SHUJAA WAIMARISHA JUHUDI ZA KUPANDISHWA DARAJA HSBC

Timu ya taifa ya raga ya wachezaji 7 kila upande, Shujaa, imefunga mkondo wa pili wa mashindano ya HSBC SVNS divisheni ya pili kwa ushindi, baada ya kuwatandika wenyeji Uruguay 22-14 usiku wa manane. Kwa jumla, Shujaa wameandikisha ushindi mara 3 na kupoteza mechi 2, ushindi mwingine ukijiri dhidi ya Canada na Ubelgiji. Baada ya […]

RUTO AAHIDI MAENDELEO ZAIDI NYANZA

Rais William Ruto ameahidi kuliimarisha kiuchumi eneo la Nyanza, analosema limebaguliwa kwa muda mrefu na serikali zilizopita. Akizungumza katika kaunti ya Homa Bay alikozindua miradi ya maendeleo, amekariri kuwa atatekeleza ruwaza walioafikiana na aliyekuwa Waziri mkuu marehemu Raila Odinga. Amewataka wakazi kuwatathmini viongozi kwa misingi ya maendeleo. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAKAZI WA BWAWA LA NAIROBI WATAKIWA KUHAMA

Wakazi wanaoishi maeneo ya chini ya bwawa la Nairobi kama vile Kibra, Lang’ata, South C na Madaraka wametakiwa kuhama kufuatia kupanda kwa kiwango cha maji kwenye bwawa hilo, ambayo yanahofiwa kusababisha maafa. Kwenye tahadhari yake, mamlaka ya raslimali za maji, WRA, imesema kiwango hicho kimefikia hali ya hatari, na kuwataka wakazi kuhamia maeneo salama mapema, […]

POLISI WACHUNGUZA MIILI 14 KWENYE KABURI LA PAMOJA

Maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai DCI wanaendelea kutegua kitendawili kuhusu ni vipi miili 14 isiyojulikana ilizikwa katika kaburi moja eneo la Makaburini kaunti ya Kericho Ijumaa asubuhi. Kwa mujibu wa wapelelezi, walipata taarifa kutoka kwa vijana 2 wa kurandaranda mitaani wanaodai watu 3 walifika eneo hilo Ahamisi na kufanya mazungumzo na usimamizi wa […]

LINDA MWANANCHI YATAKA POLISI WALIOWAVURUGA KUKAMATWA

Viongozi wa chama cha ODM wanaoegemea mrengo wa Linda Mwannchi, wametaka hatua mwafaka kuchukuliwa dhidi ya maafisa wa polisi waliowarushia viongozi hao vitoza machozi na kuvuruga mkutano wao mjini Narok hapo jana. Wakiongozwa na seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, mwenzake wa Vihiga Godfrey Osotsi, gavana wa Siaya James Orengo, na mbunge wa Embakasi East Babu […]

EPL: MAN UNITED VS BOURNEMOUTH USIKU WA LEO.

Ligi kuu ya Uingereza inarejea usiku wa leo huku Manchester United wakisafiri Bournemouth katika mechi ya mkondo wa 31. United ambao wamekua na matokeo mazuri hivi karibuni wanatarajiwa kuendeleza fomu hiyo nzuri. Hapo kesho Brighton watakua wenyeji wa Liverpool huku Everton wakivaan na Chelsea kisha Fulham wapambane na Burnley. Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

KOCHA MPYA WA MOROCCO APONGEZA UAMUZI WA CAF

Kocha mpya wa taifa la Morocco, Mohamed Ouahbi, amewapongeza wachezaji wake Abaada ya uamuzi wa CAF kutoa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 kutoka kwa Senegal na kuwapa Morocco. Senegal ilishinda fainali Januari 18 mjini Rabat kwa mabao 1-0, lakini CAF iliamua kuwapokonya wachezaji wa Senegal taji baada ya wachezaji hao kuondoka uwanjani kwa ishara […]

KORIR ATAKA SERIKALI KUWEKEZA KWENYE MICHEZO YA NDANI

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana katika Athletics Kenya, Barnabas Korir, ameitaka serikali kuendelea kwa uthabiti katika maendeleo ya miundombinu ya michezo ya ndani ili kuhakikisha wanariadha wa Kenya wanabaki kuwa washindani duniani. Korir ameyasema hayo kabla ya mashindano ya 2026 World Athletics Indoor Championships, akisisitiza kuwa kikosi cha Kenya chenye wanariadha wanane kitangaza ushindi. Aidha, […]

UJENZI WA UWANJA WA KISASA WAZUA MATUMAINI VIHIGA

Furaha imeenea kwenye sekta ya michezo katika Kaunti ya Vihiga kufuatia ahadi kubwa ya kushughulikia changamoto za muda mrefu za miundombinu ambazo zimekuwa zikikwamisha maendeleo ya michezo. Matumaini hayo yamechochewa na uzinduzi wa ujenzi wa uwanja wa kisasa wenye thamani ya shilingi milioni 900 katika eneo la Kidundu, mradi ambao wadau wa michezo tayari wameutaja kuwa […]

PVK YASUTA SERIKALI KUHUSU MAFURIKO

Muungano wa Pentecostal Voice of Kenya umetoa taarifa ukisoa jinsi serikali inavyoshughulikia janga la mafuriko linaloendelea, ukilitaja kuwa ni “kushindwa kwa kitaifa”. Wakiongozwa na Mwenyekiti na Kiongozi wa Kanisa la Jesus Teaching Ministry Apostle Peter Manyuru Muungano huo umetuma rambirambi kwa familia zilizopoteza wapendwa wao na kuonyesha mshikamano na maelfu ya waliokosa makazi kote nchini. Viongozi hao wa kanisa […]