KRU YAWEKA MKAKATI WA KUIMARISHA RAGA YA WANAWAKE

Mwenyekiti wa chama cha Raga nchini Harriet Okach amesema kuwa kujenga utamaduni imara na endelevu wa rugby ya wanawake ni kipaumbele cha muda mrefu, huku akilenga kuinua mchezo wa wa wachezaji 15s kufikia kiwango cha mafanikio ya Sevens nchini Amesema mashindano ya Rugby Africa Cup yanayofanyika jijini Nairobi yanatoa nafasi muhimu ya ushindani na maendeleo, yakishirikisha Kenya, mabingwa watetezi […]

BIASHARA HARAMU YA NYAMA YA PUNDA YAENDELEA KAJIADO

Biashara haramu ya nyama na ngozi za punda imeendelea kushamiri nchini licha ya serikali kupiga marufuku uchinjaji wa kibiashara wa wanyama hao mwaka 2020. Katika eneo la Kimuka, wakazi walinasa lori lililokuwa likisafirisha nyama inayoshukiwa kuwa ya punda pamoja na ngozi zake kabla ya kuwashambulia watu wawili waliokuwa ndani ya gari hilo. Kamanda wa Polisi […]

WADAU WAPINGA BAADHI YA VIPENGELE VYA MSWADA WA FEDHA 2026

Wadau wanaoshiriki vikao vya maoni kuhusu Mswada wa Fedha 2026 wameilaumu serikali kwa kushindwa kurekebisha viwango vya ushuru wa mishahara maarufu kama PAYE pamoja na kuanzisha ushuru mpya kwa miamala ya fedha kupitia simu. Wakizungumza mbele ya Kamati ya Fedha na Mipango ya Bunge la Taifa la Kenya, Taasisi ya Wahasibu Walioidhinishwa Kenya (ICPAK) pamoja na Muungano […]

RUTO KULIHUTUBIA TAIFA HII LEO

Rais William Ruto anatarajiwa kulihutubia taifa wakati wowote kuanzia sasa huku Wakenya wakisubiri kwa hamu kauli yake kuhusu changamoto za kiuchumi zinazoendelea nchini. Tangazo hilo limetolewa na msemaji wa Ikulu Hussein Mohamed ambaye amesema Rais atazungumza na wananchi lakini hakufafanua ajenda kamili ya hotuba hiyo. Hotuba hiyo inajiri wakati nchi ikikabiliwa na shinikizo la kupanda kwa bei […]

NAULI ZAPANDA LICHA YA MAZUNGUMZO

Wasafiri kote nchini wanakabiliwa na gharama kubwa za usafiri baada ya nauli kupanda licha ya wadau wa sekta ya matatu kuahidi kutopandisha bei wakati mazungumzo yanaendelea. Hapa  jijini Nairobi baadhi ya nauli zimeongezeka kwa hadi asilimia 50 kufuatia matamshi ya awali ya waendeshaji wa usafiri wa umma. Serikali imetakiwa kushughulikia suala la bei ya mafuta huku baadhi ya viongozi […]

WANGA A ANDIKA BARUA YA HISIA KWA ORENGO

Gavana wa Kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga ameandika barua ya wazi yenye hisia kwa Gavana wa Kaunti ya Siaya James Orengo akisema kauli zake za hivi karibuni zilimuumiza na kumfedhehesha. Katika taarifa hiyo, Wanga amesema anaongea kama mtu binafsi na si kama Gavana wa Homa Bay wala kama mwenyekiti wa chama cha ODM. Amesema alikaa […]

ORENGO ASEMA MAISHA YAKE YAKO HATARINI

Gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo amesema maisha yake yako hatarini baada ya serikali kuondoa walinzi wake bila maelezo. Akizungumza na kituo kimoja humu nchini, Orengo amesema Inspekta Jenerali wa Polisi anapaswa kuwajibika iwapo jambo lolote litamtokea. Orengo amesema maafisa wake tisa wa usalama waliokuwa wakimhudumia katika kaunti za Siaya na Nairobi waliondolewa ghafla Jumatano jioni bila sababu […]

RUTO KUKUTANA NA WADAU WA SEKTA YA USAFIRI

Rais William Ruto ameanza ziara ya maendeleo ya wiki moja katika eneo la Pwani huku shinikizo likiongezeka la kuzuia mgomo mpya wa kupinga bei ya mafuta. Ruto aliyerejea nchini kutoka ziara rasmi katika mataifa ya Azerbaijan na Kazakhstan, anatarajiwa kukutana na wadau wa sekta ya usafiri kujadili ongezeko la gharama za mafuta na athari zake kwa uchukuzi. Wawakilishi wa […]

UEFA YAPANGA MFUMO MPYA WA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2030

UEFA imetangaza mfumo mpya wa kufuzu kwa kombe la dunia mwaka 2030 utakaoiga mfumo unaotumika katika UEFA Champions League. Mfumo huo utakuwa na ngazi mbili ambapo mataifa 36 bora yatawekwa katika Ligi ya Kwanza na kugawanywa kwenye makundi matatu yenye timu 12 kila moja. Timu zitacheza mechi sita dhidi ya wapinzani tofauti, huku mataifa yatakayomaliza juu yakifuzu […]

AUSTIN ODHIAMBO AAMINI HARAMBEE STARS WAKO TAYARI

Kiungo Austin Odhiambo amesema Harambee Stars iko tayari kukabiliana na mataifa makubwa barani Afrika katika kufuzu kwa AFCON 2027. Kenya imepangwa kundi moja na Afrika Kusini , Guinea pamoja na Eritrea katika kundi linalotajwa kuwa gumu. Licha ya Kenya kufuzu moja kwa moja kama mwenyeji pamoja na Uganda na Tanzania, timu hiyo itashiriki mechi za kufuzu ili kujiweka […]