#Local News

RAIS AONGOZA UZINDUZI WA MRADI WA NYOTA MOMBASA

Vijana katika kaunti ya Mombasa wamepatiwa fedha za kuanzisha biashara kupitia Mradi wa Nyota katika hafla iliyoongozwa na Rais William Ruto jijini Mombasa.

Kupitia mpango huo, vijana walipokea ruzuku ya shilingi elfu ishirini na tano kila mmoja kama mtaji wa kuanzisha au kukuza biashara zao.

Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kutoka kaunti za Mombasa, Kwale na Taita Taveta kwa kuwapa mtaji na fursa za kujiajiri ili kuboresha maisha yao kiuchumi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *