KAMATI YA BUNGE YAIDHINISHA FEDHA KULIPA MADENI YA NHIF
Kamati ya Bunge ya Afya imeidhinisha ombi la Wizara ya Afya la kutenga shilingi milioni 5.3 kusaidia kulipa madeni ya Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa (NHIF) yanayodaiwa na vituo mbalimbali vya afya.
Hatua hiyo inalenga kupunguza mzigo mkubwa wa madeni unaoathiri vituo vya afya vinavyodai serikali, hali inayochangia kudorora kwa utoaji wa huduma za afya nchini.
Wabunge wamesema kuwa kulipwa kwa madeni hayo kutasaidia kuboresha utoaji wa huduma na kuimarisha sekta ya afya kote nchini.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































