MURKOMEN AWATAKA VIONGOZI KUSHIRIKIANA NA POLISI  WAKATI WA SIASA

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, amewataka viongozi wa kisiasa nchini kuwa huru kuwasiliana na idara ya polisi kuhusu ratiba ya mikutano yao ili kuhakikishiwa usalama wakati wa mikutano hiyo. Akizungumza kwenye kikao cha mashauriano na tume ya IEBC kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao, Murkomen amesisitiza kuwa suala la usalama ni jukumu […]

IEBC YAONYA VIJANA DHIDI KUSHIRIKI VURUGU WAKATI WA UCHAGUZI

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini  IEBC imewataka vijana kujiepusha na uhalifu ikiwaonya wanasiasa dhidi ya kuwatumia vijana kuzua vurugu wakati wa uchuguzi. Akizungumza wakati wa kikao cha mashauriano na washikadau mbalimbali mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon ameweka wazi kuwa tume hiyo haitasita kuwachukulia hatua za kisheria viongozi hao bila kujali iwapo wapo mamlakani […]

KESI DHIDI YA OKOTH OBADO YATUPILIWA MBALI

Aliyekuwa  gavana wa Migori Okoth Obado  watoto wake wanne pamoja na washirika wao wameondolewa mashtaka ya ufisadi wa shilingi milioni 73.5 baada ya mahakama ya kukabiliana na ufisadi ya milimani  kuruhusu ombi la mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya  umma la kuondoa kesi hiyo kufuatia makubaliano ya nje ya mahakama. Katika uamuzi wake hakimu Celisa Okore […]

OPIYO WANDAYI AELEZA SABABU ZA KUPANDA KWA BEI YA MAFUTA

Waziri wa Kawi na Petroli Opiyo Wandayi amesema ongezeko la bei ya mafuta nchini limechangiwa na hali ya soko la kimataifa kufuatia mvutano unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati huku akiwahakikishia Wakenya kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta na hakuna uhaba unaotarajiwa kwa sasa. Wandayi amesema serikali ina  mpango   wa kuhakikisha mafuta yanaingia nchini bila changamoto […]

ARTETA ASISITIZA MIFEREJI YA MABAO KULENGA UBINGWA

Kocha mkuu wa Arsenal Mikel Arteta, amewataka vijana wake kuwabebesha Burnley mzigo wa mabao watakapokutana Jumatatu kwenye mechi yao ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza EPL, wanapolenga ubingwa wa ligi hiyo kwa mara ya kwanza katika muda wa miaka 22 iliyopita. The Gunners wako mbele ya Manchester City na pointi 2 zikiwa zimesalia mechi […]

AFCON U17: SA WAPAMBANIA USHINDI, TZ YASHINDA ANGOLA IKISHIKILIA MALI

Timu ya taifa ya Afrika Kusini ilitoka nyuma na kuandikisha ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Senegal katika mechi yao ya ufunguzi kwenye dimba la mataifa bingwa barani Afrika kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17, AFCON U17. Mashindano hayo yaliyoanza Jumatano wiki hii, yataendelea hadi mwanzoni mwa mwezi ujao nchini Morocco. Senegal walitishia kuwatia […]

KIVUMBI CHA FKF CUP

Jumla ya timu nne zitashuka dimbani hapo kesho kuwania nafasi ya kufuzu fainali ya kombe la FKF, mechi zote 2 zikiratibiwa kusakatwa katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi. Katika semi fainali ya kwanza, Tusker FC walioshinda kombe hilo mara ya mwisho msimu wa 2021-22, watapambana na KCB FC huku Tusker wakipigiwa upato wa kunyakua kombe […]

KESI YA GACHAGUA KUENDELEA MEI 22

Kesi ya kushinikiza fidia kwa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua itaendelea Ijumaa wiki ijayo huku naibu Rais Kithure Kindiki akiiomba mahakama kutupilia mbali kesi hiyo ambapo Gachagua anataka kupewa malipo ya muhula mzima ambayo angepokea iwapo hangetimuliwa kutoka afisini. Kupitia kwa wakili wake, Kindiki amesema kulipwa fidia kwa mtangulizi wake kutahujumu uamuzi wa seneti kumwondoa […]

BEI YA PETROLI, DIZELI YAVUKA SH.200

Wakenya kwa mara nyingine watalazimika kugharamika zaidi kwa mahitaji ya kila siku baada ya serikali kuongeza bei ya mafuta ya petroli kwa shilingi 16.65 kwa kila lita huku dizeli ikiongezeka kwa shilingi 46.29 kwa kila lita, bei hizo mpya zikitekelezwa kwa kipindi cha siku 30 zijazo. Kwa mujibu wa mamlaka ya kudhibiti kawi na petroli […]

MWANIAJI WA UDA AIBUKA MSHINDI EMURUA DIKIRR

Mgombeaji wa ubunge katika eneo bunge la Emurua Dikirr kupitia tiketi ya chama tawala cha UDA David Keter, ametangazwa mshindi wa kiti hicho kwenye uchaguzi mdogo ulioandaliwa hapo jana, baada ya kujizolea jumla ya kura 18,266. Kulingana na tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, mgombeaji wa DCP Vincent Rotich alimaliza wa pili akiwa na […]