#Football #Sports

HANSEL OCHIENG’ AWEKA MALENGO MAKUBWA GOR MAHIA

Mshambuliaji mpya wa Gor Mahia, Hansel Ochieng’, amesema lengo lake la kwanza ni kuisaidia klabu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya FKF katika msimu wa 2026/27.

Ochieng’ pia amesema anatamani kuifikisha Gor Mahia hatua za juu za Ligi ya Mabingwa barani Afrika na kuchangia mafanikio ya klabu hiyo kimataifa.

Mshambuliaji huyo amesaini mkataba wa miaka miwili na mabingwa hao wa Kenya baada ya kujiunga kutoka APS Bomet, akiwa pia amewahi kuzichezea AFC Leopards, Kakamega Homeboyz na Nairobi City Stars.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *