NG’ETICH NA EBENYO KUONGOZA SIRIKWA CLASSIC

Bingwa wa Dunia wa mbio za nyika, Agnes Ng’etich, na mshindi wa nishani ya fedha ya mita 10,000 kwenye Mashindano ya Dunia 2023, Daniel Ebenyo, wataongoza toleo la tano la Sirikwa Classic Cross Country Tour litakalofanyika Jumamosi, Februari 14 mwaka huu mjini Eldoret Nyota hao wawili wanatarajiwa kushiriki wakiwa bado kwenye kiwango bora kufuatia maonyesho yao […]

KAHATA AWEKA MATUMAINI KWA KCB

Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia, Francis Kahata, ameonyesha matumaini kuwa bao lake la kwanza litakuwa mwanzo wa mafanikio mema kwa klabu yake mpya huku nusu ya pili ya ligi ikianza. Kiungo huyo mkongwe alipachika bao wakati KCB iliposhinda Posta katika ushindi muhimu uliopatikana kwenye Uwanja wa Kasarani Bao hilo lilikuwa la kwanza la ligi […]

KIZZA BESIGYE AHAMISHWA HOSPITALINI KUFUATIA HALI MBAYA YA AFYA

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Dkt. Kizza Besigye, aliondolewa gerezani na kukimbizwa hospitalini baada ya afya yake kudorora na kufikia hali hatari usiku wa kuamkia Jumanne. Besigye, kiongozi wa PFF, amekuwa gerezani kwa muda na alipokuwa akikimbizwa hospitalini, msafara wake uliandamana na maafisa wengi wa usalama. Chama chake kimeshutumu serikali kwa kumnyima Besigye huduma bora […]

BABU OWINO AKANUSHA USHIRIKIANO NA GACHAGUA

Mbunge wa Embakasi Mashariki, Babu Owino, amekanusha madai kuwa anatafuta aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, kwa lengo la kushirikiana naye kisiasa, huku akisisitiza kuwa nia yake ni kuchukua uongozi ndani ya chama cha ODM. Owino amesema lengo lake kuu ni kuvutia kura kutoka kwa jamii zote jijini Nairobi ili kutimiza azma yake ya kuwania ugavana, […]

OGAMBA AWAOMBA WAZAZI KURIPOTI SHULE ZINAZOKIUKA SHERIA

Waziri wa Elimu, Julius Ogamba, amewataka wazazi kuripoti shule zinazowalazimisha kununua sare au vifaa vya masomo kutoka kwa wauzaji maalum, akisisitiza kuwa hatua za kisheria zinaweza kuchukuliwa tu pale malalamishi yanapoungwa mkono na ushahidi. Wito huo unajiri huku malalamishi yakiongezeka kutoka kwa wazazi wa wanafunzi wa Gredi 10 kuhusu gharama kubwa ya sare za shule na madai […]

AFISA WA POLISI AKUMBATIA MTI KERICHO

Kulishuhudiwa kioja katika Kaunti ya Kericho baada ya afisa wa ngazi ya juu katika idara ya polisi kuamua kukumbatia mti, mtindo ambao umechukuliwa na baadhi ya Wakenya kama njia ya kudhihirisha uhamasisho. Kennedy Wanjala ambaye ni afisa msimamizi wa Kituo cha polisi cha Sosiot Eneo bunge la Belgut alisema alichukua hatua hiyo kama njia ya kulalamikia dhuluma […]

WAWILI WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI KAKAMEGA

Watu wawili wamepoteza maisha kwa kupigwa risasi, huku mtu wa tatu akiendelea kupokea matibabu hospitalini akiwa na majeraha mabaya ya risasi, kufuatia makabiliano kati ya wakazi wa kijiji cha Mukulusu na maafisa wa Huduma ya Misitu ya Kenya  katika eneo la Shinyalu, Kaunti ya Kakamega. Vurugu hizo zilianza baada ya mzozo kuzuka kuhusu njia ambayo […]

RUTO AAGIZA HATIMILIKI YA SOKO LA GIKOMBA

Rais William Ruto ameagiza hatimiliki ya Soko la Gikomba jijini Nairobi kutolewa ndani ya siku 90 akisema soko hilo liko kwenye ardhi ya umma na kwamba kutoa hatimiliki kwa jina la Kaunti ya Nairobi kutatatua suala la umiliki wake mara moja Akitoa kauli hiyo wakati wa mkutano na wafanyabiashara wa Soko la Gikomba uliofanyika katika Ikulu ya […]

NCIC YAONYA WANASIASA KUHUSU UCHOCHEZI

Tume ya Taifa ya Mshikamano na Utangamano (NCIC) imewaonya wanasiasa dhidi ya kuwachochea Wakenya katika vitendo vya vurugu. Akizungumza jijini Nairobi wakati wa uzinduzi wa nyaraka mbili muhimu zinazolenga kudhibiti matamshi ya chuki, Mkurugenzi wa NCIC anayesimamia Uchunguzi na Uzingatiaji wa Sheria, Profesa James Wanyande, alisema haitakuwa shughuli kama kawaida, akisisitiza kuwa wahusika wa chuki […]

UBOMOAJI MUKURU WAATHIRI WAKAAZI

Mamia ya wakaazi wa Mukuru kwa njenga eneo la Embakasi Kusini wameachwa bila makao baada ya ubomoaji wa makaazi wa eneo hilo katika kile kilchotajwa kuwa ni sehemu ya upanuzi wa barabara. Wakaazi hao waligadhabishwa na hatua hiyo huku Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja akijitenga na shughuli hiyo akisema Serikali ya kaunti haikutoa amri ya […]