RUTO AZINDUA KANGAMANO LA ELIMU NAIVASHA

Rais William Ruto amesisitiza mageuzi makubwa katika sekta ya elimu nchini, akieleza kuwa serikali inalenga kuhakikisha mfumo wa elimu unalenga ujuzi, ubunifu na mahitaji ya soko la ajira. Katika hotuba yake mjini Naivasha Ruto ametaja umuhimu wa taifa kueka  mkazo kwenye ubora wa ufundishaji na mazingira bora ya kujifunzia ili kuinua viwango vya kitaaluma kwa wanafunzi wote nchini Ameahidi […]

UKUAJI WA VIWANDA NCHINI WAPUNGUA… CHANZO?

Msukumo wa taifa la kenya wa kuwa na viwanda maarufu zaidi unarudishwa nyuma na miundombinu dhaifu na mapungufu ya ujuzi, kufuatia ripoti mpya ya bara la afrika. Ripoti ya RED 2025 ya Maendeleo ya Viwanda barani Afrika na Baraza la Biashara la Afrika imetoa taarifa kwamba wakati Kenya ina nguvu katika ufadhili wa kidijitali na muunganisho, haina misingi muhimu inayohitajika kusaidia ukuaji wa viwanda. Kenya ina […]

NEYMAR, ROBINHO JR WAPATANA HADHARANI KUFUATIA KOFI

Nguli wa soka nchini Brazil Neymar Jr amemwomba msamaha hadharani mchezaji mwenza wa klabu ya Santos Robinho Junior baada ya kumzaba kofi kinda huyo wakati wa mazoezi. Klabu ya Santos ilisema kwamba imeanzisha uchunguzi kufuatia makabiliano kati ya Neymar na Robinho Junior, ambaye ni mwanawe mshambulizi wa zamani wa klabu ya Real Madrid na Manchester […]

PSG YAILAZA BAYERN KUWEKA MIADI NA ARSENAL FAINALI

Mabingwa watetezi wa ligi ya mabingwa bara Ulaya, Paris St-Germain, watamenyana na viongozi wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza kwenye fainali ya kombe hilo, baada ya kuandikisha ushindi katika awamu ya semi fainali. PSG waliilaza Bayern jumla ya mabao 6-5, licha ya sare ya bao 1-1 jana usiku kufuatia ushindi wa mabao 5-4 kwenye […]

APS BOMET YAIMARISHA NAFASI YA KUSALIA LIGI KUU

Timu ya APS Bomet ilipiga hatua kubwa katika juhudi zake za kukwepa kushushwa daraja mwishoni mwa msimu, kufuatia ushindi wao mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya KCB FC ugani Green Stadium jana alasiri. Mshambulizi wa maafande hao wa utawala alifunga bao hilo la pekee la mchezo katika dakika ya 29 na kuwapa Black Berets uongozi […]

ORENGO: ODM KUBWA KWA UDA, DEBENI TUPO

Viongozi wa ODM wanaoegemea mrengo wa Linda Mwananchi wamesisitiza kuwa ni sharti chama hicho kiwe na mgombeaji wa urais kwenye uchaguzi mkuu ujao, kwa misingi kwamba ODM ndicho chama kikubwa kiliochosalia nchini. Kwenye mahojiano na shirika moja la habari, gavana wa Siaya James Orengo, amedai kuwa mrengo wa seneta wa Siaya Oburu Oginga umekuwa ukifanya […]

IPOA YACHUNGUZA MAUAJI LUANDA

Mamlaka ya kitaifa inayoangazia utendakazi wa polisi IPOA, imeanzisha uchunguzi katika kifo cha mtu mmoja katika eneo la Luanda kaunti ya Vihiga polisi waliponasa pikipiki 20 zinazohusishwa na wizi. Wakati wa tukio hilo la hivi majuzi, wakazi walipinga kunaswa kwa pikipiki hizo na kuifunga barabara kuu ya Kisumu-Busia na kusababisha ghasia, walipojaribu kuvamia kituo cha […]

VIONGOZI TRANS NZOIA WALALAMIKIA ‘MSAKO WA KISIASA’

Huku kikosi maalum cha polisi kikiendeleza msako dhidi ya magenge ya wahalifu katika kaunti ya Trans Nzoia, imeibuka kwamba operesheni hiyo inakiuka haki za kimsingi za raia. Akizungumza na wanahabari baada ya maafisa wake wakuu 2 kukamatwa kwa kuhusishwa na uhalifu, gavana wa kaunti hiyo George Natembea, amesema operesheni hiyo imekiuka sheria na kuwalenga wakosoaji […]

KCCPS YAFUNGA MFUMO WA KUTUMA MAOMBI

Zoezi la wanafunzi waliofanya mtihani wa KCSE mwaka jana kutuma maombi ya kusajiliwa katika vyuo vikuu nchini kupitia KUCCPS limefungwa rasmi usiku wa kuamkia leo, ikibainika kuwa idadi kubwa ya wanafunzi walichagua kozi mbali mbali ila hawakukamilisha mchakato wa kutuma maombi yao. Afisa mkuu mtendaji wa KUCCPS Dr. Mercy Wahome, ameweka wazi kwamba kuchagua kozi […]

COTU YAPUUZILIA MBALI PENDEKEZO LA GACHAGUA

Muungano wa Vyama vya Wafanyakazi nchini Kenya COTU  umetoa wito kwa serikalikuimarisha maslahi ya wafanyakazi huku ukisema kupanda kwa gharama ya maishakumeendelea kuongeza mzigo kwa maelfu ya familia za wafanyikazi nchini. Akizungumza katika kikao na wanahabari, Naibu katibu Mkuu wa muungano huo BensonOkwaro amepuuzilia mbali pendekezo la aliyekuwa Naibu rais Rigadhi Gachagua lakuzinduliwa kwa muungano mpya […]