MAN CITY WAWATIA ARSENAL KWENYE TANURI NA KICHAPO KWA PALACE

Manchester City waliandikisha ushindi rahisi wa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace licha ya kocha mkuu Pep Guardiola kukichezesha kikosi cha akiba, na kuwatia viongozi wa EPL, Arsenal kwenye tanuri la moto. Guardiola alifanya mabadiliko 6 ya kikosi kilichowalaza Brentford mabao 3-0 wikendi iliyopita, na kuwaacha nje wachezaji wake mahiri kama vile Erling Haaland, Jeremy […]

OKETCH KUCHUANA NA NASER ANAPOONJA DIAMOND LEAGUE

Mshikilizi wa rekodi ya kitaifa katika mbio za mita 400 Mercy Oketch, anajiandaa kwa kinyang’anyiro cha kupimana nguvu kwa mara ya kwanza katika mbio za Diamond League Jumamosi hii jijini Shanghai, Uchina. Akiwa anashiriki kwa mara ya kwanza kwenye mbio hizo, Oketch atapambana na wanariadha wenye kasi zaidi ulimwenguni, akiwemo bingwa mara tatu wa fainali […]

INGWE WAKWARUZA ULINZI, WAWEKA HAI MATUMAINI YA UBINGWA

Matumaini ya Ulinzi Stars kujiondoa katika eneo la kushushwa daraja yalizimwa jana baada ya kukwaruzwa na AFC Leopards kwa kichapo cha mabao 2-0 na kuwaacha wanajeshi hao miongoni mwa timu 3 ambazo sasa zinakabiliwa na hatari ya kuiaga ligi kuu ya soka, KPL mwishoni mwa msimu. Shambulizi la kiungo wa Rising Stars Kelly Madada katika […]

KENYA YAANZISHA JUHUDI ZA KUMPIGIA DEBE JAJI NDUNG’U

Serikali ya Kenya imezindua rasmi juhudi za kumtafutia uungwaji mkono Jaji wa Mahakama ya upeo Njoki Ndung’u katika azma yake ya kuwania nafasi katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu, ICC. Rais William Ruto ameagiza Wizara ya masuala ya kigeni kuanzisha kampeni ya kimataifa ya kuhakikisha Kenya inapata nafasi hiyo ya uwakilishi. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SING’OEI ATETEA UTOAJI WA PASPOTI KWA RSF

Wizara ya masuala ya kigeni imetetea kujihusisha kwa serikali katika juhudi za upatanishi nchini Sudan huku ikiendelea kukabiliwa na madai ya utoaji wa paspoti za usafiri kwa baadhi ya maafisa wa ngazi ya juu wa kundi la wapiganaji la RSF. Kwenye mahojiano na shirika moja la habari, katibu mkuu katika wizara hiyo Korir Sing’oei, amesisitiza […]

UDA, DCP KUTOANA KIVUMBI EMURUA DIKIIR 

Wakazi katika eneo bunge la Emurua Dikiir wameendelea kujitokeza kushiriki uchaguzi mdogo wa kumchagua mbunge wao kumrithi marehemu Johanna Ng’eno aliyewaongoza tangu mwaka 2013 eneo bunge hilo lilipobuniwa. Zoezi la upigaji kura limeanza mapema leo, huku wapiga kura wapatao 44,000 wakitarajiwa kushiriki zoezi hilo linalowaniwa na wagombeaji watano, kivumbi kikali kikiwa baina ya UDA na […]

WAZEE WA VIJIJI KUPATA TABASAMU

Serikali imetangaza pendekezo la kuwalipa mshahara wa shilingi 3,000 kila mwezi wazee wa vijiji kote nchini, ambao ni takribani 110,000 kama njia mojawapo ya kutambua mchango wao katika mfumo wa utawala nchini. Akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu utawala na usalama, katibu mkuu katika wizara ya masuala ya ndani Raymond Omollo, amesema wazee walio […]

OPARANYA APONGEZA WAKENYA KWA KULIPA HUSTLER FUND    

Waziri wa vyama vya ushirika Wycliffe Oparanya anasema kiwango cha ulipaji wa mkopo wa hustler fund kimeimarika pakubwa na kufikia asilimia tisini. Akijibu maswali ya maseneta katika bunge la seneti hii leo, Oparanya amekiri kwamba kiwango cha kutolipa mkopo huo kilikuwa juu pindi ulipozinduliwa japo anakariri kwamba kila mkenya aliyekopa pesa hizo ataandamwa ili alipe. […]

BEATRICE WANGARI AACHILIWA KUHUSIANA NA KIFO CHA OBWAKA

Mwanamke anayehusishwa na kifo cha mwenyekiti wa Bodi ya Nairobi hospital   Daktari Dr John Obwaka ameachiliwa huru huku uchunguzi kuhusu kifo hicho ukiendelea. Jaji wa mahakama kuu Daiana Kavenza amemwachilia huru Beatrice Wangari kwa bondi ya binafsi ya shilingi laki moja baada ya mahakama kubaini kwamba hakuna ushaidi wa kutosha wa kuendelea kumzuilia zaidi. Akitoa […]

DAKTARI GIKONYO AHOJIWA MAHAKAMANI KATIKA  KESI YA GACHAGUA

Kesi ya kusikizwa kuondolewa Mamlakani aliyekuwa Naib Rais Rigadhi Gachagua inasikizwa Mahakamani Daktari wa magonjwa ya moyo Daniel GiKonyo  amedhibitisha kupokea simu kutoka kwa Rais William Ruto aliyetaka kujua hali ya kiafya ya aliyekuwa Naib Rais Rigadhi Gachagua baada ya kukimbizwa hospitalini wakati wa kusikizwa kwa hoja ya kumung’atua ofisini  katika  bunge la seneti. Akizungumza […]