XABI ALONSO AHUSISHWA NA UHAMISHO WA LIGI KUU YA UINGEREZA

Kocha Xabi Alonso ameripotiwa kufungua uwezekano wa kuhamia Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu wa kiangazi baada ya mawasiliano ya awali kufanywa kupitia mawakala wake. Chelsea inadaiwa kuwa na orodha ya makocha wanaowafikiria, huku wakifuatilia upatikanaji wa Alonso pamoja na Andoni Iraola ambaye anataka kuendelea kubaki katika Ligi Kuu ya Uingereza. Hata hivyo, bado hakuna […]

MATHARE UNITED YATANGAZA KUONDOKA KWA KOCHA JOHN KAMAU

Mathare United imetangaza kuondoka kwa kocha mkuu John Kamau huku mechi tatu pekee zikisalia kabla ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu ya FKF 2025/2026. Klabu hiyo imesema Kamau ataondoka mara moja kutoka nafasi yake ya ukocha huku Kocha msaidizi Mohammed Mchulla akipewa jukumu la kuiongoza timu hiyo kwa muda katika mechi zilizobaki za msimu huu. Hatua hiyo […]

OGOLLA ASIKITISHWA NA MIGOGORO NDANI YA FKF

Aliyekuwa mchezaji wa kimataifa wa Kenya na kocha wa soka John Bobby Ogolla ameonyesha masikitiko yake kuhusu migogoro inayoendelea ndani ya FKF. Shirikisho hilo limekumbwa na mivutano ya uongozi kati ya Rais Hussein Mohamed, naibu wake MacDonald Mariga pamoja na wanachama wengine wa kamati kuu, huku madai ya ubadhirifu wa fedha za bima ya mashindano […]

OMANYALA AJIANDAA KWA MBIO KALI SHANGHAI

Mwanariadha Ferdinand Omanyala anatarajiwa kushiriki mojawapo ya mbio ngumu zaidi msimu huu atakapowania mbio za mita 100 katika mashindano ya Diamond League Shanghai mwishoni mwa wiki hii. Nyota huyo wa mbio fupi anaingia katika mashindano hayo akiwa katika kiwango kizuri baada ya kufanya vyema katika mashindano mbalimbali barani Afrika. Omanyala alianza msimu wa mwaka 2026 […]

MVUA KUBWA YAENDELEA KUSHUHUDIWA TRANS NZOIA

Wakazi wa wadi ya Kiptoro- Chepsiro kaunti ya Trans Nzoia wametakiwa kuchukua tahadhari kutokana na ongezeko la watu kufa maji eneo hilo, watu wawili wakiripotiwa kufariki katika muda wa wiki moja iliyopita. Naibu chifu wa Kiboswa Gilbert Chepsiror, amesema kisa cha hivi punde kinamhusisha mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo, aliyeripotiwa kujirusha katika mto Moiben unaounganisha […]

ODM YATANGAZA NAFASI ZA KUSAJILI WANACHAMA WA SIASA

Chama cha ODM kimefungua rasmi maombi ya uteuzi kwa wanasiasa wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi  mkuu wa mwaka wa 2027 kupitia tiketi ya chama hicho. ODM  imewaalika  wanachama kutoka kote nchini kuwasilisha maombi yao kabla ya tarehe 30 Juni mwaka huu. Nafasi zilizotangazwa ni pamoja na Urais, ugavana, useneta, ubunge,  uwakilishi wa wanawake pamoja […]

ELIMU YA KENYA INAENDELEA KUWA GHALI

Wakazi wa eneo la Machakos wanaitaka serikali ya Rais William Ruto kuangazia gharama ya elimu nchini wakisema kuwa masomo ya CBE yamekuwa ghali hswa wakati huu ambao uchumi wa taifa unaonekana kuzorota. Wakizungmza hii leo katika kaunti ya Machakos  wakaazi hao wamewarai  viongozi  wanaohusika na  mgao wa  pesa za kupiga jeki masomo nchini yaani bursary […]

YOWERI MUSEVENI AAPISHWA

Yoweri Kaguta Museveni ameapishwa rasmi  hii leo kuwa Rais wa taifa la Uganda kuhudumu kwa muhula wa  saba  katika hafla iliyofanyika uwanjani Kololo jijini Kampala. Hafla hiyo imeudhuriwa na viongozi mbalimbali wa bara la Afrika akiwemo Naib Rais Kithure Kindiki, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mwenzake wa Sudan Kusini Salbakir Mayaordid, Rais wa Somalia […]

ANTONIO GUTERES AWATAKA VIONGOZI WA AFRIKA KUBUNI NJIA ZA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOKUMBA DUNIA

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guteres ametoa wito kwa viongozi wa  Afrika kuwa mstari wa mbele katika kutafuta suluhisho kwa changamoto zinazokumba dunia ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi. Akihutubu katika kongamano linaloendelea la Africa Forward Summit, Guters amepigia debe haja ya sauti ya Afrika kuzingatiwa katika maamuzi muhimu duniani. Imetayarishwa na Hilda Ajema

RAIS RUTO ATAJA NAFASI YA AFRIKA KATIKA MIFUMOYA KIAMATAIFA

Rais William Ruto ameendelea kusisitiza nafasi ya Afrika katika mifumo ya kimataifa pamoja na changamoto zinazokabili bara hili katika sekata ya Afya na maendeleo. Akizungumza katika kongamano la Africa Forward Summit linaloendelea kwa siku ya pili jijini Nairobi, Rais Ruto amesema Afrika lazima ipate sauti sawa katika maamuzi ya kimataifa na kupunguza utegemezi wa misaada. […]