Kwenye kesi yake, Omtatah amekariri vipengee vya 86 na 138 vya […]