NTSA YAFUTILIA MBALI LESENI ZA MADEREVA 62
Mamlaka ya kitaifa inayosimamia usalama barabarani NTSA imefutilia mbali leseni za madereva 62 kutoka kampuni 7 za magari ya uchukuzi wa umma baada ya ukaguzi uliobaini kuwa madereva hao wamekiuka sheria za usalama.
Kupitia taarifa, NTSA imesema madereva hao watahitajika kufanya majaribio mapya ya uendeshaji wa magari kabla ya kuamuliwa iwapo watarejeshewa leseni zao au la.
Aidha, mamlaka hiyo imeziagiza kampuni zilizoathirika kuwapa madereva wao wote uhamasisho kuhusu usalama wa barabarani.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































