#Local News

NATEMBEYA AIBUKA MAARUFU MAGHARIBI

Ulingo wa kisiasa Magharibi mwa Kenya umechukua mkondo tofauti, utafiti ukionyesha kuwa wenyeji sasa wamewaasi viongozi wa siku nyingi eneo hilo na kuwakumbatia viongozi wa kizazi kipya.

Kulingana na matokeo ya utafiti wa shirika la Infotrak yaliyotolewa hapo jana kuhusu umaarufu wa viongozi wa eneo hilo, gavana wa Trans Nzoia George Natembeya anapendelewa na asilimia 32 ya wakazi, akiwapiku spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula na mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi.

Kwenye utafiti huo wa mwezi jana, seneta wa Nairobi Edwin Sifuna pia amepata umaarufu zaidi eeno hilo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

NATEMBEYA AIBUKA MAARUFU MAGHARIBI

MATOKEO YA KCSE KUTANGAZWA LEO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *