GACHAGUA, SIFUNA WADOKEZA KUSHIRIKIANA

Aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua na katibu mkuu wa ODM Edwin Sufuna, wamedokeza kuhusu uwezekano wa kushirikiana kwenye uchaguzi mkuu ujao katika azma yao ya kumng’oa mamlakani Rais William Ruto. Wakizungumza katika kaunti ya Nyeri, wawili hao wamesema muungano wa upinzani utalazimika kuzika tofauti zao iwapo unalenga kutimiza azma hiyo. Kauli yao inajiri huku utafiti […]

WIZARA YA ELIMU YALALAMIKIA MGAO FINYU

Serikali imekiri uwezekano wa kutatizika kwa utoaji wa huduma za elimu ya kiufundi nae elimu ya juu nchini kutokana na uhaba wa fedha, ikisema shilingi bilioni 19 zinahitaji ili kufadhili utoaji wa elimu hiyo. Akiwa mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu elimu, katibu mkuu katika idara ya masomo ya TVET, Daktari Esther Mworia, […]

ARNE SLOT ATHIBITISHA KUSALIA LIVERPOOL

Kocha wa Liverpool FC, Arne Slot, amethibitisha kuwa ataendelea kuinoa klabu hiyo msimu ujao huku akisema tayari anahusika katika mipango ya usajili wa wachezaji wapya. Slot amesema ana mkataba na Liverpool na mazungumzo yanayoendelea ndani ya klabu yanaonyesha wazi kuwa atasalia kuwa kocha wa kikosi hicho msimu ujao. Kauli hiyo imewapa matumaini mashabiki wa Liverpool […]

JUNIOR STARLETS KAMBINI KABLA YA KUVAANA NA UGANDA

Mshambuliaji wa Junior Starlets, Faith Boke, amesema kikosi hicho kina imani ya kuichapa Uganda katika mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia la Wanawake chini ya miaka 17. Kenya watavaana na Uganda katika mechi ya kwanza Mei 22 katika uwanja wa FUFA Stadium kabla ya marudiano kuchezwa Mei 30 katika Nyayo National Stadium. Starlets walifika […]

MUYOTI AIPA POLICE IMANI DHIDI YA BANDARI 

Kocha mkuu wa Kenya Police FC, Nicholas Muyoti, amesema ana imani kikosi chake kitaibuka na ushindi watakapovaana na Bandari FC katika nusu fainali ya kombe la Mozzart Bet siku ya Jumamosi. Muyoti amewataka wachezaji wake kubaki makini, wenye nidhamu na kudhibiti presha ya mchezo huo utakaochezwa katika Nyayo National Stadium. Mshindi wa mashindano hayo atawakilisha […]

ULINZI STARS WAPIGANIA NAFASI KUBAKI KPL

Kocha mkuu wa Ulinzi Stars, Mulinge Ndeto, amewataka wachezaji wake kucheza kwa ari ya ushambuliaji huku wakisaka kusalia katika Ligi Kuu ya Kenya. Ndeto amesema mechi tatu zilizobaki ni kama fainali kwa timu hiyo. Ulinzi walipoteza mabao 2-0 dhidi ya AFC Leopards katika uwanja wa Nyayo National Stadium na kubaki nafasi ya 16 wakiwa na […]

BEI MPYA YA MAFUTA KUTANGAZWA LEO

Wakenya wakisubiri bei mpya ya mafuta kutangazwa hii leo,serikali imetoa shilingi bilioni sita kwa wauzaji wa mafuta  kufidia udhibiti wa bei za  bidhaa hizo  za mwezi uliopita kabla ya kutangazwa kwa makadirio ya bei za  mafuta leo hii . Kulingana na wauzaji bei ya petroli huenda ikapanda iwapo gharama zilizobebwa na waagizaji wa mafuta zitazingatiwa  […]

DCP YAPANDA KWA UMAARUFU, UDA NA ODM KWENYE MTEREMKO

Uungwaji mkono wa Chama cha DCP chake aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua umeongezeka kutoka asilimia 6 mwezi Novemba mwaka jana hadi asilimia 16 mwezi Mei mwaka huu. Hii ni kulingana na utafiti wa kampuni ya TIFA ikionyesha jinsi ambavyo chama hicho kimekuwa kwa kasi zaidi. Utafiti huo pia unaonyesha kupungua kwa umaarufu wa vyama vya […]

TIFA SURVEY: RUTO AONGOZA MBIO ZA URAIS NA 24%

Rais William Ruto anaongoza katika mbio za urais kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 kulingana na utafiti uliofanywa na kampuni ya TIFA. Kulingana na utafiti huo, Ruto anaongoza kwa asilimia 24 ya uungwaji mkono akifuatwa na Kalonzo Musyoka aliye na asilimia 19 kisha Fred Matiangi akiwa na asilimia 14. Wengine ni pamoja na seneta wa […]

WABUNGE WAHOFIA BAJETI FINYU YA MASHIRIKA YA UTALII 

Wabunge wameibua wasiwasi kuhusu kutengwa kwa mashirika muhimu ya utalii kwenye bajeti inayopendekezwa ya 2026/27, wakionya kuwa hatua hiyo inaweza kusitisha ajenda ya ukuaji wa utalii nchini Kenya. Kamati ya Bunge ya Kitaifa ya Utalii na Wanyamapori inahoji ni kwa nini Mashirika kadhaa ya Serikali ya Semi-Autonomous (SAGAs) chini ya Idara ya Utalii hayakupata mgao licha […]