WAATHIRIWA WA MAFURIKO TRANS NZOIA WATAKA KUHAMISHWA
Waathiriwa wa mafuriko katika eneo la Namanjalala, kaunti ya Trans Nzoia, wanataka kuhamishiwa katika maeneo salama kufuatia athari kubwa za mafuriko.
Wakazi hao wanasema maisha yao yako hatarini huku wakikosa makazi ya kudumu baada ya mafuriko kuharibu makazi yao.
Mafuriko hayo yalisomba nyumba pamoja na mali zao, na kuwaacha wengi bila makazi wala mahitaji ya msingi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































